Wadada mna nini na magari?

Wadada mna nini na magari?

Samboko

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2011
Posts
5,421
Reaction score
7,877
Habari ya weekend wana jf,

Tangu nikiwa mdogo kijijini hukoo nilikua najiwazia siku nikipata ela nitanunua gari kwanza, wala sio nyumba, nilitamani siku moja na mimi niende na gari kijijini naendesha mwenyewe, maana nilikua naona wivu sana baadhi ya majirani zetu wakija na magari yao kule,

Nikaja mjini kutafuta baada ya miaka kadhaa ya kutafuta nikaweza kununua gari,
Sasa hapo ndio nikajua wadada wanapenda wanaume wenye magari, hata waliokua hawanisalimii wakawa na heshima, hakuna kutongoza tena gari tayari ni kitongozeo tosha na vituko vingivingi hivi kwao.

Sasa huyu wa juzi j5 ndio kaniacha hoi,
Nimetoka zangu kkoo jioni nipo kwenye daladala nikakaa na dada mmoja baada ya stori za hapa na pale nikaomba namba akanipa nikamtext palepale tushuke wote nna maongezi nae, akajibu sawa.

Tukashuka wote pale africa sana nikashangaa mwenzangu huyooo anatokomea zake nikamfuata kwa nyuma akawa anaongeza mwendo ili nisimfikie na njia aliyokua anaelekea na mimi naelekea hukohuko, nikafika kwa dada nkaingia ndani nkachukua funguo za gari nililokua nimemwachia tangu j2, kutoka nje nikawasha gari kuangalia mbele yule dada anarudi kumbe alikua ananikimbia mimi,

Nkamfuata kumfikia nikapunguza mwendo nikamuuliza ulikua unanikimbia nini? Akasema hapana, nkamwambia ingia kwenye gari akaingia, nikamuuliza nyumbani kwao wapi nimpeleke akaniambia nikampeleka hadi kwao wala sikumsemesha tena chochote nikaondoka,

Jana jioni kanitumia sms "mambo, ushaondoka kkoo?" mi wala sikumjibu,
Nikabaki najiuliza tuu, kuona gari urafiki uendelee akasahau alinikimbia pale kituo cha daladala.
 
Yani mpaka wake za watu Gari unawagegedaa
1471127133194.jpg
Lamborghini Baby
 
Na hichi kinachowatia vijana wengi umasikini wa kiakili na kimwili........yaani kila siku kijana unakuwa mgeni wa nyuchi za wanawake........mpaka unalazimika kuishi kwenye mitazamo yao na kuwaridhisha wao.......
Sasa sijui siku wanawake wakianza kuvutiwa na wanaume wenye makalio makubwa na wewe utaenda kujidunga shindano....ili uendelee kuwapata na kukidhi haja zao......

Vijana jitahidini kuishi kwenye mistari yenu ya maisha......pia msitpanye fedha kwenye mambo yasiyo na tija.....bora kuwekeza kwenye miradi ya muda kwani wakati ni ukuta na ujana ni maji ya moto......
 
Ni ulimbukeni wa wadada. Siku zote kile usichokuwa nacho ndicho unachokitamani. Wadada wengi familia zao ni hoe hae, unaweza kukuta baba yake hata baiskeli hana, kwahiyo akiona unamiliki gari lazima akupapatikie hata kama ni gari la mkopo yy ataamini fedha kwako zimelala. Binafsi mwanaume mwenye gari hanibabaishi, ila yule mwenye vigezo navyohitaji haki ya nani wallah silali kwa ajili yake.
 
Ni ulimbukeni wa wadada. Siku zote kile usichokuwa nacho ndicho unachokitamani. Wadada wengi familia zao ni hoe hae, unaweza kukuta baba yake hata baiskeli hana, kwahiyo akiona unamiliki gari lazima akupapatikie hata kama ni gari la mkopo yy ataamini fedha kwako zimelala. Binafsi mwanaume mwenye gari hanibabaishi, ila yule mwenye vigezo navyohitaji haki ya nani wallah silali kwa ajili yake.
Kweli maskini wanatabu sana
 
Back
Top Bottom