Wadada punguzeni maringo

Wadada punguzeni maringo

Slim5

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
28,374
Reaction score
38,248
Najua mko poa.

Endelea kunishusha, kunipandisha, mimi nimekuwa huku nikiamini mtoto wa kike ni haki yake kulinga, kuwa na nyodo. Lakini basi isiwe too much, fanya nyodo kidogo, na kidogo kuwa na staha! Hili ni somo kwa wana Jamii forum wote, hasa dada zangu! Leo nina hii.

Mrembo ndio, japo sio kiviiile, umejoin staff team yetu, juzi juzi tu, hata mshahara wa kwanza bado hujavuta. Umekuja na speed 120, werevu wanasema mwenye nguvu mpishe, tukakupisha, tulijua wapi mbio za sakafuni, zitaishia.

Slim5 sina makuu, nacheka na kila mtu, sina kinyongo, sijui kukunja! Ulivoona nakuchekea ukajua, nimefika bei, ukajua nitakuomba mzigo, kichwa kichwa.Kama ni game ume-offside, mimi si wa hivo.

Mimi nacheka na kila mtu! Nimeona papuchi nyingi sana, yako sidhani kama ina jipya! Na kuangalia tu, kila nikija kumuona boss wangu, kwa vile lazima nianzie kwako, una kazi ya kunishusha, kunipandisha!

Jumatatu, Unanishusha, unanipandisha!
Jumanne, Unanishusha, unanipandisha!
Jumatano, Unanishusha, unanipandisha!
Alhamisi, Unanishusha, unanipandisha!
Ijumaa, Unanishusha, unanipandisha!

Kwa kuwa hili haliathiri utendaji wangu wa kazi, sintakaa nikuulize nini chanzo! Sihitaji reconciliation na wewe! Sintapoteza muda wangu eti kutafuta sababu kwa nini unanidharau.

So long hunijui, sikujui, wacha maisha yaendelee, wakati ukifika utajitambua, na utajifunza namna sahihi ya kuishi na watu sehemu za kazi, na penginepo! Tumekutana kwa bahati mbaya, na ntafanya kazi na wewe kwa bahati mbaya hivo, hivo.

Nakuonea huruma leo uso umekushuka kama ndugu wa mke baada ya ndoa kuvunjika, rafiki yako kaniomba lift wakati wa kuondoka, nikasimama kuwabeba, mkachoma ndani, ukajiachia siti ya nyuma! Ukajikausha kau, zaidi ya kaukau, ukianzisha story yako sichangii, akianzisha rafiki yako, nachangia, nacheka.

Mungu sio Rugemalira, kumbe njia yetu moja, Morogoro rd, rafiki yako leo kashuka K. Korogwe, wee kumbe unaenda Kibamba, slim5 ubavuni kwangu Mbezi Mwisho, njia nzima umekuwa mpole kama mwanamke aliekopwa papuchi,

Umejaribu kujichekesha, kujisemesha, mie kimya! Uso wa mbuzi, zaidi ya mbuzi mwenyewe! Kutoka K. Korogwe aliposhuka mwenzio, sijafungua mdomo wangu mpaka nakushusha Mbezi upande gari za kwenu!

Nakusubiria Jumatatu, nikuone Unanishusha, unanipandisha kama kawaida yako.Jifunze kuishi na watu vizuri, kuwa mwema kwa watu wakati wa kwenda, waweza kukutana nao wakati wa kurudi.

Alamsiki Slim5
 
interesting....
hili la kusema 'mtu fulani ana maringo'
au hasalimii anajisikia ..most of time tuko very wrong

baadhi ya watu kutokana tu na malezi hawajui tu namna ya kuishi na watu
wengine wametoka kwenye very different background....

unaweza tafsiri ni maringo au kujisikia kumbe tu mtu anaogopa watu
au hana tu 'social skills' zinazohitajika hapo

au mwingine ni mwili tu but bado mtoto mno kuelewa how to deal na watu tofauti..
wengine wana stress tu za kufa mtu hata akikusalimia why hasalimii watu utamuonea huruma
 
Sorry,eti wewe ni wakike au wakiume?
 
Kashajua usafiri wako ndo njia ya nyumbani anasevu nauli..basi j3 subiri kuchangamkiwa na kukaribishwa lunch kwa madoido kibao ili jion ajikale siti ya ubavuni hapo mpka mbezi... Sasa akili kichwan mwako
 
 
Last edited by a moderator:
Dah! Kweli kuna ke wanadharau ila nawe unamichambo ya kike!!!!!! Ni kana kwamba ulisubiria akwame upate pakuropokea.

Haingii akilini mtu kaja tu ofisini na bila sababu yoyote akufanyie hivyo. Eti unasema akitia story huongei! Ulimfikisha hadi kwao bila kumuongelesha!!!! Wewe ni mwanaume? Kweli!!!???

Namna ya kuhandle vitatizo vidogo vidogo wengi yatushinda Wallah.
 
Dah! Kweli kuna ke wanadharau ila nawe unamichambo ya kike!!!!!! Ni kana kwamba ulisubiria akwame upate pakuropokea. Haingii akilini mtu kaja tu ofisini na bila sababu yoyote akufanyie hivyo. Eti unasema akitia story huongei! Ulimfikisha hadi kwao bila kumuongelesha!!!! Wewe ni mwanaume? Kweli!!!??? Namna ya kuhandle vitatizo vidogo vidogo wengi yatushinda Wallah.

Hakuna sehemu nimesema, nimemfikisha kwao!
 
Si mchezo ila wengine kweli wana nyodo za makusudi..labda mpaka akuzoee
 
C umpe tu cheupe live!unamuogopa au nawe si ungemkatalia asipande gari yako
 
Back
Top Bottom