Waandishi wa kitabu cha Zaburi

Waandishi wa kitabu cha Zaburi

John Achila Mukumwa

Senior Member
Joined
Jan 4, 2024
Posts
112
Reaction score
217
Waandishi wa kitabu cha zaburi

Zaburi ni nini katika Biblia
Zaburi maana yake ni nyimbo takatifu. Hivyo kitabu cha Zaburi katika biblia, ni kitabu cha nyimbo takatifu. Zimeitwa nyimbo takatifu kwa sababu zimetungwa kwa lengo la kumrudisha mtu kwa muumba wake, kwa njia hiyo ya kusifu na kumwimbia. Pia, pamoja na kwamba zilikuwa ni nyimbo, lakini ndani yake pia zilikuwa zimejaa unabii wa mambo yanayokuja.

Katika agano la kale nyimbo hizo ziliimbwa na Wayahudi (Waisraeli) wakati wa kuabudu katika masinagogi yao. Hata leo, wakristo wanatumia baadhi ya mashairi hayo kutengeneza nyimbo nzuri za kumwimbia Mungu, kumshukuru na kumsifu.


Kitabu cha Zaburi katika biblia kwa sehemu kubwa (50%) kimeandikwa na Mfalme Daudi. Biblia inasema kuwa Daudi alianza kumwimbia Mungu tangu akiwa mdogo (1Samweli 16:16)

Kwa kifupi, kitabu cha Zaburi ni mkusanyiko wa maombi, mashairi na nyimbo ambazo zinalenga mawazo ya yule anayemuabudu Mungu, katika sifa na kuabudu. Sehemu za kitabu hiki zilitumika kama nyimbo katika ibada ya Israeli ya kale. Urithi wa kimuziki wa zaburi umeoneshwa na mada yake inatokana na neno la Kigiriki ambalo linamaanisha “wimbo unaoimbwa na vyombo vya kimuziki”.

Zaburi nyingi za kibinafsi zinahusisha sifa ya Mungu kwa ajili ya uwezo wake na wema wake, kwa ajili ya uumbaji wake wa ulimwengu, na kwa ajili ya matendo yake ya awali ya ukombozi kwa ajili ya Israeli. Wanawazia ulimwengu ambamo kila mtu na kila kitu kitamsifu Mungu, na Mungu naye atasikia maombi yao na kujibu.

Kitabu cha Zaburi kimegawanywa katika vitabu vitano.
Zaburi ya 1-2 ni za utangulizi
Zaburi imepangwa kama ifuatavyo:
Kitabu cha 1: 3-41
Kitabu cha 2: 42-72
Kitabu cha 3: 73-89
Kitabu cha 4: 90-106
Kitabu cha 5: 107-150

Tangu nyakati za kale, yasemekana kuwa kuhani Ezra ndiye aliyepanga kitabu cha Zaburi jinsi kilivyo leo.

Kitabu cha Zaburi kina jumla ya zaburi 150.
Kitabu hicho kimeandikwa na zaidi ya watu 7.

Waandishi wa kitabu cha Zaburi wameoneshwa hapo chini:
1. Mfalme Daudi: aliandika jumla ya zaburi 75 (50% ya zaburi zote 150)
Zaburi alizoandika Daudi ni zifuatazo:
2-9, 11-32, 34-41, 51-65, 68-70, 86, 95, 101, 103, 108-110, 122, 124, 131, 133, 138-145
2. Mfalme Sulemani: zaburi 2 (72 na127)
3. Nabii Musa: zaburi 1 (90)
4. Asafu: kiongozi wa sifa, muimbaji, muonaji, anayesimama mbele ya sanduku la Mungu daima kumsifu Mungu: zaburi 12 (50, 73-83)
5. Wana wa Kora: zaburi 11 (42, 44-49, 84-85, 87)
6. Hemani: mtu wa hekima: zaburi 1 (88)
7. Ethani: mtu wa hekima: zaburi 1 (89)
8. Wasiotambulika: jumla ya zaburi 48

Zaburi 48 ambazo waandishi wake hawajulikani ni kama ifuatavyo:
1, 10, 33, 43, 66-67, 71, 87, 91-94, 96-99, 100, 102, 104-107,
111-121, 123, 125-126, 128-130, 132, 134-137, 146-150

Utaona kuwa kuna zaburi 48 ambazo waandishi wake hawajulikani. Aidha, haijulikani wana wa Kora walioandika zaburi 11, walikuwa wangapi. Kama ingejulikana, kungekuwa na zaidi ya waandishi 7.

Ukiacha Sulemani na Musa, waandishi wengine wote walikuwa makuhani au Walawi ambao walihusika na kutoa muziki kwenye ibada madhabahuni wakati wa utawala wa Daudi.

Daudi aliyeandika zaburi 75 (50%) kati ya zaburi 150 ni nani

Daudi alikuwa ni Mfalme na mwanamuziki wa kipekee kwa kuwa alikuwa mwimbaji na pia mtungaji wa mashairi. Alipokuwa mvulana, alikuwa mchungaji na akili yake yenye utambuzi na ufahamu wa hali ya juu ilihifadhi habari nyingi kuhusu maeneo ya malisho ya Bethlehemu.
Alikuwa amefurahia kusikia sauti ya vibubujiko vya maji na sauti ya wana-kondoo wanapojibu anapowaita. Akivutiwa na umaridadi wa sauti hizo zilizomzunguka, alichukua filimbi na kinubi na kuanza kumsifu Mungu. Bila shaka ilipendeza kusikia muziki wa Daudi alipoimba Zaburi ya 23.

Kwa sababu ya utu wake mchangamfu, Daudi alipenda nyimbo zenye furaha zinazochangamsha na miziki yenye midundo yenye kupendeza.

Kwa ujumla, Daudi alikuwa msanii mwenye kipawa, kwa kuwa alikuwa mtengenezaji wa ala za muziki, mshairi, mtungaji, na mtumbuizaji. Daudi alifanya mambo makubwa hata zaidi.

Daudi hukumbukwa kwa kuwa yeye ndiye aliyepanga uimbaji na muziki katika nyumba ya Yehova. Alikuwa na waimbaji na wanamuziki 4,000, waliosimamiwa na Asafu, Hemani na Ethani.

Daudi aliwaweka chini ya wataalam mbalimbali 288 ambao waliwafunza na kuwaongoza. Wanamuziki na waimbaji hao 4,000 walikuwepo wakati wa sherehe tatu kubwa zilizofanywa kila mwaka. Hebu piga picha, kwaya hiyo kubwa yenye kuvutia (1Mambo ya Nyakati 23:5; 25:1, 6-7). Muziki wa Daudi ulioongozwa na roho takatifu, ulikuwa bora katika njia.

Jambo tunaloweza kujifunza ni kwamba Zaburi hizi zilizoandikwa na Daudi, zimewezwa kutukuzwa na Mungu mwenyewe mpaka leo, kwa sababu zimejaa maneno ya sifa kwa Mungu na ya kumtukuza sana.

Zaburi kwa ujumla
1. Zaburi ni aina ya sala iliyotungwa kama shairi au wimbo. Zaburi zinafundisha jinsi binadamu awezavyo kuzungumza na Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kitabu cha Zaburi kinatumiwa na Wakristo kama kitabu cha sala (maombi).
2. Masomo kwenye zaburi hasa, ni sifa za Mungu, shukrani, maombolezo, huzuni na toba, furaha na imani, elimu ya kidini, na ombi la ushindi dhidi ya maadui wasiomcha Mungu.
3. Zaburi imeandikwa na watu 7. Hata hivyo, kuna zaburi 48 ambazo waandishi wake
hawajulikani. Hivyo, kama wangejulikana, kungekuwa na zaidi ya waandishi 7.
 
Waandishi Tena si watu wanasema zabur ilishushwa!

Na Hapa ndio mimi siielewagi Quran.
Quran inasema Zaburi imeshushwa kama wahyi kwa Daudi.

😁😁😁😁 ila hoja yao ni ile ile.
vitabu vya allah vimechakachuliwa. (Allah ameshindwa kuilinda Zaburi )
Watasema Zaburi iliyoshushwa kwa Daud sio hii tuliyonayo sasa.

Na ukiwaambia wakuonyeshe Zabur halisi kutoka kwa allah. Hawana. 😎😎😎.

Shem Seran hivi unawaelewa
Hawa majamaa. Yaan kwao Kila kitu kimeshushwa.
Au msamiati wa "kushushwa" tunauelewa vibaya.
 
Na Hapa ndio mimi siielewagi Quran.
Quran inasema Zaburi imeshushwa kama wahyi kwa Daudi.

😁😁😁😁 ila hoja yao ni ile ile.
vitabu vya allah vimechakachuliwa. (Allah ameshindwa kuilinda Zaburi )
Watasema Zaburi iliyoshushwa kwa Daud sio hii tuliyonayo sasa.

Na ukiwaambia wakuonyeshe Zabur halisi kutoka kwa allah. Hawana. 😎😎😎.

Shem Seran hivi unawaelewa
Hawa majamaa. Yaan kwao Kila kitu kimeshushwa.
Au msamiati wa "kushushwa" tunauelewa vibaya.
Labda tunauelewa vibaya shem🙆🏽‍♀️ Binafsi sitaki vita na hawa viumbe mmhh🫢
 
Quran 4 : 163
"Hakika Sisi tumekuletea wahyi wewe kama tulivyo wapelekea wahyi Nuhu na Manabii walio kuwa baada yake. Na tulimpelekea wahyi Ibrahim na Ismail na Is-haka na Yaakub na wajukuu zake, na Isa na Ayub na Yunus na Harun na Suleiman, na Daudi tukampa Zaburi."

☝️☝️☝️☝️ wahyi huu wa Daudi ni sawa sawa na Wahyi wa Mtume Mohamed

Quran 4 : 162
"Lakini walio bobea katika ilimu miongoni mwao, na Waumini, wanayaamini uliyo teremshiwa wewe, na yaliyo teremshwa kabla yako. Na wanao shika Sala, na wakatoa Zaka, na wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho - hao tutawapa malipo makubwa."
 
2. Hoja ya pili ni "kushushwa".

Wanasema Quran ilishushwa yote kwa siku moja ,usiku wa Mwez wa Ramadhan kwenye mbingu ya kwanza. Alaf kwa miaka 23 mtume akawa anaipokea kidogo kidogo kama wahyi.

Ina maana Quran ilishushwa kama Kitabu kwenye mbingu ya kwanza.
Kwahiyo vitabu vyote Injili, zaburi na Tourat zilishushwa kwa namna hiyo alaf Jibril akawa anawashushia wahyi mitume wake kidogo kidogo.

Au mm ndio sielewi.
 
Na Hapa ndio mimi siielewagi Quran.
Quran inasema Zaburi imeshushwa kama wahyi kwa Daudi.

😁😁😁😁 ila hoja yao ni ile ile.
vitabu vya allah vimechakachuliwa. (Allah ameshindwa kuilinda Zaburi )
Watasema Zaburi iliyoshushwa kwa Daud sio hii tuliyonayo sasa.

Na ukiwaambia wakuonyeshe Zabur halisi kutoka kwa allah. Hawana. 😎😎😎.

Shem Seran hivi unawaelewa
Hawa majamaa. Yaan kwao Kila kitu kimeshushwa.
Au msamiati wa "kushushwa" tunauelewa vibaya.
Waulize pia asili na maana ya neno Zaburi

Mimi nikikutana na waislamu wanaojifanya wanajua

Huwa nawaleta kwenye small details tu

Muulize neno Zaburi kwenye Quran linatoka wapi asili yake ni nini ?

Maana yake hilo neno ni nini hawajui
 
Waulize pia asili na maana ya neno Zaburi

Mimi nikikutana na waislamu wanaojifanya wanajua

Huwa nawaleta kwenye small details tu

Muulize neno Zaburi kwenye Quran linatoka wapi asili yake ni nini ?

Maana yake hilo neno ni nini

Sawa bro.

Jagina Covax unahitajika tafadhali.
Tupe ilim kidogo kuhusu Zaburi based na hoja za bro hamis77 hapo juu
 
Kwa muislamu hawezi kamwe kujibu hivo ,ataleta propaganda nyingi

Maana akishasema ni Nyimbo za Sifa

Utambana kwanini dini ya Uislamu inapinga Nyimbo za Sifa msikitini?

Tayari Kuna Contradiction

Kwahiyo msikitini Hakunaga nyimbo za sifa na kuabudu?.

Zile kaswida ni nini?.
Maana kiarabu kitupu. Sielew hata moja.
 
Jagina Covax ukishatupa Ilimu kuhusu Zaburi.

1. Naomba unijibu je unasadiki kuwa Asafu, wana wa Kora, Suleiman pamoja na Daudi ndio walioandika Zaburi?.

2. Unaweza kutuletea Zaburi asilia ambayo allah alimshushia Daud ambayo haijachakachuliwa?.
Au ni hii hii tunayoisoma leo.
Dah umenikumbusha Wana wa Asafu ,walikuwa wanajua sana

Nabii na mwandishi wa Zaburi
Kiongozi wa waimbaji wa ibada (1 Mambo ya Nyakati 16:4–7)

Wana wa Asafu walikuwa kizazi cha waimbaji wa Hekalu,kama ukoo wa waimbaji wa kikuhani

Biblia bhana ,tamu sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom