Waafrika wote chali World Cup

Waafrika wote chali World Cup

Kitaja

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
2,836
Reaction score
1,383
Wawakilishi waliosalia katika world cup Algeria nao wameaga usiku huu kwa kufungwa 2-1 na Germany. Japo wamejitahidi ukizingatia wamefungwa katika dakika 30 za nyongeza. Hii inahitimisha kuondoshwa kwa timu zote tano za Afrika baada ya Nigeria nao kusalimu amri ya 2-0 kwa France. Waafrika tujipange safari bado ndefu sana world cup.
 
Mkiachiwa muendelee FIFA na Brasil hawatotengeneza pesa.
 
Mkiachiwa muendelee FIFA na Brasil hawatotengeneza pesa.
Hakuna njama yoyote tuliofanyiwa madhaifu yetu yalikuwa yanaonekana wazi. Ni algeria pekee walikuwa wanajua wanachokifanya . Majingajinga ya afrika magharibi sijui yalipelekwa na nani yanapiga pasi fupi fupi kuelekea golini kwao mishoni adui anachukua mpira
 
Acha tutoke wabaki wazungu wanaojua
 
Kwa timu nyingine za kiafrika niliumia sana zilipotoka ila kwa hawa Algeria nimefurahi saaana hadi najipongeza kwa kilaji saizi na sababu kuu ni kwamba timu za kiarabu wamekuwa wakiona soka la Afrika ni wao tu miaka yote na kuna mechi tuliwahi cheza na hawa Algeria huko kwao ila sikumbuki ilikua mashindano gani ambapo tulitoka sare ya 1-1 lakini kwa walioangalia hiyo mechi watakubaliana na mimi jinsi jamaa walivyobebwa sababu tulitangulia kupata Bao na walibebwa hadi wakafanikiwa kurudisha hivyo nina furaha isiyo kifani kwa timu hii kutupwa nje ya michuano hii. safi sana German
 
Kwa timu nyingine za kiafrika niliumia sana zilipotoka ila kwa hawa Algeria nimefurahi saaana hadi najipongeza kwa kilaji saizi na sababu kuu ni kwamba timu za kiarabu wamekuwa wakiona soka la Afrika ni wao tu miaka yote na kuna mechi tuliwahi cheza na hawa Algeria huko kwao ila sikumbuki ilikua mashindano gani ambapo tulitoka sare ya 1-1 lakini kwa walioangalia hiyo mechi watakubaliana na mimi jinsi jamaa walivyobebwa sababu tulitangulia kupata Bao na walibebwa hadi wakafanikiwa kurudisha hivyo nina furaha isiyo kifani kwa timu hii kutupwa nje ya michuano hii. safi sana German

Sio bure, usingizi unakusumbua
 
Hakuna njama yoyote tuliofanyiwa madhaifu yetu yalikuwa yanaonekana wazi. Ni algeria pekee walikuwa wanajua wanachokifanya . Majingajinga ya afrika magharibi sijui yalipelekwa na nani yanapiga pasi fupi fupi kuelekea golini kwao mishoni adui anachukua mpira
Usiiamini pia FIFA 100 % hebu niambie kwenye round hii ya mtoano kwanini mechi ya Brazil waliipanga ya pili kabla ya Netherland kama siyo kujua kwanza matokeo ya Nethland na chile halafu Brazili ndo ijipange ikiwa imemjua anayeenda kukutana naye.
 
Algeria ni pekee kutoka waliocheza mpira mzuri..hongera kwao kwa walipofikia.
 
Usiiamini pia FIFA 100 % hebu niambie kwenye round hii ya mtoano kwanini mechi ya Brazil waliipanga ya pili kabla ya Netherland kama siyo kujua kwanza matokeo ya Nethland na chile halafu Brazili ndo ijipange ikiwa imemjua anayeenda kukutana naye.

Hata baadhi ya timu za Afrika zilibebwa mfano Cameroon vs Mexico, vinginevyo tumeshuhudia hizi timu 'zetu' zikicheza ugolo
 
Hapo nimejua ni kwanini wazungu wanawarushia ndizi wachezaji wa kiafrika unapowaweka wenyewe ndio utajua na haya mashindano yamethihirisha waafirika tuna kauzubaifu fulani
 
Hakuna njama yoyote tuliofanyiwa madhaifu yetu yalikuwa yanaonekana wazi. Ni algeria pekee walikuwa wanajua wanachokifanya . Majingajinga ya afrika magharibi sijui yalipelekwa na nani yanapiga pasi fupi fupi kuelekea golini kwao mishoni adui anachukua mpira
Lakini hayohayo 'majingajinga' ndiyo yaliyowatoa 'wajanja' wa Afrika iliyosalia!
 
Usiiamini pia FIFA 100 % hebu niambie kwenye round hii ya mtoano kwanini mechi ya Brazil waliipanga ya pili kabla ya Netherland kama siyo kujua kwanza matokeo ya Nethland na chile halafu Brazili ndo ijipange ikiwa imemjua anayeenda kukutana naye.

kaka sijakuelewa. ratiba ilikuwa hivi:28/6/2014 brazil vs chile saa 1:00 usiku, colombia vs uruguay saa 5😱o usiku. 29/6/2014 netherland vs mexico saa 1😱o usiku, costa rica vs greece saa 5:00 usiku.
 
Mkiachiwa muendelee FIFA na Brasil hawatotengeneza pesa.

Wawakilishi waliosalia katika world cup Algeria nao wameaga usiku huu kwa kufungwa 2-1 na Germany. Japo wamejitahidi ukizingatia wamefungwa katika dakika 30 za nyongeza. Hii inahitimisha kuondoshwa kwa timu zote tano za Afrika baada ya Nigeria nao kusalimu amri ya 2-0 kwa France. Waafrika tujipange safari bado ndefu sana world cup.

Tatizo la Afrika ni posho kwanza mpira baadae..wenzetu ni mpira kwanza posho baadae.
 
Tatizo la Afrika ni posho kwanza mpira baadae..wenzetu ni mpira kwanza posho baadae.

Kwanza mngeana na kujiuliza timu yenu ya Tanzania iko wapi na imewahi kufanya nini na tatizo lake ni nini kabla hamjaanza kulalamikia Nigeria.

Bora ya wao world cup finals ni kama kwao, wakikosekana ni bahati mbaya. Sisi jee?
 
Kwanza mngeana na kujiuliza timu yenu ya Tanzania iko wapi na imewahi kufanya nini na tatizo lake ni nini kabla hamjaanza kulalamikia Nigeria.

Bora ya wao world cup finals ni kama kwao, wakikosekana ni bahati mbaya. Sisi jee?

Ukiangalia trend mechi nyingi (karibia zote ukiondoa Kameruni) timu za Afrika zimecheza vizuri sana kipindi cha kwanza na kuharibikiwa dakika za mwisho (Ghana vs USA/Germany),Ivory coast vs Greece,Nigeria vs France,Algeria vs Germany.The pattern of our failures is similar.Tatizo hapa sio uwezo wa wachezaji (vijana wetu wana uwezo mkubwa),tatizo ni kwenye conditioning na mental strength.Hii ni tatizo la bara letu kwa ujumla wetu,utatuzi wake lazima uanzie kwenye kutambua tatizo na kukubali tatizo hili sisi kama bara la Afrika tujue tunaanzia wapi kulitatua.Hakuna haja ya kuficha kichwa kama mbuni.
 
Ukiangalia trend mechi nyingi (karibia zote ukiondoa Kameruni) timu za Afrika zimecheza vizuri sana kipindi cha kwanza na kuharibikiwa dakika za mwisho (Ghana vs USA/Germany),Ivory coast vs Greece,Nigeria vs France,Algeria vs Germany.The pattern of our failures is similar.Tatizo hapa sio uwezo wa wachezaji (vijana wetu wana uwezo mkubwa),tatizo ni kwenye conditioning na mental strength.Hii ni tatizo la bara letu kwa ujumla wetu,utatuzi wake lazima uanzie kwenye kutambua tatizo na kukubali tatizo hili sisi kama bara la Afrika tujue tunaanzia wapi kulitatua.Hakuna haja ya kuficha kichwa kama mbuni.

Lazima tuwekeze kwenye soka la vijana. Kwa hali inavyoonyesha wachezaji wengi wa kiafrika wan miili yenye nguvu na kasi uwanjani lakini wanzidiwa maarifa. Mpira bila maarifa ni sawa na chai bila sukari. Maarifa ya uwanjani yatapatikana tu kwa kuwaandaa vijana wadogo na kuwajengea nidhamu ya mchezo.

Suala lingine waafrika waache kudanganya umri wao halisi. utakuta mchezaji ni 40+ lakini anajidai ndo kwanza yuko kwenye early 30s.Hii inasababisha kukata pumzi kadri mpira unavyoendelea na ndio maan timu karibu zote za afrika zimepoteza uthibiti karibia mpira unaisha.
 
Back
Top Bottom