Vyombo vya habari duniani mwaka 3012

Free ideas

JF-Expert Member
Jun 11, 2013
3,456
1,937
Natabiri Taarifa za habari duniani mwaka 3000+ kuwa na vichwa vinavyosomeka ifuatavyo:
1. Rais wa bara la ulaya amefanya ziara ya kikazi barani Asia kukutana na Rais wa bara la Asia kwa mazungumzo ya kuimarisha uhusiano.

2. Nchi ya Africa mashariki inatarajia kufanya uchaguzi kumchagua balozi wake ambaye ni muwakilishi wa jumuia hiyo katika umoja wa mataifa katika awamu ya nne.

3. Kiongozi mkuu wa makanisa ya kikatoliki duniani bibi Hoshlewn Powel amese ni vyema kuimarisha umoja duniani kwa kuanzisha mchakato wa ushirikiano kati ya Wakatoliki na waumini wa zingine.

4. Balozi muwakilishi nchi ya amerika na canada katika umoja wa mataifa amesaini mkataba wa ushirikiano na balozi mwakilishi wa india na china ili kuweza kupeleka binadamu wengi zaidi katika sayari ya mars.

5. Idadi ya waafica wanaoishi katika sayari ya Mars yafikia 14.

6. NASA imetangaza ugunduzi mpya katika anga za mbali unaoonesha kuwepo viumbe tata katika sayari iliyopewa jina la Gyton .Viumbe vivyo ninamwonekano sawia na mwanadamu lakini vikiwa na mikia mirefu katika eneo la kitovuni

7. Shirikisho la mpira wa miguu ulimwenguni (UFA)- Universal Football Association, limetangaza kwa mara ya kwanza kombe la Ulimwengu kufanyika katika sayari Mars.

8. Shirika la haki za binadamu ulimwenguni limesema linaanda mpango wa kuwalinda wanadamu wote waliobadili jinsia na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi kama binadamu wengine.Shirika hilo limesema kati ya wanadamu bililoni 18 waliopo ulimwenguni bilioni 8 wamebadili jinsia.

9. Mamlaka ya kimataifa ya kuhifadhi viumbe kutoka sayari za mbali imesema inaelemewa na wingi wa viumbe vivyo ambavyo baadhi yao vimekua hatarishi kwa maisha ya binadamu.

10. Wamiliki wa maduka ya kuuza binadamu waliotengenezwa kwenye maabala wamesema mahitaji ya watoto bandia yamekua makubwa kuliko uzalishaji katika miaka ya hivi karibuni.

11. Rais wa bara la Africa amesema anataka usawa uwepo katika mgawanyo na matumizi ya viumbe kutoka sayari za mbali ili kukuza technolojia katika majimbo mengi katika nchi ya Africa. Amesema baadhi ya majimbo kama vile Tanzania, burundi na uganda hayana viumbe haonwa kutosha hivyo kuchelewesha utendaji na kukuza technolojia.

12. Kiongozi wa jimbo la Msumbiji apinduliwa baada ya kwenda likizo katika sayari ya mars kwa miezi mitatu.

13. Jeshi la nchi ya Asia limesema limeanza kutumia utaalam wa juu zaidi katika kukabiliana na majanga ya kibinadamu.

14. Binadamu yanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja wameziomba serikari zao kupiga matufuku ndoa za jinsia tofauti kwan zinawanyima haki ya kupata wenza wa maisha yao.

15. Kampuni ya Space X imetangaza kufanya utafiti ili kuanzisha makazi katika anga za mbali kukabiliana na changamoto za kimazingira katika sayari ya Dunia na Mars kutokana na wingi wa watu.

16. Kamapuni ya kutengeneza binadamu kwa njia ya maabala imesema idadi ya mahitaji ni kubwa kuliko uzalishaji na hii inatokana na binadamu wengi wanaozaliwa kutokua na uwezo wa kuzaa watoto kwa njia asilia (natural)

17. Umoja wa Falme za kiarabu umesema unafanya utafiti kuhusu yoote yaliyoandikwa katika Quran kuona kama yanauhalisia na ikiwezekana kubadili baadhi ya vitu ambavyo wanadhani vimepitwa na wakati.

18. Balozi wa jimbo la Ghana bwana Eboma komuni amefunga ndoa na bwana Buniku Sakara ambaye ni mfanya biashara kutoka jimbo la Chad.Wawili hao wameonekana wenye furaha na wameahidi kupata watoto 4 pamoja.

19. Shirika la afya ulimwenguni (UHO) - Universal Health Organization limesema idadi ya wanaume wanaokwenda kujifungua imekua kubwa kuliko wanawake na hivyo kuziomba taasisi za kidini kuhimiza watu kurudi katika maadili.

20. Kampuni ya kutengeneza magari ya UHOKU ya japani imepigwa faini ya PW( power) Bilioni 74 kwa kosa la kutengeneza na kuingiza sokoni magari yanayotumia mafuta aina ya petrol na diesel.

21. Kiongozi mkuu wa waislamu duniani amesema wanafanya mazungumzo na kiongozi mkuu wa makanisa ya kikatoliki ili kuungana kuwa na kiongozi mmoja atakayeongoza watu wote katika imani.

22. Wanasayansi ulimwenguni wameonya kuwepo kwa uwezekano wa uvamizi katika sayari ya Dunia kutoka kwa viumbe hatarishi kutoka sayari za mbali Hata hivyo viumbe hao bado hawajafahamika nia yao na hakuna mawasiliano ya moja kwa moja.

23. Shirika la afya Ulimwenguni (UHO) limesema kuna hatari ya kutokea upungufu wa maji katika sayari ya Mars kutokana na hali mbaya ya mazingitlra inayosababishwa na utunzaji mbaya wa vyanzo vya maji.

24. Jamii moja jimboni ufaransa imeanza kampeni ya kuhimiza wanadamu kuishi bila kuvaa nguo ili kuenzi kuenzi uumbaji wa mwenyezi mungu.Hata hivyo wamedai kua hata viumbe vingine kutoka sayari nyingine havina mavazi kama wanadamu.

25. Jimbo la america kwa kupitia wnasayansi wake limegundua chanjo maalum itakayoweza kurudisha umri nyuma kwa miaka 20. Chanjo hiyo imefanyiwa majaribio na kuonesha matokeo chanya. Wamesema chanjo hiyo itatolewa kwa watu wenye umri zaidi ya miaka 45.

26. Binadamu waliowekewa microchip katika ubongo wamelalamika kudukuliwa kila wakati na taasisi kubwa.Wamesema wanashindwa kuwa huru katika mambo yao hata ya faragha.
27. Watu saba katika jimbo la kenya huko Nchini Africa wameshindwa kupata huduma zozote za kijamii kwa kua wamegoma kuwekwa microchip katika miili yao ili kuweza kupata huduma kama binadamu wengine.

28. Kiumbe wa ajabu anayesadikiwa kutoka katika sayari mpya ya Bronta amekutwa amekufa katika mbuga ya serengeti jimboni Tanzania.

29. Umoja wa Nchi Ulimwenguni (UUNO) umepinga ajenda ya Jimbo la America ya kuanza kuwachoma sindano za sumu wanadamu wanaozaliwa wakiwa na ulemavu wa viungo. Umoja huo umedai ni kinyume na haki za binadamu.

30. Wakuu wa taasisi za kidini wamesema kuwa idadi ya waumini katika taasisi hizo imepungua kupindukia kutokana na uvumbuzi wa hivi karibuni unaoonesha upotoshwaji mkubwa katika maswala ya kiimani.

............…....Free Ideas.................
 
.
IMG_20210301_093020.jpg
 
Natabiri Taarifa za habari duniani mwaka 3000+ kuwa na vichwa vinavyosomeka ifuatavyo:
1. Rais wa bara la ulaya amefanya ziara ya kikazi barani Asia kukutana na Rais wa bara la Asia kwa mazungumzo ya kuimarisha uhusiano.

2. Nchi ya Africa mashariki inatarajia kufanya uchaguzi kumchagua balozi wake ambaye ni muwakilishi wa jumuia hiyo katika umoja wa mataifa katika awamu ya nne.

3. Kiongozi mkuu wa makanisa ya kikatoliki duniani bibi Hoshlewn Powel amese ni vyema kuimarisha umoja duniani kwa kuanzisha mchakato wa ushirikiano kati ya Wakatoliki na waumini wa zingine.

4. Balozi muwakilishi nchi ya amerika na canada katika umoja wa mataifa amesaini mkataba wa ushirikiano na balozi mwakilishi wa india na china ili kuweza kupeleka binadamu wengi zaidi katika sayari ya mars.

5. Idadi ya waafica wanaoishi katika sayari ya Mars yafikia 14.

6. NASA imetangaza ugunduzi mpya katika anga za mbali unaoonesha kuwepo viumbe tata katika sayari iliyopewa jina la Gyton .Viumbe vivyo ninamwonekano sawia na mwanadamu lakini vikiwa na mikia mirefu katika eneo la kitovuni

7. Shirikisho la mpira wa miguu ulimwenguni (UFA)- Universal Football Association, limetangaza kwa mara ya kwanza kombe la Ulimwengu kufanyika katika sayari Mars.

8. Shirika la haki za binadamu ulimwenguni limesema linaanda mpango wa kuwalinda wanadamu wote waliobadili jinsia na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi kama binadamu wengine.Shirika hilo limesema kati ya wanadamu bililoni 18 waliopo ulimwenguni bilioni 8 wamebadili jinsia.

9. Mamlaka ya kimataifa ya kuhifadhi viumbe kutoka sayari za mbali imesema inaelemewa na wingi wa viumbe vivyo ambavyo baadhi yao vimekua hatarishi kwa maisha ya binadamu.

10. Wamiliki wa maduka ya kuuza binadamu waliotengenezwa kwenye maabala wamesema mahitaji ya watoto bandia yamekua makubwa kuliko uzalishaji katika miaka ya hivi karibuni.

11. Rais wa bara la Africa amesema anataka usawa uwepo katika mgawanyo na matumizi ya viumbe kutoka sayari za mbali ili kukuza technolojia katika majimbo mengi katika nchi ya Africa. Amesema baadhi ya majimbo kama vile Tanzania, burundi na uganda hayana viumbe haonwa kutosha hivyo kuchelewesha utendaji na kukuza technolojia.

12. Kiongozi wa jimbo la Msumbiji apinduliwa baada ya kwenda likizo katika sayari ya mars kwa miezi mitatu.

13. Jeshi la nchi ya Asia limesema limeanza kutumia utaalam wa juu zaidi katika kukabiliana na majanga ya kibinadamu.

14. Binadamu yanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja wameziomba serikari zao kupiga matufuku ndoa za jinsia tofauti kwan zinawanyima haki ya kupata wenza wa maisha yao.

15. Kampuni ya Space X imetangaza kufanya utafiti ili kuanzisha makazi katika anga za mbali kukabiliana na changamoto za kimazingira katika sayari ya Dunia na Mars kutokana na wingi wa watu.

16. Kamapuni ya kutengeneza binadamu kwa njia ya maabala imesema idadi ya mahitaji ni kubwa kuliko uzalishaji na hii inatokana na binadamu wengi wanaozaliwa kutokua na uwezo wa kuzaa watoto kwa njia asilia (natural)

17. Umoja wa Falme za kiarabu umesema unafanya utafiti kuhusu yoote yaliyoandikwa katika Quran kuona kama yanauhalisia na ikiwezekana kubadili baadhi ya vitu ambavyo wanadhani vimepitwa na wakati.

18. Balozi wa jimbo la Ghana bwana Eboma komuni amefunga ndoa na bwana Buniku Sakara ambaye ni mfanya biashara kutoka jimbo la Chad.Wawili hao wameonekana wenye furaha na wameahidi kupata watoto 4 pamoja.

19. Shirika la afya ulimwenguni (UHO) - Universal Health Organization limesema idadi ya wanaume wanaokwenda kujifungua imekua kubwa kuliko wanawake na hivyo kuziomba taasisi za kidini kuhimiza watu kurudi katika maadili.

20. Kampuni ya kutengeneza magari ya UHOKU ya japani imepigwa faini ya PW( power) Bilioni 74 kwa kosa la kutengeneza na kuingiza sokoni magari yanayotumia mafuta aina ya petrol na diesel.

21. Kiongozi mkuu wa waislamu duniani amesema wanafanya mazungumzo na kiongozi mkuu wa makanisa ya kikatoliki ili kuungana kuwa na kiongozi mmoja atakayeongoza watu wote katika imani.

22. Wanasayansi ulimwenguni wameonya kuwepo kwa uwezekano wa uvamizi katika sayari ya Dunia kutoka kwa viumbe hatarishi kutoka sayari za mbali Hata hivyo viumbe hao bado hawajafahamika nia yao na hakuna mawasiliano ya moja kwa moja.

23. Shirika la afya Ulimwenguni (UHO) limesema kuna hatari ya kutokea upungufu wa maji katika sayari ya Mars kutokana na hali mbaya ya mazingitlra inayosababishwa na utunzaji mbaya wa vyanzo vya maji.

24. Jamii moja jimboni ufaransa imeanza kampeni ya kuhimiza wanadamu kuishi bila kuvaa nguo ili kuenzi kuenzi uumbaji wa mwenyezi mungu.Hata hivyo wamedai kua hata viumbe vingine kutoka sayari nyingine havina mavazi kama wanadamu.

25. Jimbo la america kwa kupitia wnasayansi wake limegundua chanjo maalum itakayoweza kurudisha umri nyuma kwa miaka 20. Chanjo hiyo imefanyiwa majaribio na kuonesha matokeo chanya. Wamesema chanjo hiyo itatolewa kwa watu wenye umri zaidi ya miaka 45.

26. Binadamu waliowekewa microchip katika ubongo wamelalamika kudukuliwa kila wakati na taasisi kubwa.Wamesema wanashindwa kuwa huru katika mambo yao hata ya faragha.
27. Watu saba katika jimbo la kenya huko Nchini Africa wameshindwa kupata huduma zozote za kijamii kwa kua wamegoma kuwekwa microchip katika miili yao ili kuweza kupata huduma kama binadamu wengine.

28. Kiumbe wa ajabu anayesadikiwa kutoka katika sayari mpya ya Bronta amekutwa amekufa katika mbuga ya serengeti jimboni Tanzania.

29. Umoja wa Nchi Ulimwenguni (UUNO) umepinga ajenda ya Jimbo la America ya kuanza kuwachoma sindano za sumu wanadamu wanaozaliwa wakiwa na ulemavu wa viungo. Umoja huo umedai ni kinyume na haki za binadamu.

30. Wakuu wa taasisi za kidini wamesema kuwa idadi ya waumini katika taasisi hizo imepungua kupindukia kutokana na uvumbuzi wa hivi karibuni unaoonesha upotoshwaji mkubwa katika maswala ya kiimani.

............…....Free Ideas.................
Jiwe atakuwa amepuputika kabisa wakati huo
 
Mkuu mwaka 3000 mbona mbali sana, hapo 2300 sidhani kama kuna member wa Jf atakae kuwa hai kwa wakati huo.
Ila natamani niwepo duniani hadi miaka hiyo nishuhudie mabadiliko chanya ya teknolojia hasa katika afya, uchukuzi, mawasiliano, utafika katika anga za mbali, kilimo na ufugaji.
 
Back
Top Bottom