Uchaguzi 2020 Wabunge wa darasa la 7 na form 4 mwisho 2020

Luqman mohamedy

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
892
1,226
Habari wana Jf,

Naanza kwa kusema ni kweli katiba imeruhusu sifa ya muwakilishi wa wananchi ajue kusoma na kuandika tu na sio degree lakini;
Matatizo ya wabunge ambao hawakupata elimu ya juu katika kujenga hoja na kutoa michango bungeni tumeyaona,wengi wamekuwa wakirusha vijembe na kusema maisha binafsi ya wenzao badala ya hoja za msingi.

Ni kweli kuna lile swali tunalojiuliza "waliosoma wametufikisha wapi"?
Ila natoa tahadhari kama muwakilishi wako wa jimbo kaishia form 4 linapokuja swala la kujadili masuala mazito yanayowahusu kama uchumi ,teknolojia ,mifumo ya elimu,mikataba mikubwa huko bungeni yeye huwa sawa na bubu anachoishia ni kugonga meza tu.
Sidhani kama mtu wa darasa la 7 anaweza kubishana na data za waziri wa fedha wakati hata decimals na percentage kwake ni msamiati

Nadiriki kusema hili limeifanya siasa ya nchi yetu kuwa ya vijembe na sio hoja ndio maana wabunge wetu wanaongea kutengeneza clip na kurushiana maneno mtandaoni.

Elimu inaweza kumpa mbunge urahisi wa kwenda nje na kukutana na wafadhili wakakaa meza moja na kuongea lugha moja ya "kimaendeleo" simaanishi kingereza na wakaelewana.

Tutake tusitake ni lazima tukubaliane na mabadiliko ya karne hii,bila elimu utaburutwa tu

Namalizia kusema sidharau ambao hawajasoma ila najaribu kumtafuta atakayehoji kitu ambacho nnachotamani ahoji.Hata vitabu vya dini vimesema "HAWAWEZI KUFANANA WALIOSOMA NA AMBAO HAWAJASOMA"

Katiba imeruhusu ila sisi wananchi tukataeee "WABUNGE WA STANDARD 7 NA FORM 4 MWISHO 2020"

Qualification entry ya ubunge mtaani iwe ni at least Diploma.
 
Kuna wakati nasema bora hao f4 kuliko miprofesa. Nipe mafanikio 2 ya Prof Maghembe. Nchi hii std 7 hanatofauti na prof.
Mfano Kabudi anafanya nini zaidi ya kutoa mate, kutoa macho, kusifu na kuabudu?
 
Hoja nzuri. Mwingine anaweza kuwa na mawazo tofauti. Lakini wewe umetoa mawazo yako ya kufikirika. Naunga mkono hoja.
 
Unajisumbua, bora hao f4 kuliko miprofesa.
Nipe mafanikio 2 ya Prof Maghembe.
Nchi hii std 7 hanatofauti na prof.
Mfano Kabudi anafanya nini zaidi ya kutoa mate, kutoa macho, kusifu na kuabudu?
Prof:Kabudi ndiyo Vituko
 
una hoja ya kuzingatiwa hapo, tupaze sauti zetu angalau bunge lirudishe heshima yake kwa kuweka wasomi mle ndani
 
Akili sio za darasani peke yake... sana sana hao ambao hawajaenda shule ndio wenye kuwaendesha wasomi
 
Pendekezo la namna hii lilipelekwa ktk bunge la katiba 2014 lakini halikufua dafu, likafeli, na waliolifelisha ni hao hao wabunge ambao asilimia kubwa ndio waliounda bunge la katiba!!

Ila kiukweli ni aibu sana kwa Taifa letu kwa miaka hii kuwa na wawakilishi bungeni level ya std7 au form4

Ila na sisi wasomi tusiishie kulalamika humu mitandaoni, mwaka ndio huu tukachukue fomu tugombee,, Vilaza kama Kina Steve Nyerere, Harmonize, Wema wanapata ujasiri kwenda front kutangaza nia na usishangae baadhi yao wakaokota dodo October,,, wasomi tunakwama wapi!????

Au ndio tusubiri miujiza ya hao Vilaza eti wakaingie bungeni afu tutegemee wapitishe sheria ya 'kujichinja' ya mgombea Ubunge awe with minimal level of degree or diploma or equivalent..!????
 
Hongera sana kwa hoja nzuri ni kweli lisipoangaliwa hili itakuwa kama ile mikataba ya wakati ule ea alina MANGUNGO wa msovero ni kweli kabisa maana wabunge ndio watunga sheria na wasimamizi wa shughuli za serikali inakuaje wawe na elu ya std seven
 
Rasimu ya katiba ilikwama ....

std 7 ndo wenyehela zinazowapitisha, Elimu kwa jamii hasa vijijini ni tatizo ambako ndo wapigakura kuliko wasomi., automatic hata kwa takrima za kofia watawapa kura tena.
 
Huo ndo ukwel hawa std7 wakjitahid sana ni kumezeshwa point1 bas.. mle ndan wakijaa wasomi lazima kutawaka kwa hoja.. sio sasa kelele nyiing
 
Back
Top Bottom