Wadau: Epuka uchumba wa muda mrefu

Wadau: Epuka uchumba wa muda mrefu

I greet you all JF members,

Kuna watu wanakaa katika mahusiano ya uchumba kwa miaka kibao bila kuishi maisha ya ndoa rasmi, kutokana na utafiti wangu(naruhusu ukosoaji) angalau mkiwa na uhusiano wa uchumba kwa kipindi cha kuanzia miezi sita mpaka mwisho isizidi miaka miwili angalau mnaweza kufunga ndoa.

Kwakuwa mtakuwa mmeshajuana na mmeshakuwa marafiki wazuri na mapenzi yanakuwa kwenye peak.

Sasa shida inatokea mkikaa mda mrefu zaidi ya huo mda mnakuwa mmezoeana mnoo,upendo/mapenzi yanapungua, mmoja baina yenu lazima atajisikia anapotezewa mda kwakuwa naamini sio kila mtu atakuwa anapenda kuendelea kusubiri ndoa miaka nenda miaka rudi mmoja atakuwa kikwazo.

Pia nimegundua mkijuana/mkizoeana sana kwa mtu mwingine asiye na busara inakuwa mwanzo wa kuleta dharau na mwishowe uchumba kuvurugika.

Binafsi nafikiria ni vema wachumba mkajadiliana mkaona mda muafaka wa kuishi katika uchumba na kipindi cha kufunga ndoa pindi mnapoanzisha uhusiano, epuka kujiingiza katika mahusiano yasiyokuwa na miguu wala kichwa.

Matokeo mwishoni unaanza kulalamikaxumechezewa/umepotezewa mda, wakati
hukuwa na mkakati wowote wa kuoa/kuolewa don't waste your time and resources on a useless person.

Karibu wenye uzoefu/mitizamo juu ya hili,ukizingatia kuwa ukipata mke/mume ni jambo jema na unapata kibali kwa Mungu.
Ndoa haijaribiwi,ni heri kukosea kujenga nyumba utabomoa lakini siko kukosea kuoa/kuolewa utajuta, unatakiwa utumie muda wa kutosha kadri uwezavyo ili kujua mwenzio yupo na mlengo gani??Huwa hakuna formula hapa.
 
Ndoa haijaribiwi,ni heri kukosea kujenga nyumba utabomoa lakini siko kukosea kuoa/kuolewa utajuta, unatakiwa utumie muda wa kutosha kadri uwezavyo ili kujua mwenzio yupo na mlengo gani??Huwa hakuna formula hapa.
unatetea usilolijua! huo uchumba wa zaidi ya miaka miwili unatofauti gani na ndoa isiyo rasmi,? mtakaa bila kuzini au kupeana matunzo?
 
unatetea usilolijua! huo uchumba wa zaidi ya miaka miwili unatofauti gani na ndoa isiyo rasmi,? mtakaa bila kuzini au kupeana matunzo?
hayo ni maoni yangu sio kila unaloliamini wewe basi na wenzio wote waamini hivyo,kwa akili yako unajua ukishakuwa na uchumba na mwanamke basi ni kusex tu,mimi nimejuana na mchumba wangu form 4,tumeoana baada ya kumaliza degree,mwanamke wa bar tu ndiye unaweza kukutana naye asubuhi jioni mkafunga ndoa.
 
hayo ni maoni yangu sio kila unaloliamini wewe basi na wenzio wote waamini hivyo,kwa akili yako unajua ukishakuwa na uchumba na mwanamke basi ni kusex tu,mimi nimejuana na mchumba wangu form 4,tumeoana baada ya kumaliza degree,mwanamke wa bar tu ndiye unaweza kukutana naye asubuhi jioni mkafunga ndoa.
sio kweli kizazi hiki! wala case yako sio representative sample ya wachumba wa Tz.pia sijalazimisha ukubali ninachoamini bila facts.
 
sio kweli kizazi hiki! wala case yako sio representative sample ya wachumba wa Tz.pia sijalazimisha ukubali ninachoamini bila facts.
ndio maana nakwambia mawazo yako mgando usilazimishe wengine wayaamini,ndio nyie mnasema hakuna wasichana bikira, wakati wapo huko mtaani,ukimuomba mungu kila kitu kinawezekana ndugu. ninachokwambia ni ukweli kutoka moyoni na jingine ndoa ya mwenzio sio yako kila mahusiano yana staili yake ya kuishi. over...
 
ndio maana nakwambia mawazo yako mgando usilazimishe wengine wayaamini,ndio nyie mnasema hakuna wasichana bikira, wakati wapo huko mtaani,ukimuomba mungu kila kitu kinawezekana ndugu. ninachokwambia ni ukweli kutoka moyoni na jingine ndoa ya mwenzio sio yako kila mahusiano yana staili yake ya kuishi. over...
nahisi utakuwa na utindiwa wa ubongo kuja kuleta mchango wako kwenye mada iliyotolewa na.mwenye akili mgando!
 
nahisi utakuwa na utindiwa wa ubongo kuja kuleta mchango wako kwenye mada iliyotolewa na.mwenye akili mgando!
UTINDIWA WA UBONGO NDIO KITU GANI NDUGU?usiwe na jazba twende taratibu mkuu,nimekuona na umevaa koti nikajua ni mtu wa busara kumbe uko kama mende mkuu,mende juu amevaa koti ukimpindua chini unakuta yupo uchi wa mnyama,au na mkeo umemuokota kwa staili hizo ndugu??
 
UTINDIWA WA UBONGO NDIO KITU GANI NDUGU?usiwe na jazba twende taratibu mkuu,nimekuona na umevaa koti nikajua ni mtu wa busara kumbe uko kama mende mkuu,mende juu amevaa koti ukimpindua chini unakuta yupo uchi wa mnyama,au na mkeo umemuokota kwa staili hizo ndugu??
AKILI MGANDO VEEPE? Msemakweli nilijua unatema madini kumbe mazafanta tu! umeanza matusi.mimi namalizia tu.
 
Asanti mkuu, 2020 ndo tunazungumizia kufunga ndoa
haina kwere mkuu.kwakuwa mnapeana huduma kama wanandoa kwa kivuli cha uchumba hata 2025 mnaweza funga ndoa.Hata Dr slaa ana mchumba mbona miaka zaidi ya mitano.
 
haina kwere mkuu.kwakuwa mnapeana huduma kama wanandoa kwa kivuli cha uchumba hata 2025 mnaweza funga ndoa.Hata Dr slaa ana mchumba mbona miaka zaidi ya mitano.
Sasa kumbe majibu unayo..... Nipe tano mzeiya kama unaamini damu ni mzito kuliko maji
 
Back
Top Bottom