Kutoka chanzo chetu - wajaribu kuhonga, wakutwa na Tanzanite pia!:Unachosema mkuu ni kweli, hii habari nilipewa leo asubuhi na jamaa yangu anayefanya kazi bandarini.
Sio tetesi ni ukweli mtupu!
Nafikiri mambo haya yanatokea wakati muafaka kabisa, wakati tunaandika katiba mpya. Watanzania wote tushirikiane na kuhakikisha inawekwa sheria ya kunyongwa mpaka kufa au kifungo cha maisha without any possibility of parole kwa watu wote wanaopatikana na hatia ya kufanya biashara ya pembe za ndovu/ujangili pamoja na wanaouza madawa ya kulevya!
Sakata la Wachina na kukutwa na Nyara za Serikali limeendelea kuchukua sura mpya ambapo Wachina wawili walifika bandarini wakitaka kuwasailimia ndugu zao ambao ni Wanajeshi.
Walipofika getini, kwakuwa tayari wanajeshi wa JWTZ waliishaimarisha ulinzi baada ya tukio la jana yake (usiku wa kuamkia leo) na meno ya tembo. Wanajeshi walitaka kuwakagua Wachina hao wakagoma na ndipo wakapekuliwa kwa lazima na kukutwa na madini aina ya Tanzanite. Wakaitwa maofisa wa Nishati na Madini na polisi wakawachukua!
Tukio la awali lilikuwa la jana Jumatatu saa 3 usiku wa kuamkia Jumanne (leo) ambapo gari moja binafsi likisindikizwa na gari la Polisi na mtu mmoja mwenye sare za Polisi lilifika katika lango la bandari eneo la geti namba 2 wakielekea geti namba 3 iliko meli ya kijeshi ya Kichina yenye wanajeshi takribani 600.
Katika gari la kiraia kulikuwa na Wachina watatu; wawili wanajeshi na mmoja raia na dereva Mtanzania.
WACHINA walitaka kuwapa walinzi rushwa ya sh milioni 25 baada ya walinzi kukuta kuna vipande 81 vya meno ya tembo.
Walinzi waligoma na kulazimisha kulikagua gari. Kuona hivyo gari la Polisi na mtu aliyevaa sare za polisi wakatoweka na wale wanajeshi wawili wa Kichina wakatoweka na kukimbilia katika meli yao ya kijeshi na kujichanganya na wenzao.
Ndipo walinzi walipowasiliana na wanajeshi na Polisi na wakaja wanajeshi na maofisa Usalama wa Taifa wa Tanzania ambao waliwachukua Mchina na dereva Mtanzania na kuondoka nao.
Tunaendelea kufuatilia zaidi kuwafahamisha kinachojiri
Tutajuta sana kumtoa Kagasheki! !Wanyongwe hadharani,
Hii operesheni tokomeza irudi tu tena kwa nguvu zaidi
Wanyongwe hadharani,
Hii operesheni tokomeza irudi tu tena kwa nguvu zaidi
Mimi mwenyewe nimesikia hii habari kutoka vyanzo ninavyoviamini sana
Kwa sheria ipi? Watueleze ni nani anayesaidiana nao kwenye hii biashara.Wanyongwe hadharani,
Hii operesheni tokomeza irudi tu tena kwa nguvu zaidi
Mimi mwenyewe nimesikia hii habari kutoka vyanzo ninavyoviamini sana