Wabunge wa CCM na mjadala wa Wabunge wa Chadema kususia Hotuba ya Rais

Gurtu

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,247
342
Wabunge wa CCM siwaelewi kwa mambo yafuatayo:
1. Wanapoteza muda mwingi kujadili suala la wabunge wa Chadema kususia hotuba ya rais siku ya uzinduzi wa bunge la 10.

Wenzetu wanachadema wametoka bungeni, wananchi tuliowachagua tunalifahamu hilo. Wananchi tuachieni jukumu letu, sisi tutaamua kama wanatufaa au hawatufai. Wabunge wa CCM kama mnataka kujadili hotuba ya rais jadilini hilo linatosha. Wabunge wa CCM mnapoteza muda wenu mwingi kumpongeza rais wakati sisi huku tunakabiliana na mgawo wa umeme. Matatizo yetu ni mengi kiasi kwamba kama wabunge wetu wangekuwa na akili timamu na muda wa kujadili wenzao.

Kwa kuangalia haraka haraka hotuba ile ya rais haikuwa na kitu cha maana kinachotoa mwelekeo wapi taifa letu lilipo na wapi linapaswa kwenda. Amezungumzia mambo kama nadhari katika vitabu. kama wabunge wanaogopa kupingana na rais wao bora wao wakae kimya.kumpongeza rais kwa sababu tu watu wanaona ni 'fashion' ni upuuzi wala si kazi iliyowapeleka bungeni.
 
Pumbavu kabisa hawa wabunge badala ya kujadili kwa nn hatuna umeme mnabaki kujadili hotuba ya JK. Jadilini kwa nn matokeo ya kidato cha 4 yako yalivyo sio kupoteza muda tu.
 
Kama dk 2 hivi nimetoka kumsikiliza Job Ndugai naibu spika wakati akiahirisha mkutano wa bunge akisema kwamba, tabia ya wabunge kutoka wa-Tanzania wameona na ndio watakoamua mustakabali wao akimaanisha kwamba tendo hilo linawaumizi sana wa-Tanzania.

Ukweli ni kwamba kwa wanamageuzi wote hakika wanaliunga mkono tendo hilo. Tena ccm itambue kwamba wao ni mti wanaoukata wenyewe kupitia madhaifu mengi wayafanyayo kwa wananchi na wanaturahishia kazi, kama hili la kubadili kanuni za bunge ili tu kuzuia nguvu ya upinzani, nawaasa waelewe siku si nyingi wao watakuwa wapinzani sasa sijui kanuni hizi zitafanyiwa tena marekebisho au??
 
NGUVU YA UMMA TUNAKUJA KUWATOLEENI MAAMUZI MAZURI ZAIDI KWENYE KILA SWALA LA GHILIBA FITINA NA USALITI WOWOTE UTAKAOTOKEA HAPO BUNGENI WALA MSIWE NA WASIWASI; MACHO YOTE KWENU

 
Kwani ni asilimia ngapi ya wananchi walitoa maoni kwamba hawapendi tabia ya Chadema kutoka nje bungeni? Waliohojiwa ni wapiga kura wa ccm au wa Chadema?
 
Achana na waota ndoto hawa! wabunge wa ccm ni mbumbumbu wa karne hii. Majibu yanatayaarishwa na sasa hakutakuwa na kuibiwa maana tutaondoa vichwa vya wachakachuaji mchana kweupe. Hatutajali risasi zao. Gharama za maisha yetu itakuwa vichwa vyao.
 
Back
Top Bottom