Serikali: Visa vya COVID-19 vyafikia 53. Vyuo na Shule kuendelea kufungwa hadi Serikali itakapotoa tamko jingine

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema agizo la kufungwa kwa shule za awali, msingi, sekondari na vyuo vya elimu ya kati na elimu ya juu litaendelea kubaki vile vile hadi Serikali itakaposema vinginevyo

Pia, amesema Rais Magufuli amesitisha maadhimisho ya Sherehe za Mapinduzi zilizokuwa zifanyike Aprili 26, pamoja na Sikukuu za Wafanyakazi za Mei Mosi ili kuepuka msongamano na kuzuia kusambaa kwa #COVID19

Aidha, Waziri Mkuu amesema hadi kufikia leo jumla ya Watu 53 wamebainika kuwa na virusi vya Corona ikiwa ni ongezeko la Wagonjwa wanne ambao wote wapo Jijini Dar

Amesisitiza kuwa Serikali bado haijatangaza kuhusu kufunguliwa kwa Shule, Vyuo na shunguli za michezo pamoja na misongamano isiyokuwa ya lazima hivyo maeneo hayo yataendelea kusalia katika Karantini na Wanafunzi wote waendelee kubaki nyumbani
1.jpg

2.jpg
 
Uwezekano wa kufunga shule J3 haupo, napendekeza mfuko wa kupambana na Covid19 uvisaidie vyuo na mashule viwezeshi vya kuandaa magunzo kwa njia ya mtandao.

Imekuwa kawaida walimu na wahazili huamka kwenda ofisini na kurudi nyumbani nothing to do, mbona wasijiongeze kuwawezesha wanafunzi wao kipondi hili cha lockdown ya corona.
 
Nashauri serikali isitangaaze visa hivi vya Corona wanatia hofu tu wananchi, Kwani huu ugonjwa upo dar Arusha na Zenji pekee?

Jibu ni No upo kila mahali hadi vijijini ndani ndani huko mikoani. Ila wanaishi kwa amani wanaugua na kupona bila kujua. Sasa wanavyozidi kutanganza wananchi wakijaa hofu Si miili itashindwa kupambana na magonjwa ya mwili.

Hakuna kitu kibaya kama hofu. Kinachoua ni hofu. No need to worry no matter how life is pretty miserable to us..The One who gives Life,He's Alive n Loyalty to Us.

Hili nalo litapita haijalishi litatuumiza vipi
 
Nashauri serikali isitangaaze visa hivi vya Corona wanatia hofu tu wananchi, Kwani huu ugonjwa upo dar Arusha na Zenji pekee..?
Jibu ni No upo kila mahali hadi vijijini ndani ndani huko mikoani. Ila wanaishi kwa amani wanaugua na kupona bila kujua...sasa wqnavyozidi kutanganza wananchi wakijaa hofu Si miili itashindwa kupambana na magonjwa ya mwili.
Hakuna kitu kibaya kama hofu..Kinachoua ni hofu
Ni vema kuwa na hofu maana tutachukua tahadhari!
 
Rais John Magufuli amesitisha maadhimisho ya Sherehe za Muungano (Aprili 26) pamoja na Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) ili kuepuka msongamano na kuendelea kuzuia virusi vya corona visisambae zaidi #MwananchiUpdates
 
Uwezekano wa kufunga shule J3 haupo, napendekeza mfuko wa kupambana na Covid19 uvisaidie vyuo na mashule viwezeshi vya kuandaa magunzo kwa njia ya mtandao. Imekuwa kawaida walimu na wahazili huamka kwenda ofisini na kurudi nyumbani nothing to do, mbona wasijiongeze kuwawezesha wanafunzi wao kipondi hili cha lockdown ya corona.
Vipi kuhusu shule za msingi za maporin ambazo hata chaki tu ni mtihani umeme wanafunzi hawajawah kuona
 
Isee!!!

Biashara sasa zimedorola na zingine kuelekea kukata kabisa Kwa sababu mtu hufanyi biashara Ila mwisho wa mwezi unatakiwa kurejesha madeni Bank, Mabenk ya kwetu yanaendelea kukomalia marejesho ya mikopo, Wakati nchi zilizokopa huko WB,IMF na sehemu zinginezo wanalia kusimamishiwa marejesho, au kufutiwa kabisa mikopo

Hili la kusimamishwa marejesho ya mikopo Kwa wafanyabiashara hapa kwetu mbona haliongelewi?
 
Back
Top Bottom