Abdull Kazi
JF-Expert Member
- Dec 29, 2012
- 322
- 255
Wabunge 19 wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,wanaosubiri hatma yao kwenye kikao Cha baraza kuu,wameingia katika mateso makubwa baada ya kutopatiwa Chakula tokea walipoingia Ukumbini humu,huku wakitakiwa wasioende popote Bila ya Ulinzi wa vijana wa Chama.
Hata wakati wa Mapumziko ya Chakula wabunge hao hawakupewa nafasi ya kushiriki mezani na wenzao kwa maelezo kuwa Bajeti yao haijawekwa.
Hata baadhi yao walipotaka kuinuka kwenda kujitafutia rizki walizuiwa kwa maelezo kuwa hawaruhusiwi kutoka katika eneo hilo mpaka uamuzi ufanyike.
Kwa mujibu wa viongozi tangazo la kubariki uamuzi wa Kamati kuu ya Chama utatolewa ifikapo saa nane usiku.
Tayari mmoja wa vijana wa Chama mwenye wafuasi na wengi mitandaoni,amepewa jukumu la kuuandaa umma juu ya uamuzi huo ikiwa ni pamoja na kueleza kuwa wabunge hao wamefika na vijana kutoka Bunda Mkoani Mara kwa ajili ya kufanya vurugu.
Hata wakati wa Mapumziko ya Chakula wabunge hao hawakupewa nafasi ya kushiriki mezani na wenzao kwa maelezo kuwa Bajeti yao haijawekwa.
Hata baadhi yao walipotaka kuinuka kwenda kujitafutia rizki walizuiwa kwa maelezo kuwa hawaruhusiwi kutoka katika eneo hilo mpaka uamuzi ufanyike.
Kwa mujibu wa viongozi tangazo la kubariki uamuzi wa Kamati kuu ya Chama utatolewa ifikapo saa nane usiku.
Tayari mmoja wa vijana wa Chama mwenye wafuasi na wengi mitandaoni,amepewa jukumu la kuuandaa umma juu ya uamuzi huo ikiwa ni pamoja na kueleza kuwa wabunge hao wamefika na vijana kutoka Bunda Mkoani Mara kwa ajili ya kufanya vurugu.