Wadada wanavyojiweka mbali na ndoa

Wadada wanavyojiweka mbali na ndoa

mr vata

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2017
Posts
465
Reaction score
617
Kama mnavyojua wakuu kwamba mwanaume kila siku ni muwindaji na hasa akiwa hana ndoa. Hapa simaanishi kuwinda swala bila shaka naeleweka vyema!
Basi bwana....
Wiki iliyopita nikiwa kwenye mishe mishe za kutafuta mkate wa kila siku nikajikuta nipo kwenye usafiri wa uma naelekea kijichi.
Wakati wa kurudi kwenye gari nilikaa siti moja na binti mmoja, kwa kumwangalia alikua na umri wa miaka 20/22 hivi. Basi hapo ndipo bandiko hili lilipozaliwa.
Mimi ni muumini sana wa mavazi ya kusitiri kwa wadada, na kiukweli nimekua nikiwaamini sana na kuwachukulia kuwa ni wastaarabu wanawake wa aina hiyo ya mavazi. Gauni au sketi ndefu, mtandio n.k
Nikajiingeza nikapata namba. Kilichofuata na stori za hapa na pale, kutakiana hali na ahadi za kuonana. Sikua na haraka. Alinivutia sana na kwa muda mchache nikajiona nipo karibu sana na suala la kuuaga ukapela. Nilijidanganya!
Katika kumshawishi shawishi ili japo akubali tukutane siku moja akakubali, nikasema yes! Kaingia. Tukapanga siku ya kukutana ili tuweze kuongea zaidi. Siku zilipokaribia kuna kuna siku akaniambia kuwa kwa sbb hana kazi suala la nauli huwa linaweza kuwa changamoto kwake kwa hiyo siku ikifika akiomba nauli kama nitaweza kumtumia hata elfu 3 ya nauli atashukuru, nikasema usijali siku hiyo hiyo nikatuma elfu kumi. Sikutaka kumpoteza.
Hapo ndipo nilijua rangi zake. Akawa anachelewa kupokea simu, mara yuko busy na hatimae akawa hapokei kabisa simu.
Baada ya tukio lile nimeona kuwa wanauma tuna mitihani sana katika kufikia kupata wanawake wa maisha yetu.
Ile pesa haukuniuma sana bali niliumia kumpoteza yule binti na zaidi naumia kuona kuwa sisi wanaume tuna mtihani mkubwa katika kutimiza hili lengo.
Kwa waliofanikiwa kila la kheri.
 
Ogopa sana mwanamke anaekuomba nauli au vocha,luku kabla hata hamjazoeana
Mwanamke mwenye kujiamini hata awe na shida vipi atatulia tu kwanza,haoneshi shida yake
Sure.Na hata kama atafikia hatua hiyo atakutumia ile style ya "fill in the blanks".
Mwenyewe jiongeze.
Like last saturday, bint yuko mkoa akanambia kuwa amekua na weekend ndefu kidogo toka ijumaa ameshinda kalala so anahis kuhitaji kutoka kidogo akanyooshe miguu na amemiss sana amarula..(sijawah onja kilevi hata bei sizojui)
Akaishia hapo hapo.Ikabid mzee nisomeshe muamala fasta kwa hallotel bila mtu kusema anahitaji nn na kwa kias gan .....end of time nikawazaa sana like wanaume matatizo mengine tunajitakia wenyewe tu..maana 50k kukutoka reasonlessly bila plan kwakwel ni udhaifu.
Sema she was so thankful at of time ikanifanya kupata faraja moyon.
Ila.nikaapa sifanyi tenaa
 
huyu ni mwakilishi tu wa aina ya wadada waliopo kizazi hiki wala usishangae sana.

Wadada wengi hasa wa huo umri ulioutaja wana matatizo sana.

-Hawana upendo hata kidogo

-Ni ma opportunists tu

-Hawana aiba ya kike

-Hawana maono wanafikiri kuhusu leo tu


kama ulivyosema wanaume tuna kazi saana kutafuta life partner
 
Mshukuru Mungu hakuja yawezekana ungekuja kujuta sana mbele ya safari. Mifano mingi tunayo haswa kwa mabinti wa umri huo ni hatari ndugu yangu
 
huyu ni mwakilishi tu wa aina ya wadada waliopo kizazi hiki wala usishangae sana.

Wadada wengi hasa wa huo umri ulioutaja wana matatizo sana.

-Hawana upendo hata kidogo

-Ni ma opportunists tu

-Hawana aiba ya kike

-Hawana maono wanafikiri kuhusu leo tu


kama ulivyosema wanaume tuna kazi saana kutafuta life partner
Kweli mkuu
 
Sure.Na hata kama atafikia hatua hiyo atakutumia ile style ya "fill in the blanks".
Mwenyewe jiongeze.
Like last saturday, bint yuko mkoa akanambia kuwa amekua na weekend ndefu kidogo toka ijumaa ameshinda kalala so anahis kuhitaji kutoka kidogo akanyooshe miguu na amemiss sana amarula..(sijawah onja kilevi hata bei sizojui)
Akaishia hapo hapo.Ikabid mzee nisomeshe muamala fasta kwa hallotel bila mtu kusema anahitaji nn na kwa kias gan .....end of time nikawazaa sana like wanaume matatizo mengine tunajitakia wenyewe tu..maana 50k kukutoka reasonlessly bila plan kwakwel ni udhaifu.
Sema she was so thankful at of time ikanifanya kupata faraja moyon.
Ila.nikaapa sifanyi tenaa
Hahha mkuu uliapa
 
Yani mkuu kukutana na dem tu dakika chache kwenye daladala, ushampenda na kuwaza kuuacha ukapela!!!! Una hatari sana mzeeee
 
  • Thanks
Reactions: VSM
Back
Top Bottom