Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Wachawi wanikosesha usingizi usiku wa leo

Wenzako ikifika usiku ni marufuku Kulitamka neno CHUMVI,
huwa tunaita MUNYU,
sasa wewe ita chumvi uje ulale na mazonge...( nimetoka ndani mada maramoja, ila nitarudi baadae)
Nakusubiri
 
Hakuna Uchawi wala Wachawi
Hayajakukuta,hata mleta mada alikuwa haamin na baada ya vimbwanga sasa kaleta mrejesho,uchaw upo na ni hatar
Na imani nyote ni wazima.
Moja kwa moja kwenye mada.

Ndgu zanguni hapo kabla nilikuwa nilikuwa siamini kuna wachawi ingawa nilikuwa nikisikia watu wakisema.
Hapo kabla nilikuwa nikiota ndoto mbaya sana na wakati mwingine nikijikuta natoka nje bila kujua usiku wa manane wakati huo nakuwa siko ktk hali ya kawaida kbsa.naweza kusema ni Mungu tu.

Ile hali ya ndoto mbaya ikawa inazidi nikaanza kwenda kwenye maombi.nilipoanza maombi ni kama nilizidisha nilikuwa nikiota ndoto mbaya nyingi zikiwa za mijoka mikubwa yenye rangi ya gold na yellow.nikalifikisha kwa mchungaji nikafanyiwa maombi ile hali ikawa inapotea kidogokidogo.ikafikia hatua naota mara chache sana.kwahiyo nikawa najisimamia mwenyew kukemea hizo ndoto

Jana usiku nikawa namsikiliza mwakasege saa tatu usiku(huwa ni utaratibu wangu wa kusikiliza mahubiri yake).lakini jana ile anaanza nikapata usingizi ghafla nakuja kustuka anamalizia.nikalala.

Sasa usiku wa saa saba hivi usingizi ukakata kabisa lkin nikawa nasisimkwa mwili isivyokawaida.najionea giza tu hapo niko macho kumbuka baadae nikawa naona uso wa mtu ila una jicho moja lipo ktkt ya kipanda uso na majitu kama mazombi ya kwenye movie.hee!!ikabidi kiamke nikatoka nje nili niwaamshe majirani.ikumbukwe sina usingizi kabisa na wala sipo ndoton.

Wakati naelekea kuwaamsha majiran nikakumbuka nina maji ya baraka ndani ikabidi nirud nijimwagie maji ya baraka kitanda na sehemu zote za chumban.nikarudi kulala.yani ni kama nimeyafungulia sasa yakaja upya na makucha juu ila kwa sasa yalikuja kama vile naota lkni niko macho kabisa.mwili mzimaaa ulikuwa unasisimka upande wa kushoto na kulia naona giza kabisa.kweli niliogopa sana.

Kilichonichanganya zaidi ni ule uso wa yule mtu.ni sura ya mtu ninaemfahamu tena ni mtu wangu wa karibu kabisa na mimi.kweli katika hali ya kibinadamu naogopa jmn wakti mwingine.naogopa hata kuingia ndani jmn.

Poleni kwa urefu wa uzi.nimeona nishee nanyi hiki kilichonisumbua usiku wa leo.


Sent from my TECNO H5 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna Uchawi wala Wachawi
Hayajakukuta,hata mleta mada alikuwa haamin na baada ya vimbwanga sasa kaleta mrejesho,uchaw upo na ni hatar
Na imani nyote ni wazima.
Moja kwa moja kwenye mada.

Ndgu zanguni hapo kabla nilikuwa nilikuwa siamini kuna wachawi ingawa nilikuwa nikisikia watu wakisema.
Hapo kabla nilikuwa nikiota ndoto mbaya sana na wakati mwingine nikijikuta natoka nje bila kujua usiku wa manane wakati huo nakuwa siko ktk hali ya kawaida kbsa.naweza kusema ni Mungu tu.

Ile hali ya ndoto mbaya ikawa inazidi nikaanza kwenda kwenye maombi.nilipoanza maombi ni kama nilizidisha nilikuwa nikiota ndoto mbaya nyingi zikiwa za mijoka mikubwa yenye rangi ya gold na yellow.nikalifikisha kwa mchungaji nikafanyiwa maombi ile hali ikawa inapotea kidogokidogo.ikafikia hatua naota mara chache sana.kwahiyo nikawa najisimamia mwenyew kukemea hizo ndoto

Jana usiku nikawa namsikiliza mwakasege saa tatu usiku(huwa ni utaratibu wangu wa kusikiliza mahubiri yake).lakini jana ile anaanza nikapata usingizi ghafla nakuja kustuka anamalizia.nikalala.

Sasa usiku wa saa saba hivi usingizi ukakata kabisa lkin nikawa nasisimkwa mwili isivyokawaida.najionea giza tu hapo niko macho kumbuka baadae nikawa naona uso wa mtu ila una jicho moja lipo ktkt ya kipanda uso na majitu kama mazombi ya kwenye movie.hee!!ikabidi kiamke nikatoka nje nili niwaamshe majirani.ikumbukwe sina usingizi kabisa na wala sipo ndoton.

Wakati naelekea kuwaamsha majiran nikakumbuka nina maji ya baraka ndani ikabidi nirud nijimwagie maji ya baraka kitanda na sehemu zote za chumban.nikarudi kulala.yani ni kama nimeyafungulia sasa yakaja upya na makucha juu ila kwa sasa yalikuja kama vile naota lkni niko macho kabisa.mwili mzimaaa ulikuwa unasisimka upande wa kushoto na kulia naona giza kabisa.kweli niliogopa sana.

Kilichonichanganya zaidi ni ule uso wa yule mtu.ni sura ya mtu ninaemfahamu tena ni mtu wangu wa karibu kabisa na mimi.kweli katika hali ya kibinadamu naogopa jmn wakti mwingine.naogopa hata kuingia ndani jmn.

Poleni kwa urefu wa uzi.nimeona nishee nanyi hiki kilichonisumbua usiku wa leo.


Sent from my TECNO H5 using JamiiForums mobile app
 
naona maimuna, makata, kashikashi, subiani, walikuwa wageni wako, anyway..
ilinitokeaga kipindi hivi ikawa nikiomba kabla ya kulala hali ndo ikawa mbaya zaidi usiku, lakini siku nilizolala bila kuomba nilipiga usingizi murua kabisa,
my take;
usianzishe vita na mapepo/ maruhani kama una imani haba
Ndivyo nilivyo mimi japo kwa siku za hivi karibuni imepungua kidogo.

So siku hizi husali tena sio!!
 
Ukiona kitu kama hicho it's damu ya yesu, njoo kesho ubungo Emaus kituo cha karesmatik kuna kongamano limeanza,muda SAA 3 had sits unafanyiwa deliverence na SAA 8 had 12 ndo Luna kongamano lenyew mahubir na maombez
Emaus wako vizuri sana, nishawahi kupata huduma ya maombi hapo

Sent from my HUAWEI MATE 9 using JamiiForums mobile app
 
Duuh pole mama aisee rud tena Kanisan ukafanye maombi mama
Hakuna namna baba inabidi nirudi aiseeh.
Sitaki kuchuma dhambi juu ya sura ya mtu wangu wa karibu niliyoiona
 
Nashindwa kuelewa muumini akiona wachawi basi anatakiwa aombewe lakini mchungaji yeye pekee akiona basi huwa ni maono hahaaaahaa wakati wote ni binadamu. Imekaaje hii
Ngoja wataalam waje mkuu.
 
Kwanini ulipoona hizo sura huku kemea tena ,wakati unajua kabisa kuwa bila ya kumkaribia Mungu unatoa mwanya kwa mapepo na wachawi kukuchezea.
Nilikuwa nikisem "Mungu wangu"mengine mdomo ulikuwa mzito
 
Sali, funga na kuomba.
Jikabidhi kwa Yesu totally, hii hali itapotea kabisa. Jina la Yesu ndiyo kiboko ya hayo mambo yanayokusumbua.
Hiyo sura ya rafiki si yeye, ni mbinu za wachawi kujificha.
Achana na Maji ya baraka, hiyo ni Tiba mbadala, ukitumia hayo Maji ndo unawaongezea nguvu wachawi.
Samahani kwa niliyemkwaza.

Sent from my Infinix HOT 3 using JamiiForums mobile app
 
Ukiona kitu kama hicho it's damu ya yesu, njoo kesho ubungo Emaus kituo cha karesmatik kuna kongamano limeanza,muda SAA 3 had sits unafanyiwa deliverence na SAA 8 had 12 ndo Luna kongamano lenyew mahubir na maombez
Asantee mkuu nitajitahidi kuja.si ni pale ubungo??
 
Pole Sana hali hizo zinaweza kutokea.

Ila, hayo uliyoyaona na ndoto hizo zinataka kutumika kukukosanisha na watu wako wa Karibu.

Mfano, jitu lenye jicho moja linabeba sura ya rafiki /mtu wako wa Karibu.

Ushauri wangu kwako, jaribu kuwa makini na lifestyle yako mengine mbwembwe tu.
Asante kwa ushauri mkuu.kuna kitu nimekichukua kutoka kwako.
Hili la mtu wangu wa karibu inabidi niwe makini na mdomo wangu kuliko kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom