Wadada wa Uchumi Supermarket - Quality Center

Wadada wa Uchumi Supermarket - Quality Center

Nyanya mbichi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2011
Posts
3,716
Reaction score
2,218
Naandika haya kwa kuwa mimi ni mhanga wa hili suala.Hawa wadada huwa wanakukata 200 au 300 hawasemi ukihesabu salio lako unakuta limepungua ukiwauliza wanakuambia hawana change,nimefanyiwa zaidi ya mara mbili mara ya tatu nikatoa mia tatu ili nipewe 500 mdada akaniambia nisubiri,mpaka mteja mwingine aje ndipo afungue vidude vyao vile , nikae kula zangu nilivyomaliza nikaenda kukumbusha salio langu kumbe mdada kaondoka ,wale walioko zamu wakamjua mpokea pesa alietoka punde msela Mmoja akamfuata aliko akiwa na receipt yangu akarudi na 500 yangu(huku ni kule kwenye menu) wale wadada wajanjawajanja sana wengi wao.

TUWE MAKINI
 
Bar ndiyo usiseme,bora ingejulikana bia ni 2500 maana kila siku 200 hawana
 
kama ni mdhuri sana mm namuachia tu kwa roho nyeupeeeee

uzuri wake ,kuna siku kulikua na mdada kajazia na yuko vizuri tu alileta stori hiyo hiyo nikazama mfukoni nikampa ya sarafu akanipa pesa ya karatasi
 
Eti ni mpare. Anadai hata tsh 1 kwa taarifa zenu. Hiyo ni haki yake na anamsaidia dada asiwe mwizi. Anaanza kuiba tsh 200 je akiwa hazina ataiba tsh ??
Au mnataka kina pro tibaijuka " hela ya mboga kitchen part"
Tafakar chukua hatua
 
Tulishaambiwa lakini, kila mtu ale ofisini kwake.
 
Chenji ni haki yangu. Ina maana mimi nikipungukiwa na mia mbili au mia atanipa bidhaa?
 
Bora umeleta hii mada hapa ndugu Mimi mwenyewe ni mhanga siku moja nilienda pale nikanunua vitu vya jumla sh 6900/- nikatoa 7000/- ili wanirudishie Mia wakaniambia hawana chenji na kunipa majibu Kama ya kwako nikakaa pembeni nakula bisi kama dakika mbili nikarudi majibu ni yale yale nikamkolomea akaenda kunitafutia chenji nikasepa kumbe ni wezi wamegundua mradi wewe fikiria Kama kila mteja ataacha mia Mia mbili kwa siku itakuwa sh ngapi? Waache huu ni wizi watafute chenji mapema wawrudishie wateja wao
 
Pole sana ndugu yetu...nilijua ni kawaida yao...kila mteja abakishe hizo change.

Na kwa kua ni mia 2 au mia 1 ...ukidai unaonekana umechoka na bado hurejeshewi change zako.

Ni hatar sana ....
 
Back
Top Bottom