Point ya
mchami nadhani iko clear kwa wengi.
Bunge letu limetoka katika mstari wake sahihi, ambao ni kuisimamia serikali, limeiruhusu serikali isimamie bunge, kwa kuweka spika anayeamrishwa na muhimili wa utawala.
Wabunge wote wanaoonekana wanaibana serikali, hao wanaambiwa hawana nidhamu.
Lakini wabunge wanaokosa kuhudhuria, wanaolala bungeni, wanaochelewa, wasiotoa mchango wowote kuisaidia serikali kuendesha shughuli zake, hao ndio wabunge wema. Hawa wanaishi kwa raha bungeni, na posho zao zina uhakika.
Hao hawatasomewa kanuni kamwe.
Hao hawataitishiwa kikao cha kamati ya nidhamu ya bunge.
Hao hawatasimamishwa kuhudhuria vikao vya bunge.
Wananchi ni juu yetu kusema kama pesa yetu tunayokatwa kwenye kodi, inayotumika kuwalipa hawa wabunge mpaka wanakuwa tajiri kupindukia inatumika kihalali pale wabunge wetu wanapolala? Au kutoroka vikao? Au kuchelewa?
Asante
mchami kwa kutuwekea tafakari, ambayo umeiweka kwa namna ya mzaha, lakini inazungumza kitu cha msingi.