wabunge wameichoka dodoma

armanisankara

JF-Expert Member
Jul 15, 2011
283
49
wabunge wamechoka kukaa Dodoma katika kipindi hiki cha mkutano wa bajeti. hawataki yu kusema kuwa wamechoka mazingira ya mji huo na hata shughuli za bunge kwa kuwa bado wanazitamani posho nono wanazopewa. na kwasababu hii baadhi ya wabunge tena wengi tu wapo wapo tu huko bungeni ilimradi wana uhakika kila siku wanatia kibindoni posho. kwa kweli ni haibu kusikia kikao cha muhimu cha bunge kinaahirishwa kwasababu ya waheshimiwa hawapo ukumbini . ni kweli wamechoka na ndiyo maana hata wakiwa katika mazingira ya jengo la bunge baadhi yao utawaona tu wapo wapo nje ya ukumbi wa wa mikutano. wanachokifanya wanakijua wenyewe ili tu siku iishe wahesabu klichopatikana.
 
Walete arusha wakitoka ukumbini waende vwanja..dom hakuna vwanja zaidi ya UWANJA WA KATI a.k.a pombe ya nywele.
 
Hata wakienda Bungeni mawazo yao hayasikilizwi zimebakiwa tu ndioo ndioo na hata hao wa ndiooo nao wamechoka hasa kuna umuhimu gani wa bunge?

Sheria zenyewe zinazotakiwa kutungwa zinapitishwa kimiujiza bado wakitaka kuisimamia serikali kina Mandege wanaweka ukuta sasa unadhani kuna nini?
 
Ona kwa mfano mnyika hapa:-Niliuliza maswali mawili ya nyongeza; nilihoji ni lini serikali itatekeleza sera husika kwa kuwa upungufu wa ruzuku kwa shule za umma ni kati ya vyanzo vya kuporomoka kwa elimu kutokana na kuathiri uendeshaji wa shule ikiwemo upatikanaji wa vifaa shuleni, na kwa kuwa kwenye vyombo vya habari jana na leo kati walimu na wanafunzi wameeleza kwamba hali hiyo ni kati ya sababu za mgomo unaoendelea hivyo nikata serikali itoe kauli bungeni ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro unaoendelea.
Hata hivyo Spika wa Bunge alimkataza Naibu Waziri asijibu swali kuhusu mgogoro kati ya walimu na wanafunzi dhidi ya serikali na kutaka kujibiwa kwa swali ya lini ruzuku itaanza kutolewa kwa kuzingatia viwango vya sera hata hivyo serikali ilitaja kiwango cha fedha ya ruzuku kwa mwaka wa fedha 2012/2013 bila kueleza iwapo viwango kwa mujibu wa sera vitafikiwa kwenye ngazi zote ikiwemo katika shule za msingi.

Sasa kuna haja gani ya bunge kama sio kupoteza kodi zetu tuu.
 
Kwa namna bajeti zinavyopitishwa hivi sasa ni heri Bunge likaahirishwa kwa kuwa hakuna kinachohojiwa!
 
Back
Top Bottom