Waafrika walioishangaza dunia

Waafrika walioishangaza dunia

Kwa nini hao wote wamekimbilia Marekani?..au je ni ule usemi wa kuwa Mwaflika bila Mzungu si chochote?... nami nilitegemea wabaki Africa kuliendeleza bara letu.. Labda kama walienda America kwa kuibwa..maana nasikia siku hizi mwafrika ukionekana tu una kipaji cha ajabu ajabu unabebwa na kwenda kufungiwa uwafanyie Assignment.
Kwa sababu ndiko kwenye facilities zote za kufanyia kazi infact watahitajika huko ndio kwenye viwanda vya kila aina.
 
mleta mada hapo uliposema "waliobadili fikra zao" naomba ufafanuzi...

kwani waafrika fikra zetu zipoje mpaka tuzibadilishe ndo tuweze kufanya mambo makubwa na yenye michango ktk jamii zetu na dunia? Naomba jibu
Kwa sababu waafrica tunawaza tumbo tu, hatuwazi jinsi ya ku solve problems kwa kutumia science. Wasomi wa Africa baada ya kupata elimu anawaza wapi atapata kazi yenye mshahara mkubwa tu, ni 0.1 percent tunao waza kuvumbua mambo
 
Kwa sababu hapa Africa hata uvumbue kitu gani hauwezi kuwa appreciated sana sana kama ni hapa Tanzania watakuuliza ww ni ccm au ukawa halafu wakupigwe zengwe. Si unaona Mbwana Sammata alivyowahishwa Lumumba kupiga picha na maccm. Africa ni shida
Umeona mkuu.

Ma innovative Tanzania hawana maana yaani hata ukijaribu na ukatolewa kwenye TV ili Watanzania wenye uwezo wakusaidie hawakusaidii.

Vyuo vikuu nao wanaufyata kimya, ni aibu kwa Tanzania kila mwaka tukashindwa kutoa japo 3 best innovative.

Niliwahi kusikia Tanzania alitokezea kijana kuunda silaha kama bunduki, mtu huyo kaishia jela sijui ni kweli?
 
Nimeipenda hii,ila katika woote nimemkubali sana huyo jamaa mnaigeria Dr. Philip Emeaguali,nimerudia mara nyingi sana kumsoma.
Nimetamani kumjua zaidi na zaidi.
 
Ndo maana unajaza na server yetu hapa. Unakopi maneno 2000 unacoment maneno 10!
sawa najaza server mkuu, tell me one thing(remarkable) you have done that your village will remember you even after 100 years.
Change your mind mkuu. Usiwe mwepesi kuhukumu, I am sure 100% hunipati kielimu wala kiuchumi labda umenizidi kwa porojo
 
Tanzania tungekuwa na mitaala ambayo mwanafunzi anasoma akipendacho tokea utotoni hakika tungepata WAVUMBUZI mbalimbali sio kama ilivyo sasa vijana wanasoma kukariri na kujibia mitiani tu na ukitaka kuona hilo nenda kwenye vyuo siku za mitiani kila mtu yuko bize akijisomea
 
sawa najaza server mkuu, tell me one thing(remarkable) you have done that your village will remember you even after 100 years.
Change your mind mkuu. Usiwe mwepesi kuhukumu, I am sure 100% hunipati kielimu wala kiuchumi labda umenizidi kwa porojo
Bosi,usidharau watu ukiwa nyuma ya keyboard! Rostam ndiye anaetuongoza watanzania kiuchumi kwa mujibu wa forbes. Wenye uchumi hawana swaga kams hizi! Tehe tehe
 
sawa najaza server mkuu, tell me one thing(remarkable) you have done that your village will remember you even after 100 years.
Change your mind mkuu. Usiwe mwepesi kuhukumu, I am sure 100% hunipati kielimu wala kiuchumi labda umenizidi kwa porojo
Elimu sikupati kwa kiingereza hiki!!
 
Hivi kwanini wanawake wanakuwa wachache kwenye mambo kama haya?mfano kama hiyo orodha hapo ya watu 11 kuna mwanamke mmoja tu.
 
Nimeipenda hii,ila katika woote nimemkubali sana huyo jamaa mnaigeria Dr. Philip Emeaguali,nimerudia mara nyingi sana kumsoma.
Nimetamani kumjua zaidi na zaidi.
Nimekupata nitaupdate madini yake huyu mtu na tujipe changamoto zaidi.
 
Jecha salum jecha huyu ni mzee aliweza kuipindua katiba iliotengenezwa na wengi na kutumia mamilon ya pesa kwa yy kuweza kufuta matokeo ya uchaguzi zanzibar wakati kisheria hana haki ya kufanya hvyo, hii ni historia na ni mvumbuzi wa kwanza duniani
Weka picha yake tumwone. Aluu huyu kawapita wote.
 
Pongezi kubwa nawapa waliofanikisha hayo yote, nami naja njiani na uvumbuzi wangu.
 
Vi
Pongezi kubwa nawapa waliofanikisha hayo yote, nami naja njiani na uvumbuzi wangu.
Vizuri mkuu kuna bado mengi hayajavumbuliwa. Ukishindwa kabisa andika kitabu kitakachobadili angalau maisha ya mtu mmoja.

Wanasema kile ambacho wewe unakidharau na kuhairisha kukifanyia kazi, wenzako wako bize wanakifanyia kazi.
 
Aliyegundua chips mayai mbona hayupo

Ovaa
 
Back
Top Bottom