Nadhani ulikuwa unataka kuchekesha watu jukwaani lakini ukweli unaujua.
Anza kujadili kwanza tutaondoaje umasikini kwa hawa raia wetu wanao ishi kwa Tsh 650 kwa siku na ni kwanini serikali ambayo imeaminiwa miaka 50 imeshindwa kutoondolea hilo, ni yupi inatakiwa awe wa kwanza kuondolewa yule aliyepewa miaka hamsini akaishia kutengeneza watu kama wewe wanaofikiria kwa matumbo baadala akili kwasababu unaamini propoganda ndizo zinatatua matatizo.
Ni vizuri tukajitofautisha na kina Lusinde na mwigulu na wenzake kwa kuwambia nini hasa inatakiwa kifanyike kututoa hapa tulipo kuliko kuendelea kuwatumbukiza watu kwenye umasikini usio na kifani wakati wamekalia kila aina ya utajiri
Yaani mimi napafahamu Moshi ndugu yangu.
Pale ukizungumzia CCM limebaki jina tu na vitega uchumi vyake. Siongei kwa ushabiki kwa sababu sipo CCM wala Sipo Chadema. Akiondoka mzee Ndesa wale watu wa pale watachagua chama cha Chadema na sio mtu.
Na ni sababu Chadema ina nguvu sana kuliko chama chochote pale.
Na hata Cirily Chami naye sidhani kama ataweza kusurvive 2015 pale.
Na kwa Ubungo ninachojua ni kuwa Mnyika ana nguvu sana na Chadema ina nguvu sana.
TUZUNGUMZE KWA FACTS NA SIO KWA USHABIKI.
Ni kama Vunjo pale Mrema ana nguvu sana yeye kama yeye sidhani kama TLP ina nguvu yoyote
Hapo umenena vema.Nadhani ulikuwa unataka kuchekesha watu jukwaani lakini ukweli unaujua.
Anna Makinda.
Job Ndungai
Lusinde
January
Wassira
Nchemba na wengineo wengi umesahau maana 2015 CCM ndo itakuwa chama cha upinzani
Mkuu mimi naona ungekamilisha list kama ungemaliza na Mhe. Mbowe, huyu jamaa wananchi wa Hai walikuwa hawajui kama kala sifuri kidato cha sita (6), sasa wamejua na wamechachamaa kwelikweli, wamesema hata awape Bilicans bungeni awamrudishi.
Watu kuishi kwa Tshs. 600 kwa siku sio kigezo toshelezi kusema kuwa wana maisha magumu, hii ni kwa sababu wananchi wengi wa kijijini hawatumii fedha kwa kiasi kikubwa katika mahitaji yao, mfano mdogo tu, mtu anaelima bustani yake na akaweka mihogo na ikikomaa anachemsha maisha yanaenda, hawa ndio wamejaa huko mikoani, awahitaji fedha kwa kiasi kikubwa ili kuendesha maisha. Hemu elewa hili mkuu na wote wenye fikra kama zako.