Wabunge mkinijibu maswali haya endeleeni na vikao vyenu, vinginevyo mnaitia hasara serikali bure

ibesa mau

JF-Expert Member
Sep 17, 2015
2,109
1,692
Eti mpo bungeni mnasema mnapanga na kujadili bajeti ya serikali , mnapanga ni maeneo yepi fedha ya serikali ielekezwe .

Sasa naomba mnijibu maswali yafuatayo na kama mkishindwa mrudi majimboni kwenu mkasaidie wapiga kura wenu.

1: Ni lini mliwahi kukaa bungeni kujadili na kupanga ununuzi wa ndege zilizonunuliwa. Na kama hamkukaa ni nani aliyeidhinisha fedha hizo

2: Ni lini mlikaa bungeni kuidhinisha fedha kwa ajiri ya utengenezwaji wa viwanja vya ndege vya chato, mwanza ,n.k. Kama hamkukaa ni nani aliyeidhinisha mabilioni hayo kuelekezwa huko,

3: Nyinyi wabunge ndio mliokuwa mmepanga mabilioni ya shilingi kwa ajiri ya sherehe mbalimbali za kitaifa , lakini serikali ikafuta maadhimisho hayo na serikali ikaelekeza fedha hizo kwenye maeneo mengine, uamuzi ambao ulifurahiwa na wananchi wenu walio wapigia kura. Je wakati mnapanga hamkuona kwamba sherehe hizo hazina tija hadi mtu mmoja aje atuonyeshe mwanga , ina maana kwamba mtu mmoja ana akili kuliko nyie mia tatu mnao kaa hapo bungeni.

4: Kwanini muendelee kukaa bungeni miezi miwili huku mkijilipa posho kwa fedha ya walala hoi wakati mnachokipanga si ndicho serikali itakacho tekeleza, inahitji mtu afike darasa saba ili kugundua kwamba nyie mnapanga yenu na serikali inatekeleza yake? .

5: Kwa nini bunge hili la awamu ya tano msibaki na kazi moja tu ya kutunga sheria , sera na miongozo ya nchi ambapo vikao vyake ni vya wiki mbili tu na kazi ya kujadili, kupanga na kuidhinisha matumizi ya fedha ya serikali muiachie serikali ambayo ndiyo mkusanyaji na tayari wanachi tumeshaona tija yake leo hii uamuzi wa mtu mmoja wa kuamua kununua bombadier umefurahiwa na kila mtu .

Kuendelea kukaa bungeni ni kutumia fedha ya mlalahoi ovyo, kwa sababu watanzania wanaona uamuzi wa raisi wetu kuchukua fedha za serikali kuelekeza kwenye mambo anayo yaona yana tija kwa wananchi ni mzuri kuliko yale mnayompangia nyie huko na watanzania tumeridhika .lakini jambo la pili fedha zenu mnazo zipangia matumizi zina mlolongo mrefu wa kupatikana na kuzifanyia matumizi, lakini hiyo kazi kwa kipindi cha miaka miwili tumeshaona faida yake raisi akifika sehemu akakuta kuna matatizo ya maji , barabara hapo hapo anaagiza tu barabara itengenezwe wiki mbili hakuna longolongo inatengenezwa bila kujali fedha itatoka wapi.

Ushauri wangu kusiwe na bunge la bajeti kuwe tu na vikao vya bunge vya kawaida vya wiki mbili ili fedha itakayo okolewa ikafanye kazi nyingine za kimaendeleo. Kwa sababu kwa serikali ya awamu hii ya tano inaweza kwenda bila hata bunge na shughuri zikaendelea kama kawaida kwa sababu kila mtu anajua raisi ni mkali hivyo watu wanaogopa kufanya kazi kwa mazoea.

Kwangu mimi bunge ni mzigo mwingine kwa serikali unaotumia fedha nyingi halafu tija yake haionekani kwa wananchi , bunge halina tofauti na mwenge yote ni ni mizigo tu tofauti yake ni kwamba mwenge ni mzigo unaotembea wakati bunge ni mzigo uliotulia unaotafuna fedha kimya kimya.

Wabunge mjitafakari wenyewe kama mnapaswa kuendelea kuwa bungeni au la. Lakini mjue Mungu anawaona.
 
karibuni tujadili kwa misingi ya nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu.
 
Hawajauliza hatima ya ajira,mikopo ya vyuo na hatima ya haki za watumishi toka wakae Dodoma wanauliza mambo ya matukio ambayo yanapita. 2020 inawahusu na inawangojea.

Kundi la wazazi, walezi wanaosomesha vyuo au watoto wasio na ajira,vijana wahitimu na wafanyakazi linawasubiri 2020.
 
Hili Swala ni gumu kwa Wabunge wetu wa Kiafrika,wengi wamo mule kwa Maslahi yao binafsi na si Taifa,kifupi ni Wachumia Tumbo aka Wasaka Tonge so kuwaambia wasiwepo mjengoni ni sawa na kuwaambia wafe njaa kitu ambacho ni kigumu! Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameroon aliachia ngazi sababu kile anachokiamini kuhusu kuwepo kubaki kwa nchi yake katika Umoja wa Ulaya ama Kujitoa kinatofautiana na Wanaichi wake akaachia ngazi hivi kuna kiongozi gani wa kiTZ Na kiAfrika anaeweza kufanya hivyo?? Kama Mtu anashindwa dhahiri kabisa ktk Uchaguzi Na Anagoma kutoka Madarakan? Kwa wenzetu Uongozi ni Wito Na Dhamana tu ila kwa Afrika Uongozi ni Uungu MTU,Umangimeza,Umimi,Umwinyi nk nk hivyo hayo unayowaza na kiwaambia Wabunge YASAHAU na kama UNASHUGHULI zingine endelea nazo tu
 
Eti mpo bungeni mnasema mnapanga na kujadili bajeti ya serikali , mnapanga ni maeneo yepi fedha ya serikali ielekezwe .

Sasa naomba mnijibu maswali yafuatayo na kama mkishindwa mrudi majimboni kwenu mkasaidie wapiga kura wenu.

1: Ni lini mliwahi kukaa bungeni kujadili na kupanga ununuzi wa ndege zilizonunuliwa. Na kama hamkukaa ni nani aliyeidhinisha fedha hizo

2: Ni lini mlikaa bungeni kuidhinisha fedha kwa ajiri ya utengenezwaji wa viwanja vya ndege vya chato, mwanza ,n.k. Kama hamkukaa ni nani aliyeidhinisha mabilioni hayo kuelekezwa huko,

3: Nyinyi wabunge ndio mliokuwa mmepanga mabilioni ya shilingi kwa ajiri ya sherehe mbalimbali za kitaifa , lakini serikali ikafuta maadhimisho hayo na serikali ikaelekeza fedha hizo kwenye maeneo mengine, uamuzi ambao ulifurahiwa na wananchi wenu walio wapigia kura. Je wakati mnapanga hamkuona kwamba sherehe hizo hazina tija hadi mtu mmoja aje atuonyeshe mwanga , ina maana kwamba mtu mmoja ana akili kuliko nyie mia tatu mnao kaa hapo bungeni.

4: Kwanini muendelee kukaa bungeni miezi miwili huku mkijilipa posho kwa fedha ya walala hoi wakati mnachokipanga si ndicho serikali itakacho tekeleza, inahitji mtu afike darasa saba ili kugundua kwamba nyie mnapanga yenu na serikali inatekeleza yake? .

5: Kwa nini bunge hili la awamu ya tano msibaki na kazi moja tu ya kutunga sheria , sera na miongozo ya nchi ambapo vikao vyake ni vya wiki mbili tu na kazi ya kujadili, kupanga na kuidhinisha matumizi ya fedha ya serikali muiachie serikali ambayo ndiyo mkusanyaji na tayari wanachi tumeshaona tija yake leo hii uamuzi wa mtu mmoja wa kuamua kununua bombadier umefurahiwa na kila mtu .

Kuendelea kukaa bungeni ni kutumia fedha ya mlalahoi ovyo, kwa sababu watanzania wanaona uamuzi wa raisi wetu kuchukua fedha za serikali kuelekeza kwenye mambo anayo yaona yana tija kwa wananchi ni mzuri kuliko yale mnayompangia nyie huko na watanzania tumeridhika .lakini jambo la pili fedha zenu mnazo zipangia matumizi zina mlolongo mrefu wa kupatikana na kuzifanyia matumizi, lakini hiyo kazi kwa kipindi cha miaka miwili tumeshaona faida yake raisi akifika sehemu akakuta kuna matatizo ya maji , barabara hapo hapo anaagiza tu barabara itengenezwe wiki mbili hakuna longolongo inatengenezwa bila kujali fedha itatoka wapi.

Ushauri wangu kusiwe na bunge la bajeti kuwe tu na vikao vya bunge vya kawaida vya wiki mbili ili fedha itakayo okolewa ikafanye kazi nyingine za kimaendeleo. Kwa sababu kwa serikali ya awamu hii ya tano inaweza kwenda bila hata bunge na shughuri zikaendelea kama kawaida kwa sababu kila mtu anajua raisi ni mkali hivyo watu wanaogopa kufanya kazi kwa mazoea.

Kwangu mimi bunge ni mzigo mwingine kwa serikali unaotumia fedha nyingi halafu tija yake haionekani kwa wananchi , bunge halina tofauti na mwenge yote ni ni mizigo tu tofauti yake ni kwamba mwenge ni mzigo unaotembea wakati bunge ni mzigo uliotulia unaotafuna fedha kimya kimya.

Wabunge mjitafakari wenyewe kama mnapaswa kuendelea kuwa bungeni au la. Lakini mjue Mungu anawaona.
Kwa kifupi hamna haja ya bunge
 
Hadi sasa, cjaona umuhimu wa bunge hili la awamu ya tano, naona kama wanachezea kodi za watanzania tu.
Naunga mkono kauli ya RC Makonda kwa wabunge hawa.
 
Bunge ni muhimu,lakini lina idadi kubwa ya wabunge kuliko uwezo wa taifa,hata kuchangia hoja muda ni mdogo sana
Ulisahau kuwa wabunge wengine wanaigia bungeni na agenda zao kinyume na matakwa ya majimboni kwao.
 
Ata presda ameshawaona hawana lolote, maaana kla ktu anawapangia yy halafu kashagundua hawana umoja wa kuleta chachu ktk taifa kashajua kucheza na akili zao bila shaka wamekuwa chuma ulete kwa serikal hii ya mtukufu
 
Huyu dikteta hata atakapovunja katiba (ndiko tuendako) na kutawala milele, wabunge hawatasema lolote zaidi ya kuchekacheka mithili ya msichana aliyekumbwa na pepo la ngono.
 
Bunge letu halina uwezo wa kupanga budget nzuri kazi hii iachiwe serikali na tuna imani na mh Rais na viongozi wa kiserikali kuliko kutupangia hawa wabunge.Kiufupi bunge la budget halina tija
 
Bandiko kama una pointi, ila unaharibu kusema waTanzania "tunaridhika". Jisemee wewe tu na wananchi wa mtaa wako kama mnaridhika. Kuridhika au kutokuridhika kwa WaTz ni utafiti utakaotolewa na "Twaweza" hapo baadae.

Pointi ya msingi ni kuwa bunge libaki na kazi moja tu ya "kupitisha miswaada ya serikali"
Sheria zinatungwa na serikali zinapelekwa bungeni kupitishwa basi. Hata wakisema hii sheria ni mbovu isipite, ilimradi serikali imeamua, itapita tu. So hawana kazi, wabaki tu na kazi ya kuipitisha miswaada ya serikali for record keeping.
 
Hili la ndegr na miundo mbinu ya Mwanza lipo kwenye bajeti husika. Magufuli amekuwa mjanja kwa kubeba credit tu. Otherwise jipya hakuna hapo ndio maana kina ZZK wapo kimya.
 
Back
Top Bottom