Waalimu tunadharauliwa sana hivi kwanini?

kimonga1

Member
Jan 21, 2024
22
33
Tanzania Wilaya ya Uyui Waalimu tunanyasika sana sijui tatizo nini? Tulikuwa kwenye semina ya mtaala mpya daaa h full vitisho maneno ya kukatishana tammaaaa. Posho hazieleweki za semina yenyewe mnaishia kupewa maji makubwa.

Hii wilaya ina shida serikaki iangalie kwa jicho la pekeee ni wilaya ambayo mpaka sasa haijalipa nauli za likizo tangu mwezi wa 11.

Waziri itupie macho wilaya hii.
 
Nyie wenyewe hamjipend Sasa nani asiwadharau?
 
Uyui huko si ndio nyumbani kwa CCM?
 
Nikiona mada kama hizi hua namtumia sister 100k ya kula kuku angalau kuniepusha na aibu na fedheha na dharau kama hizo wanazopitia walimu.

Miaka ile natakiwa kwenda chuo kikuu, nikakosa mkopo kwa fani niliyokua naitaka, wakaniambia nibadili nisome ualimu nitapata mkopo 100%. Sister akakataa, siwezi kusoma fani siipendi kisa mkopo, akaahidi atalipia.

Leo hii nakula kuku kwa mrija, naishi kwenye ndege kama Vasco da gama wa mchongo. Isingekua sister ningeishia kua mwalimu huko Singida porini vumbi kama lote, kudharaulika hadi na bodaboda.
 
Duh huu uandishi utaacha kudharaulika kweli? Bila shaka hapo umekamatia Kishikwambi unabarizi 😃
 
Wakati nyie wanawapa maji wenyewe wamejiandikia posho za malaki na malaki CWT sio msaada kabisa maana hayo ndio mambo wanatakiwa kuwasimamia walimu
 
bado hujasema😅
 
Tatizo mnakataa kujitambua..

Samahanini, ila huo ndio ukweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…