Waafrika tumeanza kujitambua?

Waafrika tumeanza kujitambua?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,074
Reaction score
859,152
Siku ya leo pale Kenya... Nairobi ilikuwa inasubiriwa kwa hamu sana na vyombo vya habari vya nje.... Hata vichwa vya habari vilikuwa vimeshaandaliwa... Walitegemea machafuko makubwa wakati Odinga alipojiapiza kujiapisha kuwa rais wa watu wa Kenya... Mwezi mmoja kabla Marekani walikuwa tayari wameshamuonya asifanye hivyo kutokana na vurugu.. Vifo na machafuko ambayo yangetokea kama angefanya hivyo

Aibu yao hawa watabiri mabaya wa Africa.... Wachochezi na wachonganishi wakubwa... Raila mbele ya halaiki kubwa ya wakenya na vyombo vya habari akajiapisha... Uhuru Kenyata ambaye ndio rais rasmi (japo kuna mengi ndani yake) hakutaka kufanya kile wazungu walichokuwa wanaombea kifanyike...!!! Pamoja na kutoa onyo na kupeleka askari wengi wenye silaha... Hatimaye ama kwa uamuzi binafsi ama kwa kushauriwa dakika za mwisho akaamuru askari wa majeshi yote waondoke eneo la tukio.... Hii ilikuwa ni sawa na lle hamu ya kutofikishwa kileleni baada ya ashiki za muda mrefu

Kenya imeushangaza ulimwengu kwa kuvuka kikwazo hiki muhimu sana... Odinga kajiapisha kwa amani bila kubughudhiwa na mamlaka za nchi... Kenyata alikuwa ikulu akishuhudia kwenye luninga... Baada ya tukio hilo muhimu watu wakatawanyika kwa furaha na amani... Ma breaking news ikafa kifo cha mende... Ikaangukia pua.. Puuuu.. Mzee wa shithole najua kaumia sana

Somo la pili ni kile kilichotokea Zimbabwe mwezi mmoja na ushee uliopita... Yakafanyika mapinduzi ya amani kwa style ya aina yake... Mugabe akaondoshwa kwa kulazimishwa kimya kimya.. Sasa Zimbabwe inajipanga kusimama tena..... Dunia imeshuhudia hilo kwa mshangao wa aina yake... Lakini najua wale watoa misaada hawakupenda hili jambo liwe la amani kiasi kile... Wamekatishwa ashiki zao

Pamoja na yale yatakayoendelea kutokea Kenya... Tuyaombee sana... Lakini mbegu ya kujitambua imeshapandwa Afrika kupitia Zimbabwe na sasa imeanza kumea Kenya... Hii ni hatua moja kubwa sana na tunapaswa kuwapongeza wenzetu hawa.. Huku tukimuomba Joseph Kabila na wakongo wafuate nyayo hizi...
Pamoja na pongezi hizo lakini kuna mapungufu pia... Zimbabwe Mnangagwa anakwepa kuwajumuisha wapinzani kwenye serikali yale... Lakini anapaswa kuutambua mchango wao mpaka wakaweza kumdhoofisha babu kwa kiwango kikubwa kilichomsaidia sana yeye kupata KITI kwa ulaini kabisa...
Kwa ndugu yangu kaka mkubwa Uhuru mamlaka zake zilikosea sana kuvifungia vyombo vyote vilivyokuwa vinarusha matangazo ya moja kwa moja kwenye tukio la Odinga kujiapisha... Wangeacha dunia ishuhudie kwa mapana yake yasiyowezekana Africa na sehemu kubwa ya dunia yakiwezekana Nairobi Kenya....
Utambuzi huu umee na kuchanua hata Tanzania
 
Wakati si milele... Yasiyowezekanika... Huwezekana pia...
Mkuu (Mshana Jr) Serikali yetu inajaribu siku zote kuzuia tu, kile kilicho jitokeza ZANZIBAR miaka 20 iliyopita kisijirudie tena...!

Vinginevyo Marungu yanabaki tu kama mbadala...!

Ipo siku nitakukumbusha..
 
Mkuu mshana jr Kenya ni habari nyingine lakini sisi huu UdU umeturudisha nyuma miaka zaidi ya 50 KISA watu wanataka kung’ang’ania madarakani milele pamoja na kuwa wameshindwa vibaya sana katika kuiongoza nchi yetu.


Kenya imetuzindua kwenye usingizi mzito... Nasi tunaweza kuwa surprise ‼️ wao na dunia kwa ujumla kama tukiamua kutoa somo nadhifu sana la
-kufuta kesi zote za kutengeneza dhidi ya viongozi wa UPINZANI
-kuachana kabisa na biashara ya kununua viongozi wa UPINZANI kwa kisingizio cha kuunga mkono
- kutamka wazi na kwa dhati kabisa kuwa atayeacha ubunge wake ili aunge mkono juhudi na jitihada asitarajie kuwepo na uchaguzi wa marudio
-kuacha uonevu na kuweka mazingira sawa kwa vyama vyote vya UPINZANI
-Tuache maramoja mawazo mtindio ya kutawala (ilipaswa kuongoza) bila kufuata katiba sheria na Kanuni
 
Mkuu (Mshana Jr) Serikali yetu inajaribu siku zote kuzuia tu, kile kilicho jitokeza ZANZIBAR miaka 20 iliyopita kisijirudie tena...!

Vinginevyo Marungu yanabaki tu kama mbadala...!

Ipo siku nitakukumbusha..
Bado tuna nafasi ya kufanya tofauti.... Lakini kama tukiamua kujifunza toka kwa wengine
 
kwa kweli ni somo ,watu wengi walitarajia mabomu na nguvu za polisi kutawanya mkusanyiko ule ,imekuwa kinyume chake ila kuna kitu will happen ,kwa mujibu wa katiba yao
 
kwa kweli ni somo ,watu wengi walitarajia mabomu na nguvu za polisi kutawanya mkusanyiko ule ,imekuwa kinyume chake ila kuna kitu will happen ,kwa mujibu wa katiba yao
Ila naona kipengele kigumu wamekivuka.... Yake maneno ya.... Wape bunduki wauane yamezidi kukosa msisimko
 
Nampa hongera MH.Uhuru Kenyatta. Ndiye rais mvumilivu kuliko wote afrika mashariki. He is the most tolerant president in east africa. Tuna cha kujifunza kutoka kwake pamoja na ukweli kwamba, amezaliwa na kukulia ikulu. He has a lot of lessons to teach us.
 
Tatizo ni uchwara Mkuu. Huyu mtu ana chuki za kutisha kufikia hata kuanzisha mambo ya kuwateka, kuwatesa na kuwaua Watanzania. Sioni dalili ya huyu mtu kubadilika hata chembe. Mkewe aliona mbali kwamba hakustahili kuiongoza hii nchi kwa kuwa hana sifa hata moja. Sasa Nchi inayumba kwa maamuzi ya ajabu ajabu, chuki, vitisho na visasi yote haya yamezua hofu na taharuki kubwa sehemu nyingi nchini. Ikifikia mtu kudai kwamba anaunga mkono mfumo wa vyama vingi nchini wakati huo huo anafanya kila awezalo hata kukiuka katiba ya nchi kwa kuminya uhuru wa vyama hivyo, Viongozi wake pamoja na wanachama hata kukiuka sheria za nchi kwa kutumia rushwa ya pesa na vyeo kuwanunua wale wenye msimamo wa kuyumba basi ujue mtu huyo ana matatizo makubwa sana.

Kenya imetuzindua kwenye usingizi mzito... Nasi tunaweza kuwa surprise ‼️ wao na dunia kwa ujumla kama tukiamua kutoa somo nadhifu sana la
-kufuta kesi zote za kutengeneza dhidi ya viongozi wa UPINZANI
-kuachana kabisa na biashara ya kununua viongozi wa UPINZANI kwa kisingizio cha kuunga mkono
- kutamka wazi na kwa dhati kabisa kuwa atayeacha ubunge wake ili aunge mkono juhudi na jitihada asitarajie kuwepo na uchaguzi wa marudio
-kuacha uonevu na kuweka mazingira sawa kwa vyama vyote vya UPINZANI
-Tuache maramoja mawazo mtindio ya kutawala (ilipaswa kuongoza) bila kufuata katiba sheria na Kanuni
 
Nampa hongera MH.Uhuru Kenyatta. Ndiye rais mvumilivu kuliko wote afrika mashariki. He is the most tolerant president in east africa. Tuna cha kujifunza kutoka kwake pamoja na ukweli kwamba, amezaliwa na kukulia ikulu. He has a lot of lessons to teach us.
[emoji115] [emoji116] [emoji115] [emoji116] [emoji115] [emoji116] [emoji115] [emoji116] [emoji115] [emoji116][emoji115] [emoji116] [emoji115] [emoji116] [emoji102] [emoji102] [emoji102] [emoji102] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144]
Tatizo ni uchwara Mkuu. Huyu mtu ana chuki za kutisha kufikia hata kuanzisha mambo ya kuwateka, kuwatesa na kuwaua Watanzania. Sioni dalili ya huyu mtu kubadilika hata chembe. Mkewe aliona mbali kwamba hakustahili kuiongoza hii nchi kwa kuwa hana sifa hata moja. Sasa Nchi inayumba kwa maamuzi ya ajabu ajabu, chuki, vitisho na visasi yote haya yamezua hofu na taharuki kubwa sehemu nyingi nchini. Ikifikia mtu kudai kwamba anaunga mkono mfumo wa vyama vingi nchini wakati huo huo anafanya kila awezalo hata kukiuka katiba ya nchi kwa kuminya uhuru wa vyama hivyo, Viongozi wake pamoja na wanachama hata kukiuka sheria za nchi kwa kutumia rushwa ya pesa na vyeo kuwanunua wale wenye msimamo wa kuyumba basi ujue mtu huyo ana matatizo makubwa sana.
 
Ukitaka kupata utamu halisi wa sharubati ya tunda, likamue au liminye zaidi, hiki kipindi tulichonacho ni cha mpito tu, kinazidi kutukamua kujiandaa kwa hiyo mbegu kumea na kusambaa Afrika. Kila kitu kina mwanzo!!
 
Yaani wewe na utu uzima wako wote huo unaandika utumbo kias hiki..eti marekani ilitabiri na kwamba ilitaka machafuko.

Unaamini kwa dhati kabisa kwamba kama kweli marekani ilitaka machafuko yameshindikana??

Wakati mwingine muwe na aibu kuficha msivovijua..if Pentagon wanted a blood bath..leo sio tu vurugu ata uyo odinga mwenyew angevunjwa kalio.

Kasome 'hands off eyes on: American Interests Abroad'
mshana jr usijihangaishe na huyu zuzumagic hajui kitu zaidi ya kukebehi
 
Back
Top Bottom