Waandishi wa Habari wanavyosalitiana na kujidhalilisha

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Jul 1, 2008
10,564
7,973
Kufuatia kifo cha kinyama cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa channel ten mkoani Iringa hivi karibuni, waandishi wa habari kupitia Taasisi/vyama vyao kama Press Clubs, MCT na Jukwaa la wahariri walitoa matamko na misimamo mbalimbali.
Mojawapo ya mambo waliyofanya ni pamoja na Wanahabari wa Iringa kutangaza kususia kuandika/kutangaza habari za polisi kwa kipindi chote hadi siku arobaini za matanga ya marehemu Mwangosi.
Jambo la ajabu sana ni kwamba hata kabla ya siku kumi vyombo vya habari vimewasaliti wanahabari wenzao wa Iringa kwa kiasi cha kutisha. Vyombo vya habari vya Startv/RFA na ITV/Radio One vikaamua kupeleka waandishi wao Iringa wakaripoti kikamilifu habari za maadhimisho ya siku ya usalama barabarani kwakuwa wawakilishi wao walioko huko wasingeweza kufanya kinyume na msimamo wa IPC.
Kwa usaliti kama huu wanaofanyiana wanahabari wasitarajie kuheshimika ama kuaminika na jamii kama wao wenyewe hawajithamini na hawana umoja na mshikamano miongoni mwao. Walianza kusalitiana siku ya maandamano yao kwa kumwalika nchimbi pamoja na vituo vya Startv/RFA na ITV/Radio One kuongoza kwa kutangaza habari za kipolisi.
 
Mkuu Mwita Maranya, hili tumeshalizungumza sana humu jukwaani.
Kwenye tasnia ya habari, kuna kitu kinaitwa "pressures shapping the news", hizi sio habari bali determinant factors zinazofanya habari fulani iandikwe na habari fulani isiandikwe!.

Moja ya factor kubwa kuliko zote ni "money matters"!. Survival ya vyombo vingi vya habari sio circulation, readership, viewership au audience bali ni matangazo!. Watangazaji wakubwa wanaitwa sponsors!.

Hawa sponsors are the ones calling the shots!. "He who pays the piper, may call the tune". Wiki ya Usalama Barabarani ni "sponsored event" hivyo mdhamini lazima atokee na huko ndiko mshahara unakopatikana!.

Uandishi wa kuajiriwa ni kazi ya kitumwa, waandishi ni watumwa tuu, kazi yao ni kutumwa!. Mtumwa hana uhuru wala ridhaa jukumu lake ni kutekeleza tuu matakwa ya masters wake!.

Kumlaumu mtumwa ni kumuonea bure!. Mtumwa ni mtu wa kuhurumiwa!.
Pasco!.
 
Tatizo hapa si waandishi wa habari wala nani bali watanzania. Mara hii mmesahau juzi madaktari hata walimu na wafanyakazi wengine walivyofanya kitu kile kile? Tunahitaji kubadilika kama nchi na jamii vinginevyo hapa hakuna wa kumcheka mwenzie.Tusishangilie ni mapema.
 
upepo umeshapita hawajibiki mtu hapa, madaktari wenyewe wamelegea ndio ije waandishi?
 
Mkuu Pasco nimuelewa sana.
Lakini pamoja na hayo wameshindwa nini kuvumilia hizo siku arobaini tu? Hata kama ni mambo ya fedha lakini wamiliki wa vyombo vya habari (ambao nawa-treat kama wanahabari) walitakiwa kujifunga mkanda japo kwa muda huu mfupi ili kujiwekea heshima.
 
Last edited by a moderator:
Kufuatia kifo cha kinyama cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa channel ten mkoani Iringa hivi karibuni, waandishi wa habari kupitia Taasisi/vyama vyao kama Press Clubs, MCT na Jukwaa la wahariri walitoa matamko na misimamo mbalimbali.
Mojawapo ya mambo waliyofanya ni pamoja na Wanahabari wa Iringa kutangaza kususia kuandika/kutangaza habari za polisi kwa kipindi chote hadi siku arobaini za matanga ya marehemu Mwangosi.
Jambo la ajabu sana ni kwamba hata kabla ya siku kumi vyombo vya habari vimewasaliti wanahabari wenzao wa Iringa kwa kiasi cha kutisha. Vyombo vya habari vya Startv/RFA na ITV/Radio One vikaamua kupeleka waandishi wao Iringa wakaripoti kikamilifu habari za maadhimisho ya siku ya usalama barabarani kwakuwa wawakilishi wao walioko huko wasingeweza kufanya kinyume na msimamo wa IPC.
Kwa usaliti kama huu wanaofanyiana wanahabari wasitarajie kuheshimika ama kuaminika na jamii kama wao wenyewe hawajithamini na hawana umoja na mshikamano miongoni mwao. Walianza kusalitiana siku ya maandamano yao kwa kumwalika nchimbi pamoja na vituo vya Startv/RFA na ITV/Radio One kuongoza kwa kutangaza habari za kipolisi.

Wewe kukaa bila kupata habari unaona unajithamini kweli? Yaani watu wameumbuka ile mbaya. Mawazo ya watu wachache kama wewe mlio na sababu zenu binafsi hayawezi kuzuia watu zaidi mil.40 kupata habari.
 
Wewe kukaa bila kupata habari unaona unajithamini kweli? Yaani watu wameumbuka ile mbaya. Mawazo ya watu wachache kama wewe mlio na sababu zenu binafsi hayawezi kuzuia watu zaidi mil.40 kupata habari.
Wewe sio kitob---kweli? Kama vile nakufananisha,sorry lakini ni kutokana na michango yako hapa jukwaani imekaa ki Mata(m)komata(m)ko.hata hivyo nimeipenda. Sana jinsi ilivyo,inafaa sana kutiwa mfano na wengine humu jamvini.
 
Wewe kukaa bila kupata habari unaona unajithamini kweli? Yaani watu wameumbuka ile mbaya. Mawazo ya watu wachache kama wewe mlio na sababu zenu binafsi hayawezi kuzuia watu zaidi mil.40 kupata habari.

Mamaisara sidhani kama umeielewa hoja yangu. Nitajaribu kukutafunia sasa ukishindwa kumeza utakuwa unabahati mbaya.
Wanahabari wao wenyewe ndio walitoa msimamo wa kususia habari za polisi japo kwa siku arobaini za maombolezo ya Mwangosi lakini kabla hatujamaliza siku saba tayari wamejisahaulisha msimamo wao na kuanza kuwapamba polisi kadri wanavyojisikia.
 
Last edited by a moderator:
Mwita Maranya kusupport harakati za wafanyakazi wa tz kudai haki zao ni kutafuta aibu mbeleni

Mkuu Narubongo mimi hapa nafanya kuwakumbusha kwa mara nyingine msimamo waliokuwa wameuchukua ili siku nyingine wasikurupuke kutoa kauli na misimamo wanayojua kwamba hawawezi kutekeleza.
 
Last edited by a moderator:
nawasifu baadhi ya waandishi wa habari wa pale iringa kuendelea na msimamo wao hao uliowataja comrade wote wamepewa bahasha njaa ni ktu mbaya sana ndg yng wakwanza kuonesha njaa zao walikuwa na watangazaji wa kitua kimoja cha radio kiitwacho country fm hawa ndio wana njaa balaa
 
Mkuu Narubongo mimi hapa nafanya kuwakumbusha kwa mara nyingine msimamo waliokuwa wameuchukua ili siku nyingine wasikurupuke kutoa kauli na misimamo wanayojua kwamba hawawezi kutekeleza.

kabla mwangosi hajazikwa tayari waandishi hawa hawa walianza kucheza na maneno ili kuhalalisha sababu za polisi, sasa mwenye shida mwenyewe hayupo serious na hana nia ya kusaidiwa yanini kupoteza muda? kina mama bisimba wamesimama kulipeleka swala hili mahakama za kimataifa.. yaani sijui wanajisikiaje sasa hivi
 
Last edited by a moderator:
Waandishi wengi wa Tanzania ni "Makanjanja" wapo kimaslahi zaidi na kuandika udaku.
 
Mamaisara sidhani kama umeielewa hoja yangu. Nitajaribu kukutafunia sasa ukishindwa kumeza utakuwa unabahati mbaya.
Wanahabari wao wenyewe ndio walitoa msimamo wa kususia habari za polisi japo kwa siku arobaini za maombolezo ya Mwangosi lakini kabla hatujamaliza siku saba tayari wamejisahaulisha msimamo wao na kuanza kuwapamba polisi kadri wanavyojisikia.

Mkuu Maranya, hivi kweli unategemea kina Mamaisara wataelewa? I hope you did not mean it!!!!!!
 
Kufuatia kifo cha kinyama cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa channel ten mkoani Iringa hivi karibuni, waandishi wa habari kupitia Taasisi/vyama vyao kama Press Clubs, MCT na Jukwaa la wahariri walitoa matamko na misimamo mbalimbali.
Mojawapo ya mambo waliyofanya ni pamoja na Wanahabari wa Iringa kutangaza kususia kuandika/kutangaza habari za polisi kwa kipindi chote hadi siku arobaini za matanga ya marehemu Mwangosi.
Jambo la ajabu sana ni kwamba hata kabla ya siku kumi vyombo vya habari vimewasaliti wanahabari wenzao wa Iringa kwa kiasi cha kutisha. Vyombo vya habari vya Startv/RFA na ITV/Radio One vikaamua kupeleka waandishi wao Iringa wakaripoti kikamilifu habari za maadhimisho ya siku ya usalama barabarani kwakuwa wawakilishi wao walioko huko wasingeweza kufanya kinyume na msimamo wa IPC.
Kwa usaliti kama huu wanaofanyiana wanahabari wasitarajie kuheshimika ama kuaminika na jamii kama wao wenyewe hawajithamini na hawana umoja na mshikamano miongoni mwao. Walianza kusalitiana siku ya maandamano yao kwa kumwalika nchimbi pamoja na vituo vya Startv/RFA na ITV/Radio One kuongoza kwa kutangaza habari za kipolisi.

MARANYA hivi usaliti ni kwa wanahabari tuu?!! mbona wengi wanasalitiana tu,umesahau juzijuzi Madaktari?Haya mambo yapo kila mahali,utasikia huku walimu,huku polisi,huku wanafunzi vyuoni huko,yaani ni taabu tu kila kona ya nchi hii.

Mkuu Mwita Maranya, hili tumeshalizungumza sana humu jukwaani.
Kwenye tasnia ya habari, kuna kitu kinaitwa "pressures shapping the news", hizi sio habari bali determinant factors zinazofanya habari fulani iandikwe na habari fulani isiandikwe!.

Moja ya factor kubwa kuliko zote ni "money matters"!. Survival ya vyombo vingi vya habari sio circulation, readership, viewership au audience bali ni matangazo!. Watangazaji wakubwa wanaitwa sponsors!.

Hawa sponsors are the ones calling the shots!. "He who pays the piper, may call the tune". Wiki ya Usalama Barabarani ni "sponsored event" hivyo mdhamini lazima atokee na huko ndiko mshahara unakopatikana!.

Uandishi wa kuajiriwa ni kazi ya kitumwa, waandishi ni watumwa tuu, kazi yao ni kutumwa!. Mtumwa hana uhuru wala ridhaa jukumu lake ni kutekeleza tuu matakwa ya masters wake!.

Kumlaumu mtumwa ni kumuonea bure!. Mtumwa ni mtu wa kuhurumiwa!.
Pasco!.

Wewe chunga na angalai kauli zako,nani kakwambia kwamba kazi ya uandishi wa habari ni ya kitumwa?!,Thubutuuuuu,hi ni kazi kama ziilivyo nyingine,sema ni ukuda tu wa baadhi ya waandishi wa habari,kwa sababu nasiki hata huko Geita wanavutana na DC Mmoja anaitwa Manzie Omar Mangochie ambaye anawataka waandike ayatakayo na baada ya baadhi yao kukataa na kumtwanga stori amewaandikia barua za kuwattishi,lakini kazi hiyo imefanywa na baadhi ya waandishi wanadaiwa 'makuwadi' katika mkoa huo wa Geita.

Waandishi hao wanadaiwa kwamba wao kazi yao huwa ni kutafuta habari walizoandika wenzao kila siiku na kuwatafuta wahusika walioandikwa na kuwapelekea magazeti kwamba wameandikwa.

Sasa unadhani kwa staili kama hiyo wanaweza kuwa na umoja?!

Tatizo hapa si waandishi wa habari wala nani bali watanzania. Mara hii mmesahau juzi madaktari hata walimu na wafanyakazi wengine walivyofanya kitu kile kile? Tunahitaji kubadilika kama nchi na jamii vinginevyo hapa hakuna wa kumcheka mwenzie.Tusishangilie ni mapema.

Safi sana kaka kwanza suala la iringa ingelipendeza kama wananchi wa Mkoa huo wangeliandamana wote kupinga mauaji ya Mwangosi badala ya kuwaachia waandishi peke yao,ingelikuwa ni nchi za wenzetu wao ndio wangeliandamana kwa sababu mtu aliyekuwa akiwalisha habari ameuawa sasa ni nai atawalisha,lakini kama ulivyosema tatizo la watanzania wengi huwa hawaangalii mbele wanaangalia nini kipo kwa wakati huo.

Bahasha zetu zile,zileeee!

Acha Bangi zako kama umezoea kuchukua bahasha kwenye si wote.

nawasifu baadhi ya waandishi wa habari wa pale iringa kuendelea na msimamo wao hao uliowataja comrade wote wamepewa bahasha njaa ni ktu mbaya sana ndg yng wakwanza kuonesha njaa zao walikuwa na watangazaji wa kitua kimoja cha radio kiitwacho country fm hawa ndio wana njaa balaa

Kweli kaka lakini kama kweli kwa stahili hiyo ya vyombo vikubwa kama ITV na Star Tv kuamua kuwapeleka waandishi kwenye maeneo husika ambayo wanajua waandishi wengine wana msimamo unategemea nini?

Jibu hakuna kitu hapo,wacha tu nji hii tulishazoea kila siku ni mawengewenge tu.
 
WABHEJASANA,umenielewa kweli au umekurupuka tu??Kama unavuta bangi ni wewe mwenyewe,toa ujuha wako hapa
 
Last edited by a moderator:
Hiyo ni laana,kwa sababu hiyo wako radhi kuandika polisi hawahusiki na kifo cha Mwangosi ili mradi kipindi kiko sponsored?acheni bana,lazima ifike mahali tuwe na namna nzuri ya express feeling zetu na kuonyesha kutokuunga mkono unyama huu eti tu watu fulani wana-sponsor programu na kisha tunapata mishahara.huo ni upuuzi tena wa kijinga kabisa,na kwa huluka yetu watanzania tuna utamaduni wa kutoa onyo kwa njia mbali mbali ikiwa ni factor ya kupelekea mtu kujirekebisha na makosa yake,we Pasco si unajua hata kwetu usukumani inavyokuwa mtu akifanya makosa?na kama itakuwa kuendekeza njaa,mtakwisha waandishi ama sivyo msiripoti kinyume na matakwa ya magamba na serikali yake.
Hapa hakuna cha programu iko sponsored wala nini?huo ni usaliti wa wazi.shame on media zilizojipeleka Iringa kukava wiki ya usalama barabarani
 
Back
Top Bottom