Nteko Vano
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 434
- 111
Vyama vya upinzani vinaweza kufanya shughuli za maendeleo katika majimbo ambayo wanayashikilia bila kutegemea fedha toka serikalini. Tunaweza kupata maji ya uhakika, umeme, miradi midogo midogo katika vikundi kwa eneo husika, na kutatua kero mbalimbali zinazotupa changamoto.
Nimejaribu kufikiria kama wananchi wameitikia kwa nguvu zote bila kinyongo kuchangia kampeni za CDM, Arumeru kumbe tunaweza kutumia mbinu hiyo na nyingine zifananazo na hiyo kufanikisha kutatua matatizo yanayotukabili. Ninajua kuna wataalam wanaweza kushauri jinsi ya kuendeleza utaratibu huo hata kama suala moja litachukua miaka mitano lakini kama litaisha itakuwa ni hatua na njia safi.
Vyama vya upinzani vitafaidika na mpango huu kwa kuzuia CCM kwa njia moja au nyingine kutumia mbinu ya kudhoofisha maendeleo ya majimbo ambayo upinzani wanayo ili iwe tiketi ya kuombea kura mwaka 2015. Nina imani kuwa mpango huu utakuwa endelevu kwa vyama vyetu vya upinzani.
Wana JF, naleta kwenu ili tujadili naomba kila mtu mwenye wazo lake kuhusiana na hili atoe mchango wake. Litakuwa na athari gani na tunaweza kuepuka vipi athari hasi na je, ni mikakati ipi inaweza kuwekwa ili kutimiza hili kama linawezekana.
Nawasilisha
Nimejaribu kufikiria kama wananchi wameitikia kwa nguvu zote bila kinyongo kuchangia kampeni za CDM, Arumeru kumbe tunaweza kutumia mbinu hiyo na nyingine zifananazo na hiyo kufanikisha kutatua matatizo yanayotukabili. Ninajua kuna wataalam wanaweza kushauri jinsi ya kuendeleza utaratibu huo hata kama suala moja litachukua miaka mitano lakini kama litaisha itakuwa ni hatua na njia safi.
Vyama vya upinzani vitafaidika na mpango huu kwa kuzuia CCM kwa njia moja au nyingine kutumia mbinu ya kudhoofisha maendeleo ya majimbo ambayo upinzani wanayo ili iwe tiketi ya kuombea kura mwaka 2015. Nina imani kuwa mpango huu utakuwa endelevu kwa vyama vyetu vya upinzani.
Wana JF, naleta kwenu ili tujadili naomba kila mtu mwenye wazo lake kuhusiana na hili atoe mchango wake. Litakuwa na athari gani na tunaweza kuepuka vipi athari hasi na je, ni mikakati ipi inaweza kuwekwa ili kutimiza hili kama linawezekana.
Nawasilisha