Wachezaji Wa Simba S. C Acheni "Kumzururisha" Mzungu

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,459
29,157
Hivi Karibuni Mchezaji Dejan alipofunga goli Mashabiki wengi wa Simba tulifurahi sana. Sababu ya kufurahi ni kua toka asajiliwe Mchezaji huyu hakua amefunga goli kwenye mechi yoyote ile ukiacha mazoezini labda.

Wengi tulianza kuamini kua Mchezaji huyu "tumepigwa", wengine kufikia kusema aheri ya Meddy Kagere na Chris Koppe Mugalu walioondoka kuliko Dejan Mzungu.

Kwa kua mechi zilizopita hakucheza dakika zote 90 sikuweza kumuangalia Kwa mapana zaidi, lakini jana ndio nimemuona vizuri kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Al Hilal.

Wachezaji wenzake hawakua wakipeleka mipira kwake ipasavyo, wangeweza hata kurudisha mipira nyuma kuliko kumpasia yeye.

Alikua akikimbia sehemu mbalimbali, kati, kushoto na kulia ili aweze kupewa mipira lakini haikua hivyo. Ni kama vile Wachezaji wenzake hawamuamini au wanamfanyia mtimanyongo.

Yaani mmepangwa Wachezaji 11 uwanjani wa timu mmoja lakini Wachezaji wenyewe wanaamua kucheza 10 kwa kumfanya mmoja wao kama mfanya mazoezi tu. Ataanza mechi, atakimbia kimbia, atatoka jasho, na halftime atarudi tena lakini ukimfanyia assessment unagundua dakika zote 90 hakua na any impact.

Hii inaweza isiiathiri timu kama inacheza na timu yenye kiwango kidogo kuliko Simba (dhaifu) lakini kwa mechi kubwa italeta madhara. Manake mtajiona kwa number mko 11 ki nadharia uwanjani kumbe wanaotumika ni 10 tu kivitendo.

Ni wakati sasa Wachezaji waitwe waulizwe wana shida gani na Dejan mpaka wanaamua kutomtumia. Inawezekana ni roho mbaya zetu tu watu weusi, au Dejan pamoja na kuji-position sehemu mbalimbali lakini wenzake wanamuona labda hayuko eneo zuri la kupewa mipira (offside au amekabwa).

Ni vizuri kuongea hili mapema kuliko kuendelea kufuga tatizo. Huu ni mtazamo tu.
 
Nimependa maoni yako mkuu, lakini kwa dejan mbona zipo pasi nyingi jana amepewa lakini either anaanguka au anazidiwa ujanja na mabeki?

To me nafikiri ni nzuri zaidi dejan awe anaingia sub kama alivyoanza mechi kadhaa zilizopita.
Haya pia ni maoni yangu mkuu.
 
Kuna pass mtu anakupa ili kuondoa lawama au ionekane amekupa, lakini sio anakupa ufunge. Anakuona kabisa umekabwa anakusakizia hivyo hivyo.

Pale ambapo Dejan anakua open hana mtu hapewi pasi
Mimi nitawatetea Wachezaji Kwa Mechi ya Jana. Tatizo la Dejan ana mikimbio mizuri na positioning mbovu. Ni kama anaukimbia mpira mpaka atafutwe.

Katika soka mpokea pasi ndiye anayetoa maelekezo Kwa mtoa pasi wapi apeleke pasi yake Kwa kuonyesha uelekeo, kitu ambacho Jana kilimshinda kabisa Dejan.

Angalia Mambo aliyoyafanya Aziz Ki kwenye Mechi za Mwanzo za kirafiki za Yanga. Ana mpira, halafu anamuelekeza mwenzake aelekee wapi ili Ampe mpira matokeo yake akipeleka anakuta nafasi imezibwa na kiungo au beki.

Mechi za ligi naona kocha kamwambia, huwezi kufanya Mambo mawili Kwa wakati mmoja ukafanikiwa.

Kwa hiyo kama unataka Dejan awe Bora, kitu ambacho wengi tunatamani mwambie awe na mikimbio yenye uelekeo sahihi vinginevyo ataendelea kuonekana mtalii uwanjani kama Jana.
 
Mzungu niliona waswasi akinyimwa pas na ether chama au sako nadhani ni wivu na pia sako hataki jamaa aendelee kuwa maarufu kuliko wao chama anataka kukukota Mpira kutoka katika had mwisho Sana atamtafuta sako amlishe mipira kuliko kumpa mzung ambae ameomba na apewi Mpira chana Ana pasiana na sako tu

Nililiona Hilo Kama vile hawataki kuona mzungu anafanya vzr kuliko wao
Mzungu alibadilish postion Mara tatu lkn wapi jamaa hawampi Mpira Ni mbaya Sana

Simba tutawala msimu mzima huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo kocha amemfanya mzungu very special kuliko wachezaji wote pale simba na anamuona ana ubora kuliko mchezaji yoyote kwa hyo kama ana quality hyo inabidi apambane na hali yake athibitishe hilo.
 
Mzungu niliona waswasi akinyimwa pas na ether chama au sako nadhani ni wivu na pia sako hataki jamaa aendelee kuwa maarufu kuliko wao chama anataka kukukota Mpira kutoka katika had mwisho Sana atamtafuta sako amlishe mipira kuliko kumpa mzung ambae ameomba na apewi Mpira chana Ana pasiana na sako tu

Nililiona Hilo Kama vile hawataki kuona mzungu anafanya vzr kuliko wao
Mzungu alibadilish postion Mara tatu lkn wapi jamaa hawampi Mpira Ni mbaya Sana

Simba tutawala msimu mzima huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Sasa ubinafsi wao unaigharimu timu
 
Wakati Dan Senkuruma anakuja Simba akiwa mfungaji Bora Bora Kenya kina sjibu Kwa makusudi walikuwa hawampi pasi au eakimpa pasi ni pale alipokuwa amekabwa au yupo nafasi mbaya
Boniface Ambani alikuja Tanzania kutokea Kenya nae akawa mfungaji bora msimu huo huo. Sasa sijui aliwanyima mgao wa zawadi ya ufungaji bora Wenzake au alijiona yeye bora akajimwambafai, msimu uliofuata wakawa hawampi pasi.
 
Tatizo kocha amemfanya mzungu very special kuliko wachezaji wote pale simba na anamuona ana ubora kuliko mchezaji yoyote kwa hyo kama ana quality hyo inabidi apambane na hali yake athibitishe hilo.
Hiki ndicho kinakuja kumfukuzisha kocha
 
Tatizo kocha amemfanya mzungu very special kuliko wachezaji wote pale simba na anamuona ana ubora kuliko mchezaji yoyote kwa hyo kama ana quality hyo inabidi apambane na hali yake athibitishe hilo.
Kivipi ndugu? Mbona mzungu anaingia sub, tena dkk za mwisho isipokuwa jana. Usije kuwa una chuki zako binafsi kwa kocha wetu.
 
Tatizo kocha amemfanya mzungu very special kuliko wachezaji wote pale simba na anamuona ana ubora kuliko mchezaji yoyote kwa hyo kama ana quality hyo inabidi apambane na hali yake athibitishe hilo.
Hili ni tatizo,
Star yoyote duniani hata awe mzuri vipi hawezi kufunga magoli bila ushirikiano na wenzake.
 
Kivipi ndugu? Mbona mzungu anaingia sub, tena dkk za mwisho isipokuwa jana. Usije kuwa una chuki zako binafsi kwa kocha wetu.
Hapana mkuu sina chuki kumkataa kagere na kusema haendani kwenye mfumo ila mzungu ndo anafaa striker wote hawataki mpaka chama ilikuwa hamtaki eti yupo slow kuanzisha mashambulizi ajabu ndo amehusika magoli yote ya simba kitendo cha kutoa list ya wachezaji ambao hawataki halafu mzungu anamuacha kina igawa team kwasababu mpira unaonekana hauchezwi chumbani ni kama mashabiki wa Manchester United walivyokuwa wanalalamika kwa Maguire.
 
Back
Top Bottom