Wachina wanatorosha madini yetu

mleta taarifa hana kosa lolote na wala sijasema kuwa anakosa. mimi nimemuuliza swali tu full stop.
Kwahiyo wewe ulivyofundishwa ni kwamba mtu akiongeaa ukweli basi ni amekosa maslai kwenye hilo jambo analoliongelea ukweli wake..?
 
Sitashanngaa kuyasikia hayo! Shida ni ndoa iliyopo kati ya ccm na chama tawala cha China.
Kama ulifuatilia uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, ambao karibu mataifa makubwa yote duniani yalihudhuishwa ukandamizaji wa haki a demokrasia ulofanywa na ccm dhidi ya vyama vya upinzani, Lakini China ilikuwa taifa pekee lililoipongeza ccm haraka na hata kuannza kuyanyoshea kidole mataifa meginne yaliyokuwa yanasisitiza demokrasia likiyataka kutoigilia mambo ya ndani ya Tanzania! Kumbe ile haikuwa bure walijuwa kuna mkate mbele yao!
 

 
Wewe mtu ni wa ajabu sana, kosa lake huyu ni nini? Ina maana hapaswi kutoa taarifa kama hizi ili serikali ifanye kazi yake?
Jf mods, watu wa hivi wanaweza vipi kuendelea kuwa humu?
Ndio hapaswi kutoa taarifa inatakiwa aishi na kujali maisha yake.
 
Yani ukisoma comments ndio unapata picha halisi hata huku mitaani hali ilivyo.
Ndio maana hata wanasiasa wanabadilishana mavyeo na kuitafuna hii nchi jinsi wanavyotaka maana walishasoma akili zetu zilivyo.
Haiingii akilini mgeni anafanya uhujumu uchumi halafu mtu anatoa taarifa then watu wanamponda na maneno mengine kibao.

So sad!
 
Ila mkuu kosa la huyu mtoa taarifa ni nini? Mbona kafanya Jambo jema sana, wenye mamlaka wanapaswa kuchunguza Kama kweli waloshughulikie.
Wewe unaweza kwenda China na kufanya Kama wao wanavyofanya huku?
Ndio mkuu naweza kwenda. Tatizo hamjiamini
 
Tuna tatizo Tanzania
 
Hii tabia ya watanzania kulalamika kila siku haitupeleki popote. Nchi hii ni yetu Mwenyezi Mungu katupa na raslimali zake zote za ardhi, misitu, maji, madini, wanyama pori, gesi ya asili, mapori ya hifadhi, n.k. Wachina wengi wamekuja hapa Tanzania kwa biashara za bithaa au huduma kama ujenzi, uchimbaji wa madini, utalii, au hata utalii, bila kusahau wachache waliooa na kuzaa hapa Tanzania. Tuna wajibu wa msingi wa kulinda raslimali zetu zote na siyo kulalamika. Hao wachina kama mmewaacha maporini bila usimamizi, au watu wetu wanakubali kula rushwa halafu wanaachia madini yanatoroshwa ..... ni nani hapo mwenye shida. Mchina au Mtanzania mwenye nchi?
 
Mkuu umetimiza wajibu wako ila ukweli ni kwamba nchi imerudi kwenye wizi mkubwa wa rasilimari zetu, na hapo kuna mkubwa anakuwa anapata chake hivyo inakuwa ni rahisi saana kutoa taarifa kwa hao wachina, suala la kutoa taarifa kwenye social platform pia ni zuri kikubwa taarifa ifike kwa wahusika na wewe uwe salama
 
Sawa sawa mkuu!
 
Kwa akili za watanzania ni sawa na za mtu mpuuzi asiyeelezeka!

Kiongozi anaewajibika kulinda maslahi yao kwa nguvu hawamtaki na yule mpenda haki watamuita katili ama dikteta eti sababu hawashirikishi kwenye shughuli za upigaji dili ama ana insist nidhamu! Mtu anayejali welfare ya wananchi kwa ujumla na kuhakikisha anafanya vitu tangible huyo ni mbaya sana katili!

Kiongozi ambaye anashirikiana na vibaraka wa ughaibuni na viongozi wazawa kukwapua mali na kupiga madili huko serikalini ndio anashabikiwa na kuonekana ndio mtu wa maana! Huyu ndio aachwe achape kazi ila wanaonufaika ni kundi dogo huku wakipuuza welfare ya wananchi wengi kwa ujumla!

Ni sawa na akili zile zile za o’level za kumuita discpline master mnoko wakati ndio kazi yake inamtaka awe hivyo! Ni kusimamia nidhamu na sio jambo jepesi!

Wachina pigeni haoo mpaka yabaki mahandaki tu!
 
Mleta mada hongera kwa kwa kuonyesha uzalendo,umetimiza wajibu wako,

Nilikuwa naongea na baadhi ya wachimbaji hapo siku kadhaa zimepita ni kweli kuna tetesi hao jamaa wanachota,sasa nadhani wahusika wafanyie kazi hili suala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…