Waafrika hadi sasa tunashindwa nini ku-document dini zetu kama waarabu, wahindu, wajapan, Wachina, wayahudi?

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Duniani kuna dini zaidi ya 99 na madhehebu ya dini mengi yasiyo na idadi. Wakristo wana madhehebu zaidi ya 43,000.

Takwimu zzinaonyesha angalau nusu 54% ya wakazi wa Dunia hii wanaamini kwenye miungu ya mashariki ya kati, yaani miungo ya waarabu na wayahudi, sehemu nyingine wanaamini miungo wao na idadi kubwa ya watu inaongezeka ya kutokuamini muungu wowote. Wachambuzi wanakadiria labda kufikia mwaka 2100 dini inaweza kua ina waamini wachache sana kuliko ilivyo sasa.

Hoja yangu ni kwamba,Afrika tumekua na miungu wetu ama ambao wamekua wakiabudiwa na vizazi vilivyotutangulia miaka na miaka na kwa bahati mbaya ujio wa hizi dini za mashariki ya kati na miungu wao kukawa na kampeni kubwa na mbaya dhidi ya miungu wetu na kudharau miungu wetu.

Ukiangalia uhalisia, hii miungu yote inafanana, hii ya kiafrika na hata ya mashariki ya kati, haina tofauti yoyote, hizi zaka, sadaka, sijui rituals gani zote zinafanana. Kazi yake ni kutoa faraja kwa maisha ya Duniani lakini haina msaada wowote zaidi ya hapo.

Kitu pekee kimesababisha dini hizi za mashariki ya kati kuchukua nafasi zaidi huku kwetu ni documentation, waarabu na wayahudi walijanjaruka mapema, wakaweka hizo ibada zao kwenye maandishi. Ukiangalia hizi dini hazikupata nafasi kubwa sana kwenye jamii ambayo tayari ilikua na documentation ya dini zao kama India, Japan, China na mashariki ya Asia yote.

Je waafrika tumeshindwa nini kuweka kwenye maandishi dini zetu za asili na kubaki kung'ang'ania hizi dini wa jamii nyingine. Good thing kuhusu dini zetu hazikua na chuki kama hizi dini za watu wa mashariki ya kati, hazitaki kulazimisha mtu aamini miungu wake na ukikataa uuwawe. Wataalam wa dini hebu wekeni dini zetu za kiafrika kwenye maandishi mrisishe vizazi.
 
Dini ni uumbaji wa mwanadamu. Mungu hana dini yoyote. Nilishaachana na dini za kimapokeo hizi. Dini hizi za kimapokeo Zinatatizo kuu moja, zinatengeneza ubaguzi na utengano wa binadamu. Dini yangu kwa sasa inaongozwa na imani kuu ya UTU. Ninafuata sayansi(kwani Mungu alipomuumba mwanadamu alimpa akili ya kupambana na mazingira yake). Sheria nafuata zile tulizojiwekea wanadamu na kutii kanuni za asili. Sintompa mwanangu hata mmoja jina la kiarabu wala kizungu kwani si utashi wa Mungu, bali ni ujinga wetu sisi waafrika kutotambua kuwa dini hizi za Uislam na Ukristo ni nyenzo ya cultural imperialism!
 
Acheni mabishano hakuna dini hata moja iliyo sahihi isipokuwa dini ya KIISILAMU. Na dini hii mwenyewe Allah (SWT) ndio kasema atailinda.
Nawe hapo wajiona mjanjaaaaa!!!

Anyways, kuna jamaa anaitwa prince Katega. Ana nondo nzito sana kuhusu dini. Ni kama Deception alivyo katika kuudadavua UKIMWI
 
Acheni mabishano hakuna dini hata moja iliyo sahihi isipokuwa dini ya KIISILAMU. Na dini hii mwenyewe Allah (SWT) ndio kasema atailinda.
Kwa kusema hvyo ikatosha kithibitisha kuwa ni kipimo cha din ya kwel?
 
Dini zetu si ndio huu Uchawi tulionao wenzetu wa Afrika ya Magharibi wamejitahidi kuendelea na Voodo yao

Sisi huku Afrika ya Mashariki inatubidi nasi tuhalalishe
Hata kwenye dini za mashariki ya kati kuna uchawi, ndio maana kuna majini na albadili kwenye dini ya waarabu.
 
Yani hata majina yetu hatuyataki tunajiita majina ya wageni halafu tunajiana wajaaaaaanja !!!!
Hapa ndio hua nasikitika sana.

Mtu anaitwa Mwita ama Maduhu anaona hayo ama Mushi majina hayana maana, ni majina ya kishenzi, ya mizimu, majina ya laana ila Christopher, Brown, Foxx, Adella, Angela, Joyness, Paulina, Fransisca na majina kama hayo ndio mazuri, ndio majina ya maana, ndio majina yaliyobarikiwa. Mambo ya kipumbavu kabisa.
 
Acheni mabishano hakuna dini hata moja iliyo sahihi isipokuwa dini ya KIISILAMU. Na dini hii mwenyewe Allah (SWT) ndio kasema atailinda.
Ameshashindwa kuilinda.

Angakua na uwezo wa kuilinda asingeamuru watu waue wengine ambao hawamkubali kwa kuwaahidi wanawake mabikra wazuri huko kusipokuwepo kunakoitwa akhera.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Back
Top Bottom