Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
WASOMI na wanasiasa wamesema kitendo cha Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kuirejea kauli yake ya kukemea mashangingi kinaonyesha jinsi mtendaji huyo mkuu wa serikali asivyojua wajibu wake na kutokuwepo kwa uwajibikaji.
Juzi akiwa mjini Dodoma, Waziri Pinda alisema kumekuwa na mashindano ya mawaziri kununua magari ya kifahari, badala ya kupunguza matumizi na kuwasaidia Watanzania masikini.
Waziri Pinda, ambaye alikuwa nje ya nchi kwa ziara ya kikazi, alionyesha kushangazwa na jinsi viongozi wa serikali ya India wanavyotumia magari ambayo si ya kifahari na kueleza kuwa viongozi wa wilaya hawana budi kuanza kununuliwa magari ya thamani ya chini ya Sh100 milioni.
Waziri Mkuu aliwahi kutangaza kuwa serikali imeamua kutonunua tena magari hayo, lakini alitoa kauli hiyo wakati shehena nyingine ya magari ya kifahari ikiwa njiani kuja nchini.
Akizungumza na Mwananchi jana, mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu alisema: "Mimi nilivyosikia waziri mkuu kasema hivyo, nilicheka na kujiuliza maswali mengi sana.
Kauli hii inaonyesha udhaifu wa serikali na pia inaonyesha waziri mkuu haelewi majukumu yake. Yeye ana uwezo wa kumshauri rais na kupanga mambo ya msingi ya serikali.
"Kulalamikia magari ya kifahari serikalini ni kilikuwa kilio cha wananchi kwa serikali, sasa wananchi wanategemea majibu na siyo serikali kulalamika tena kwa wananchi. Kauli yake inaonyesha kuwa anawashitaki mawaziri na makatibu wakuu kwa wananchi."
Alisema serikali inapaswa kueleza aina ya magari ambayo inataka yatumike serikalini na siyo kuwalalamikia wananchi.
Profesa Baregu alisema bado wananchi wanahitaji majibu mengi ambayo serikali imekuwa ikiyakalia kimya kwa muda mrefu.
Alisema majibu ya masuala ya ubadhirifu wa fedha serikalini na mikataba tata bado wananchi wanahitaji majibu yake na si malalamiko.
Naye katibu mkuu wa NCCR Mageuzi, Samuel Ruhuza alisema kauli za Waziri Pinda zina lengo la kuwaridhisha Watanzania na hazina ukweli wowote.
Alisema pia kuwa lengo la kauli hizo lengo ni kujijengea mazingira mazuri ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
"Kusema kweli waziri mkuu katushangaza sana kwa kuwa kwa sasa anataka kuonyesha kuwa serikali inajali matatizo ya wananchi kwa kuwa itapunguza matumizi kwa kununua magari ya bei nafuu.
Tunajua kuwa yeye alikuwa mtu wa usalama na hivyo anajua kitu watu wanachotaka kusikia, hivyo anatumia fani yake hiyo kuwalaghai Watanzania," alisema.
Juzi akiwa mjini Dodoma, Waziri Pinda alisema kumekuwa na mashindano ya mawaziri kununua magari ya kifahari, badala ya kupunguza matumizi na kuwasaidia Watanzania masikini.
Waziri Pinda, ambaye alikuwa nje ya nchi kwa ziara ya kikazi, alionyesha kushangazwa na jinsi viongozi wa serikali ya India wanavyotumia magari ambayo si ya kifahari na kueleza kuwa viongozi wa wilaya hawana budi kuanza kununuliwa magari ya thamani ya chini ya Sh100 milioni.
Waziri Mkuu aliwahi kutangaza kuwa serikali imeamua kutonunua tena magari hayo, lakini alitoa kauli hiyo wakati shehena nyingine ya magari ya kifahari ikiwa njiani kuja nchini.
Akizungumza na Mwananchi jana, mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu alisema: "Mimi nilivyosikia waziri mkuu kasema hivyo, nilicheka na kujiuliza maswali mengi sana.
Kauli hii inaonyesha udhaifu wa serikali na pia inaonyesha waziri mkuu haelewi majukumu yake. Yeye ana uwezo wa kumshauri rais na kupanga mambo ya msingi ya serikali.
"Kulalamikia magari ya kifahari serikalini ni kilikuwa kilio cha wananchi kwa serikali, sasa wananchi wanategemea majibu na siyo serikali kulalamika tena kwa wananchi. Kauli yake inaonyesha kuwa anawashitaki mawaziri na makatibu wakuu kwa wananchi."
Alisema serikali inapaswa kueleza aina ya magari ambayo inataka yatumike serikalini na siyo kuwalalamikia wananchi.
Profesa Baregu alisema bado wananchi wanahitaji majibu mengi ambayo serikali imekuwa ikiyakalia kimya kwa muda mrefu.
Alisema majibu ya masuala ya ubadhirifu wa fedha serikalini na mikataba tata bado wananchi wanahitaji majibu yake na si malalamiko.
Naye katibu mkuu wa NCCR Mageuzi, Samuel Ruhuza alisema kauli za Waziri Pinda zina lengo la kuwaridhisha Watanzania na hazina ukweli wowote.
Alisema pia kuwa lengo la kauli hizo lengo ni kujijengea mazingira mazuri ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
"Kusema kweli waziri mkuu katushangaza sana kwa kuwa kwa sasa anataka kuonyesha kuwa serikali inajali matatizo ya wananchi kwa kuwa itapunguza matumizi kwa kununua magari ya bei nafuu.
Tunajua kuwa yeye alikuwa mtu wa usalama na hivyo anajua kitu watu wanachotaka kusikia, hivyo anatumia fani yake hiyo kuwalaghai Watanzania," alisema.