Wabunge wa CCM hawana mamlaka ya kumwachisha kazi Waziri; JK awatosa!

Siyo lazima wapeleke hoja bungeni. Kama wamekubaliana mawaziri wajiuzulu, basi wawaache wajiuzulu.Bungeni, labda waziri mkuu akijiuzulu ndipo mawaziri automatically watakuwa hawana lao. Mawaziri wote!
Another option ni kuwapeleka ethics tribunal.
Kuepuka bureaucracy na fedheha, bora waandike barua za kujiuzulu, mambo mengine yaendelee.

Sawa. Lakini nauliza tena, "wasipojiuzulu"; nikimaanisha kwamba, barua zao zisipokubaliwa na mwenye mamlaka ya uteuzi, hiyo "caucus" ya CCM itafanya nini?
Ndiyo maana naungana na Mag3 katika kuamini kwamba, wabunge wa CCM wameshindwa kutumia wingi wao katika kuweza kupitisha ajenda muhimu ya kitaifa. Wange-table hiyo hoja, waliyojadili ndani ya "caucus" hakika wangekuwa wame-revolutionise siasa za Tanzania. Kwani hoja yao ingeungwa mkono kwa kiasi kikubwa na wabunge kutoka minority camp, na hapo ndipo wangekuwa wamemtega vizuri "mwenye mamlaka ya uteuzi".
Lakini kwa hicho walichokifanya "wenyewe tu" ndani ya caucus,hakika narudia kusema ni mazingaombwe.
 
Caucus ni mkutano wa watu wenye lengo moja, thats it. Caucus ni jina tu linaweza kutumika kumaanisha mkutano au kundi la watu wenye nia ya ku push agenda fulsani. Thats all, acheni ubishi jamani, mnachekesha.

Mzee naelewa caucus ni nini. Na hapa ninachoongelea ni caucus ya CCM.
Kwa kutumia caucus yao, je, CCM wameweza ku-push hiyo ajenda yao? Jibu nafikiri unalo, hawajafanikiwa.
 
Mzee naelewa caucus ni nini. Na hapa ninachoongelea ni caucus ya CCM.
Kwa kutumia caucus yao, je, CCM wameweza ku-push hiyo ajenda yao? Jibu nafikiri unalo, hawajafanikiwa.
Hicho siyo kinachozungumzwa hapa. Issue ni kuwa Caucus haina mamlaka au uwezo, mimi sikubaliani nalo hili.
Caucus ina uwezo wa kuwawajibisha mpaka JK.... all they need is to grow some balls!!
 
Rafiki yangu timbilimu, hapa tujibizane kwa hoja ukitaka ku-discredit uwezo wa watu utakuwa umechemsha sana, maana wewe hunijui wala mimi sikujui lete fact siyo personal attacks, uwezo wangu mimi ninaujua mwenyewe na wala siwezi kuusemea uwezo wako ila kwa taarifa tu mimi siyo mtu wa kuongea bila facts, fuatilia post zangu zote kama unaweza ujiridhishe.

Ukija kwenye suala la uwezo wangu kama utafanikiwa kunijua kwa CV yangu utajiona mwenye bahati sana kupata reply kutoka kwangu. I believe that in JF everyone is a critical thinker so I respect your contributions, but will agree with them when are facts proven.

Kwa taarifa yako tu ni kwamba Wabunge wa CCM au Bunge hawana uwezo kumuondoa waziri aliyeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya muungano. Ila wanaweza kumpigia kura ya kutokuwa na Imani waziri mkuu kama wanataka kundoa mawaziri wapige kura hiyo ambayo automatically itakuwa ime-dissolve cabinet. Ila hawawezi kwenda kwa Ngeleja au Nundu na kumtaka aondoke uwezo huo hawana kwa mujibu wa katiba.

Mfupa hauna ulimi....
 
Napenda kuuliza kitu kimoja. Tangu wenyeviti wa kamati za bunge walipobainisha ubadhirifu kwenye wizara mbalimbali, umepita muda gani wa kuchunguza tuhuma hizo ili itoshe kusema kuwa mawaziri hawafai kwa kushindwa ku-act. Kama niko sawa,ni less than 1 week tangu wenyeviti walipowasilisha ripoti ka kamati zao. Je tumewapa muda mawaziri hawa kubainisha ukweli wa tuhuma hizi?
Watanzania wenzangu:
Tusiwe too emotional kwenye masuala nyeti na hasa katika mustakabali wa taifa letu. Nchi haiwezi kuendeshwa kwa ushabiki wa kivyama kiasi kwamba hata mihimili ya dola isiachwe ikafanya kazi independently. Tunajenga demokrasia ya aina gani ambayo mtu anahukumiwa kabla ya kujitetea na kujiridhisha kuwa yuko guilty au la! Kwa yeyote ambaye alishafanya kazi either kwenye shirika la umma,binafsi,taasisi au popote,atakubaliana nami kuwa makosa ya kiutendaji hutokea. Katika misingi ya uadilifu,lazima tuhuma zichunguzwe,na atakayebainika kutenda kosa aadhibiwe kwa mujibu wa sheria.
CAG kawasilisha ripoti zake za ukaguzi. Kuna sehemu yeyote katika ripoti yake amebainisha specifically kuwa waziri fulani ameiba kiasi fulani cha fedha? Kama hakuna,yaweza kuwa ni ubadhirifu ambao umetokana na wetendaji walioko chini yake,inatakiwa msingi wa ubadhirifu huo uchunguzwa,na hapo ndio tunajenga hoja ya kuwa kiutendaji waziri amehusika kwa kiwango gani ili hatua zichukuliwe. Tujifunze kutenda haki hata kama haki itaenda kwa mtu tusiyempenda. Tatizo kubwa ninaloliona ni kuwa kuna media exaggaration kwenye kila kitu katika serikali,na hii ni hatari sana kama hatutachuja yale tunayoyasoma au kusikia kwenye hivi vyombo vya habari. Naendelea kuamini kuwa haki au tuhuma dhidi ya mtu haziwezi kuwa prooved magazetini. Hili ni kosa kubwa mno watanzania. Tunataka uhuru wa vyombo vya habari,lakini tuna uhuru wa kuchuja pia. Tusisahau kuwa haya magazeti yanamilikiwa na watu, na hata wanasiasa waliojipambanua kupigania haki zetu.! Tuhuma zinaanzia kwenye magazeti,wananchi wanaandaliwa kisaikolojia kuwa kilichoandikwa ndio ukweli,mtuhumiwa hana haja ya kusikilizwa. Na lolote atakalosema baada ya kuandikwa gazetini haina maana kwetu.Huu ndio uhuru wa habari na athari zake? Kumbukeni kuwa,chama chochote cha siasa lengo lake ni kushika dola,but we must not accomodate bullying over the victims of this journey. Unfortunately hata bunge linajiendesha kwa style hii. Itikadi za kisiasa mbele ya maslahi ya wananchi.
Wabunge wa CCM:
Kama watu ambao kwa upande wangu nitawaona wanafiki ni hawa wabunge wa CCM. Samahani kama nimemjeruhi mtu katika hili. Ni wabunge hawahawa ambao wamekuwa wakilalamikiwa kwa kupitisha miswada na hoja za hovyo,na kupiga meza kukubali hata lisilotakiwa kukubali. Ambao walikuwa mstari wa mbele kudai nyongeza ya posho. Rais kakataa kupitisha hizo posho,tayari ishakuwa kinyongo dhidi ya serikali. Do you think JK angepitisha zile posho leo kuna mbunge wa CCM angethubutu hata kuunga mkono hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu? Ni unafiki gani huu?
Turekebishe mfumo wa utendaji serikalini,hapo ndio kwenye tatizo. Kumfukuza kazi waziri ambaye anafanya kazi kwenye mfumo m-bovu haitasaidia kitu. Tutegemee miujiza gani kwa mawaziri wakati mfumo tulionao ni wa hovyo? Naamini katika mageuzi,naamini katika haki na uadilifu.!
Nawasilisha.
 
Hicho siyo kinachozungumzwa hapa. Issue ni kuwa Caucus haina mamlaka au uwezo, mimi sikubaliani nalo hili.
Caucus ina uwezo wa kuwawajibisha mpaka JK.... all they need is to grow some balls!!

Mzee unasahau hata unachokisema!!

Ni kweli, party caucus ina nguvu sana hata ya kumwajibisha JK. Lakini ninavyoelewa kwamba bila ya ku-table hoja zao ndani bungeni, hayo yatakuwa mazingaombwe tu mzee.

Kwa maana hizo caucuses za CCM zimeshakuwepo tangu enzi za kina Jairo et al., lakini moves hizo hazikuweza kuzaa uwajibikaji unaousema!!

Kama unaendelea kuamini kwamba bila ya hoja kuwa tabled, waziri au JK anaweza kuwajibishwa na party caucus, basi mzee, nafunga mjadala nawe.
 
kuna tetesi kuwa baraza la mawaziri litavunjwa hivyo hakuna haja ya mawaziri kujiuzulu kama wengi tunavyotegemea.

Wenye habari watujuze tafadhali Kwa upande wangu mimi naona kama litavujwa haitokuwa sawa kwani serikali itakuwa imewaachia huru wale wote wanahusika uchafu uliofochuliwa na CAG. ila kama litavinjwa basi wahusika wachukuliwe hatua na sio danganya toto kama kesi ya EPA ya Yona na mwenzake Mramba.
 
Hakuna kuvunja kitu wajiuzuru kwanza hao 7 ili wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria kwani watakua wametuthibitishia maovu yao.
 
Hakuna kuvunja kitu wajiuzuru kwanza hao 7 ili wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria kwani watakua wametuthibitishia maovu yao.

Mkuu unazungumzia serikali ipi? Na usishangae wakabadilishwa kuwa wizara tofauti ila wakabaki kuwa mawaziri. Serikali ya baba riz zaidi ya uijuavyo
 
....Wabunge wa CCM sijui wametumia kipengele gani cha katiba ya nchi au hata ile ya CCM kuwashinikiza Mawaziri waachie ngazi. Walichotakiwa kufanya ni kumshinikiza Mwenyekiti wa Magamba Msanii Kikwete kuwatosa Mawaziri wote ambao utendaji wao umekuwa zero.

Ni aibu nyingine kubwa kwa Kikwete kushindwa kuwawajibisha Mawaziri wake wengi ambao wamekuwa wakivurunda kila kukicha na kusubiri hadi Wabunge wafanye hivyo.

Kilichofanywa na Wabunge hawa ni kulinda maslahi yao kati ya sasa na uchaguzi wa 2015 ili hatimaye waweze kuchaguliwa tena kwa kutumia kete ya kwamba "waliwawajibisha" Mawaziri wazembe.

Wameona anguko la chama chao linakuja kwa kasi kubwa na hivyo kutishia usalama wao wa kuchaguliwa tena katika uchaguzi wa 2015 na hivyo kuamua kukurupuka ili kulinda maslahi yao, kama kweli wanekuwa wanataka kulinda maslahi ya Tanzania na Watanzania basi wangeishinikiza Serikali yote ijiuzulu ili kupisha Serikali ya muda kwa kipindi cha miezi 12 hadi 15.

Mkuu,binafsi nina wasiwasi sana juu ya uamuzi utakaotolewa na JK,kama walishindwa kuwawajibisha mafisadi ndani ya chama hili la mawaziri litawezekana?
 
Mkuu,binafsi nina wasiwasi sana juu ya uamuzi utakaotolewa na JK,kama walishindwa kuwawajibisha mafisadi ndani ya chama hili la mawaziri litawezekana?

KIKWETE ameshawaambia kuwa hizi ni BLABLA tu zitapita.

Ameshagoma kuwawajibisha marafikia zake (Mawaziri)

CCM INAKUFA MIKONONI MWA KIKWETE KABLA YA 2015, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA TU!!!!



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Good. Sasa tatizo lipo wapi kama wabunge ambao wamechaguliwa na wananchi (regardless of party affiliation) wakawawajibisha mawaziri baada ya kupokea ripoti kutoka kwa CAG?
Labda sijakuelewa, that was a caucuss meeting ya wabunge wa CCM na wameamua kuwashikia kidete mawaziri. Only CCM MPs can do that.
Wapinzani, hata ku-caucuss kwa ajili ya posho wameshindwa na bado wanazila kama kawaida. Only CCM Mps can change the government. Hata kama rais angekuwa Mbowe au Mtei.
So what's da beef???
Rather unprofessional argument!!
 
Hapa ni patamu lakini ndugu zangu wana CCM, CHADEMA, CUF, TLP nk niambieni ni chama gani kina uchungu na nchi hii? ukienda CCM wenye majina makubwa hawakusaini kuwawajibisha mawaziri na jingine kwanini upigaji kura ulichukua muda? nilifikiria idadi ya wapiga kura wabunge ingezidi nusu na zoezi lingechukua muda mrefu mmno kuonyesha kukerwa. Naamini wabunge wengi 85% + ni maduwanzi hawakerwi na ufisadi na ubadhilifu wa mamilioni ya pesa za wananchi. Kumbe wananchi walipiga kura kuchagua manunda. Kama mawaziri+wabunge wako hivyo je mwananchi aliyemchagua si viazi tu?.
 
Back
Top Bottom