Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 9,409
- 14,156
Habari za week end wadau?
Naomba tusaidieni kimawazo kwa hili;
Kuna mshikaji wangu, nimemsoma ana tabia fulani ambayo nashindwa kuielewa lakini kwa kuwa nimeileta hapa jamvini nitasaidiwa kimawazo... jamaa nilikutana naye kama miezi sita iliyopita nilikuwa na tatizo na simu yangu na yeye ni customer care katika kampuni ya Airtel, baada ya kufika pale alinisaidia tatizo langu nikaondoka, mida ya jioni nilipita Bar kupata moja moja bahahti nzuri tukakutana nae basi tukaendelea kukata maji tukabadilishana namba za simu tangu hapo tukawa tunawasiliana.
Kuna kipindi alisafiri kwenda Arusha alipokuwa kule alinipigia simu anashida na kiasi cha pesa kama Laki Moja nikampatia alikaa kama mwezi na siku kadhaa akarudi, matokeo yake hakuniambia chochote akanyamaza tu, na mimi sikumuuliza chochote.
Siku nyingine tena tulikuwa tunapata moja moja alikuwa na demu wake, akawa ameishiwa cash akaenda Bank lakini karibu ATM nyingi za jirani zilikuwa hazifanyi kazi akanipiga tena mzinga nikampa elfu 50, akaondoka na demu wake.
Siku iliyofuata akanilipa sh elfu 30 akasema nyingine atanipa siku inayofuata, matokeo yake hatukuonana karibu wiki mbili, na nilipokuja kuonana nae hakusema chochote.
Tukaenda kupata nyama choma na lager kama kawa siku hiyo alilipa bili yote yeye, baada ya hapo mimi nikaenda zangu home na yeye akaenda zake kwake. Last week ijumaa usiku nikamkuta Bar yupo na demu wake nikajoin nao tukapiga lager na nyama choma baadae akasema twendeni club, tukaenda club.
Baada ya kufika club demu wake akawa anataka wine, na yeye hakuwa na cash ya kutosha maana tulikuwa tayari tupo fiti kichwani na mimi sikutaka kumwangusha nikampa elfu 25 akachukua chupa ya wine kwa ajili ya demu wake. Ilipofika time ya kurudi home akalipa taxi, kila mtu akaenda zake home, kesho yake asubuhi nikamtumia sms nikamkumbushia hela zote ninazomdai hakunijibu akakaa kimya hakujibu kitu.
Leo mchana demu wake kanipigia simu anaomba shiling elfu 35 kaambiwa na jamaa yake achukue kwangu akirudi jioni atanirudishia na mimi nikampotezea, nikamwambia sipo around mpaka jioni. Nimekaa jioni nimepigiwa tena simu nikamwambia nipo kwa washikaji nitamcheki.
Wadau, tukiwa kama familia moja hapa JF hasa jukwaa hili naomba ushauri wenu maana jamaa simuelewi, ni miezi sita nimejuana nae lakini ana tabia ya kukopa na huwa harejeshi halafu kitu kingine yeye ni mfanyakazi kampuni ya simu Airtel ina maana hana rafiki au jamaa anaofahamiana nao?
Naomba tusaidieni kimawazo kwa hili;
Kuna mshikaji wangu, nimemsoma ana tabia fulani ambayo nashindwa kuielewa lakini kwa kuwa nimeileta hapa jamvini nitasaidiwa kimawazo... jamaa nilikutana naye kama miezi sita iliyopita nilikuwa na tatizo na simu yangu na yeye ni customer care katika kampuni ya Airtel, baada ya kufika pale alinisaidia tatizo langu nikaondoka, mida ya jioni nilipita Bar kupata moja moja bahahti nzuri tukakutana nae basi tukaendelea kukata maji tukabadilishana namba za simu tangu hapo tukawa tunawasiliana.
Kuna kipindi alisafiri kwenda Arusha alipokuwa kule alinipigia simu anashida na kiasi cha pesa kama Laki Moja nikampatia alikaa kama mwezi na siku kadhaa akarudi, matokeo yake hakuniambia chochote akanyamaza tu, na mimi sikumuuliza chochote.
Siku nyingine tena tulikuwa tunapata moja moja alikuwa na demu wake, akawa ameishiwa cash akaenda Bank lakini karibu ATM nyingi za jirani zilikuwa hazifanyi kazi akanipiga tena mzinga nikampa elfu 50, akaondoka na demu wake.
Siku iliyofuata akanilipa sh elfu 30 akasema nyingine atanipa siku inayofuata, matokeo yake hatukuonana karibu wiki mbili, na nilipokuja kuonana nae hakusema chochote.
Tukaenda kupata nyama choma na lager kama kawa siku hiyo alilipa bili yote yeye, baada ya hapo mimi nikaenda zangu home na yeye akaenda zake kwake. Last week ijumaa usiku nikamkuta Bar yupo na demu wake nikajoin nao tukapiga lager na nyama choma baadae akasema twendeni club, tukaenda club.
Baada ya kufika club demu wake akawa anataka wine, na yeye hakuwa na cash ya kutosha maana tulikuwa tayari tupo fiti kichwani na mimi sikutaka kumwangusha nikampa elfu 25 akachukua chupa ya wine kwa ajili ya demu wake. Ilipofika time ya kurudi home akalipa taxi, kila mtu akaenda zake home, kesho yake asubuhi nikamtumia sms nikamkumbushia hela zote ninazomdai hakunijibu akakaa kimya hakujibu kitu.
Leo mchana demu wake kanipigia simu anaomba shiling elfu 35 kaambiwa na jamaa yake achukue kwangu akirudi jioni atanirudishia na mimi nikampotezea, nikamwambia sipo around mpaka jioni. Nimekaa jioni nimepigiwa tena simu nikamwambia nipo kwa washikaji nitamcheki.
Wadau, tukiwa kama familia moja hapa JF hasa jukwaa hili naomba ushauri wenu maana jamaa simuelewi, ni miezi sita nimejuana nae lakini ana tabia ya kukopa na huwa harejeshi halafu kitu kingine yeye ni mfanyakazi kampuni ya simu Airtel ina maana hana rafiki au jamaa anaofahamiana nao?