Wabunge watafuna Posho hovyo! CCM, CHADEMA wote washiriki mchezo mchafu

Naelewa jinsi ya kufanya retirement ila swali langu ni kuwa kila taasisi ina sheria za fedha (financial policy) hivyo si lazima iwe hivyo unavyosema kuwa kufanya retirement ni lazima. Na kama policy iko kimya (silent) inapaswa uulize kwa nia njema (in good faith). Kuna taasisi ambazo watu wenye vyeo fulani (executives) hawaulizwi kwa maana marejesho ya posho kinachotakiwa ni ripoti ya lengo analokusudiwa kulifanyia kazi; kaenda - hajaenda, kala - hajala, katuma mtu au kafanya mwenyewe. Na ndio maana swali langu la msingi ni kua sheria/kanuni zinasemaje hapa? Tuna miaka hamsini na mbili na bunge letu hili, je Nassari ni wa kwanza? Kuna wangapi huko nyuma walirudisha na kama hawakurudisha walifanya/walifanywa nini? Kwa nini ishu isiwe sheria/kanuni na usimamizi wake bali ishu inakua watu?

Nimekupata mkuu, inaonyesha hawa jamaa huwa wanazitafuna si unaona Zambi kuna ambazo alisema kuna ugeni wa katibu mkuu na kumbe kuna zingine za nyuma alipiga kimya. Ila speaker jana alisema waliochukua warudishe taratibu zinaeleweka. Nilichojifunza hapa kuna mazoea flani ambayo yamezoeleka kuhusu hizi posho za safari na hata za wakati wa bungeni mtu anasaini tu hata kama hayupo analamba mzigo iwe kwa viongozi wakuu au wa chini, yaani ni sawa na huku uswahilini uwe na boss anapenda fedha anaweza akasaini akasepa siku nyingine na wewe unalamba hela unasepa mwisho wa siku imekuwa mazoea
 
HIVI TUNAPOSEMA ARUDISHE PESA ZA WALIPA KODI; NI KWELI NI FEDHA ZA WALIPA KODI? AKIZIRUDISHA ZITATUFIKIA? Hii nchi ili urasimu uishe LAZIMA WATU WOTE WAONDOLEWE WAPANDWE WENGINE WAPYA! Anayebisha abishe nami nimpe mifano ya watu tuliowaita wazalendo kumbe ni sawa na kulala kwenye kitanda chenye kunguni mchana! Mkuu wa mkoa wa Kg aliwahi sema " SITAKI KUSIKIA HABARI ZA KILIMO CHA TUMBAKU KTK MKOA WANGU- ZAO HILI LINACHANGIA KIKUBWA KTK KUHARIBU MAZINGIRA", baada ya hapo; bodi ya Tumbaku taifa wakamchagua kuwa mw/kiti wa Bodi ya Tumbaku ATTT tanzania! Baada ya kuhudhuria kikao kimoja tu alikuja na kusema "WATU WOTE LIMENI TUMBAKU NI ZAO LINALO WEZA KUMWINUA MKULIMA KIUCHUMI". Nami nikakumbuka mikakati ya zamani kanisani kiuongozi " Mtu yeyote anayeikritisaizi dini mpeni cheo ktk dini hiyo" - utaona tu!

Observation nzuri kweli maana hapo kitakachofanyika ni kubadilisha matumizi tu
 
Mnamo mwaka 2010 #chadema waliwatangazia wananchi kuwa hawamtambui rais dr jakaya kikwete, swali: ni lini chadema wametangaza au walitangaza kuwa wanamtambua rais??? Swali la pili; chadema mwaka 2010 walitangaza kuwa hawatachukua magari ya kifahari, je ni lini chadema walitangaza kwa wananchi kuwa wamechukua hayo magari? Na pia chadema walitangaza mwaka 2010 kuwa hatachukua posho za bungeni, swali je ni lini chadema walitutangazia wananchi kuwa wamechukua hizo posho????

#tutaheshimiana
 
Back
Top Bottom