Wabunge Waliopita Bila Kupiñgwa

Wabunge Waliopita Bila Kupiñgwa

Pelekaroho

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2010
Posts
1,602
Reaction score
378
Mara zote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi kwenye uchaguzi mkuu, kumekuwa na wabunge hasa wa CCM ambao huwa tunaambiwa wamepita bila kupingwa. Napenda kufahamu kutoka majimboni je, ni wabunge gani ambao wamepita bila kupingwa. Karibuni tutaarifiane.
 
Hilo lilikuwa neno la kisiasa la kipindi hicho. Halikuwa tofauti na gori la mkono, sasa hivi ni ushindani hata kama ikitokea mgombea akawa mmoja hatuwezi kusema tena eti kapita bila kupingwa.
 
Hatuwezi tukakubali mtu akapita bila kupingwa tutasimamisha hata jiwe ili tulipigie kura!!!
 
Hatuwezi tukakubali mtu akapita bila kupingwa tutasimamisha hata jiwe ili tulipigie kura!!!

:amen: hakuna jiwe litaachwa bila kugeuzwa aka hakuna jimbo litapita bila kupingwa. :car:
 
Mara nyingine mtu kupita bila kupingwa siyo kwa sababu anakubalika, hapana, bali inatokana na rushwa au ghilba, kwa watu wanao onesha nia ya kutaka kugombea na wenye uwezo wa kushinda au kuleta changamoto ya nguvu kwa muhusika mkuu. Kama ilivokuwa kule Bumbuli kwa Januari Makamba na kule kwa Nimrod Mkono (kwa kutaja mifano michache)

Sababu za watu kupita bila kupingwa zingali zinaishi, na wahusika wamekuwa wakitumia mbinu tofauti kufanikisha malengo yao, kuna mahali katika uchaguzi wa 2010 wagombea wa CHADEMA, kwa maksudi walijaza fomu za kugombea kwa kufanya makosa, ambapo baada ya kukatiwa rufani na wapinzani wao walishindwa na hivo kukosa haki ya kugombea.

Nimeanzisha huu uzi ili kutoa angalizo kwa watendaji wa UKAWA kuwakumbusha kuwa, wanaosema bao la mkono wana mbinu nyingi na chafu kufanikisha malengo yao, kwa hiyo wawe na tahadhali za kutosha kwa watu wanaopitishwa kugombea katika ngazi tofauti tofauti yaani ubunge na udiwani na hata rais.
 
Kwamba hakuna mgombea wa UKAWA, ukonga.@ Hornet
 
Wagombea waliopita bila kupingwa kupitia CCM

Hizo mbwembwe sasa, mimi sizungumzii mchakato ndani ya chama fulani, ninazungumzia kama hakuna wagombea kutoka vyama vingine na ninadhani hiyo ndo maana ya kupita bila kupingwa katika zama hizi za vyama vingi.

Mchakato wa kumpata mgombea wa CHADEMA ulikuwa kama hapa chini

Matokea ya kura za maoni nafasi ya Ubunge Jimbo la Ukonga, uteuzi wa awali ni kama ifuatavyo;
Nixon Tugara 59
Asia Msangi Daudi 05
Benson Ntiruseswa 00
Deogratias Munishi 08
Deogratias Kalinga 00
Deogratias Mramba 05
Elly A. Dallas 15
Gasto G. Makwetta 01
Jamse D. Nyakisagane 00
Kalanga J Simbano 00
Lucas M. Otieno 06
Mwanaidi Ramadhani 00
Waitara M Mwikwabe 49
 
Hiyo zana yakupita bila kupigwa ilikuwa Enzi za mwalimu na hafi2010,ckuhizi ni mapambano ,ili kupata mtumishi wa kweli mana ccm wamekuwa wakitoa watumishi ambao wanasema milioni 10 nipesa ya mboga yani inasikitisha sana,
 
Lau Masha aliwahi kujishaua kuwa kapita bila kupingwa na anasubiri tu kuapishwa. From nowhere akatokea kamanda Wenje na kumkata mtama. Leo hii yuko wapi?
 
Kuna majimbo ambayo nimeona ni kama vile kupita bila kupingwa. CDM wameachia kwa wengine ndani ya UKAWA, ingawa ndo walikuwa na nafasi sana. Sasa, shida itakuja kuvielewa vyama vingine hata kama watakuja kwa jina la UKAWA.
 
Mambo ya zamani hayo sasa hakuna kupita kiulaini. Kazima upimwe ubavu.
 
Mambo ya zamani hayo sasa hakuna kupita kiulaini. Kazima upimwe ubavu.

Hapo juu nimesema kwamba kuna mbinu nyingi huwa zinatumiwa na hawa watu wanaopenda sifa ya kupita bila kupingwa, kwa mfano kufanya makosa ya waziwazi wakati wa kujaza fomu za kuomba uongozi. Nakumbuka moja ya makosa yaliwahi kuwanyima watu nafasi ya kugombea ni kujaza CHADEMA, badala ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo sehemu aliyotakiwa aandike chama ànachogombea.
 
Mara zote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi kwenye uchaguzi mkuu, kumekuwa na wabunge hasa wa CCM ambao huwa tunaambiwa wamepita bila kupingwa. Napenda kufahamu kutoka majimboni je, ni wabunge gani ambao wamepita bila kupingwa. Karibuni tutaarifiane.

Wabunge watakaopita bila kupingwa hawatokuwepo safari hii. Ila wabunge wanaosubiri kuapishwa ambao hawana haja ya kampeni wako wengi sana, kutoka UKAWA
 
Wabunge watakaopita bila kupingwa hawatokuwepo safari hii. Ila wabunge wanaosubiri kuapishwa ambao hawana haja ya kampeni wako wengi sana, kutoka UKAWA

Pamoja saana kamanda Shark
 
Back
Top Bottom