Wachawi wamemchukua mwanangu

Wachawi wamemchukua mwanangu

Joined
Aug 13, 2015
Posts
94
Reaction score
75
Wanajamvi ndugu yenu nimefiwa,

Nina majonzi sana na hasira kali moyoni mwangu, mke wangu alijifungua juzi saa 2 usiku katika hospitali ya wilaya ya Maswa, mtoto alikuwa wa kike na mwenye afya njema, mzuri wa sura na mchangamfu sana.

Jana mida ya saa 4 usiku tukashangaa kumkuta mtoto kalegea na anatokwa damu masikioni na mdomoni na hakuwa akihema, ikabidi tumkimbize hospitali haraka sana, kufika hospitali tukaambiwa ameshafariki dunia, sikumuuliza Dr ni nini kimemuua mwanangu nilikuwa nimechanganyikiwa, kufika nyumbani mwanangu sura yake ilikuwa imebadilika kabisa na siyo yake.

Mchana wa leo wakati maiti inaandaliwa kuvikwa sanda tumeona mambo yasiyo ya kawaida katika mwili wa mwanangu, mwili wake katika sehemu za mbavu umetobolewa tobolewa na kubadilika rangi ikawa kahawia, kucha zake zote zimekuwa nyeusi kama aliyevilia damu, mwili wake ni wa moto kama vile yu hai.

Wakati alikufa tangu jana usiku, amebadilika na kuwa mweupe kupindukia, nimemzika mwanangu kwa majonzi sana, naapa lazima nitalipa kisasi, roho inaniuma sana ndugu zangu, sina niliyemkosea.
 
Daaa.....ina huzunisha na kusikitisha sana
Pole sana mkuu kwa kupoteza uzao wako.
Naomba ufunge kwa wiki moja ukiongea na mungu
hakika utapata majibu ya duku duku lako.
 
Last edited by a moderator:
Dawa ya wachawi ni kupiga moto tu na dawa ya moto ni moto!
 
Pole sana ila kwa nini ume conclude ni uchawi. Hivyo ulivyoeleza vinaweza kuashiria kalogwa
 
Pole sana mkuu kwa kumpoteza malaika huyo.
Inashauriwa ukigundua mtoto amefariki katika nguvu za giza usimzike ungepambana na maombi mno na majibu yake ungeyaona ontime kama imani yako ni kama yangu lakin.
.
 
Muite Mungu naye atakuwa pamoja na wewe.
 
Pole sana Mkuu.

Mungu akupe nguvu na hekima katika kipindi hiki kigumu.
 
pole sana mkuu..ila utalipa kisasi kwa nani au huyo mchawi inamjua? muombe mungu akuongoze katika maamuzi yako..
 
Inauma sana, Pole sana kiongozi Mungu akupe nguvu katika wakati huu mgumu kwako.
 
Pole lakini siafikiani na wewe kusema utalipiza kisasi
Na wasiwasi na njia utakayotumia lakini nahisi utajiingiza kwenye tatizo lingne kubwa.ni muda wa kutulia
 
Back
Top Bottom