Vyakula na ubonge maharage, bia, karanga, ugali

Vyakula na ubonge maharage, bia, karanga, ugali

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
11,674
Reaction score
20,689
Kuna tatizo la ubonge linainyemelea nchi. Hasa kwa watu wa kipato cha kati. Kiufupi ubonge unatokea pale ambapo unakula chakula chenye nguvu nyingi kuliko unazohitaji. Matokeo yake chakula hicho kinaenda kuhifadhiwa kama mafuta mwilini na kuleta ubonge.

Hivyo basi ili kuepuka ubonge tunahitaji kufahamu mahitaji ya nguvu mwilini na nguvu zilizomo katika vyakula tunavyokula. Kwa kawaida mahitaji ya nguvu katika mwili yanategemea mambo mengi. Kama jinsi yake, mwili wake, kazi yake, mazoezi etc. Lakini kwa wastani ni kati ya 2,000 kilocalories hadi 3,000 kilocalories. Mwanaume wa kawaida asiye active physically anahitaji kama Kcal 2,200 hivi kwa siku.

Sasa katika vyakula tunavyokula Tanzania mara nyingi, hakuna chenye nguvu nyingi kama mboga maharage. Kilo moja ya maharage ina Kcal 3,470!! Kwa siku ukila gram 200 tu za maharage tayari unakuwa umeingiza kama Kcal 700 hivi.
Maharage yana nguvu kuliko nyama ya ng'ombe. Kilo ya nyama ya ng'ombe inahesabika kuwa na Kcal 2500.

Chakula kingine tunachokula sana ni ugali. Unga wa mahindi ni moja ya vyakula vyenye nguvu hasa. Kilo moja ya unga wa mahindi una Kcal 3800. Kama ukila ugali mchana na usiku kwa kusonga jumla nusu kilo basi unakuwa umetumbukiza mwilini Kcal 1400.

Mchele, kilo moja ya mchele ina Kcal kama 1300. Unga wa mahindi una kama mara tatu yake. Pengine ndiyo maana Waasia wala wali hawanaga ubonge.

Kilo moja ya ngano ina kama Kcal 3400.

Bia. Walevi huwaga si walaji wazuri, sababu moja wapo ni kuwa bia nazo zinashibisha sana, kwa maana zina nguvu nyingi. Lita moja ya bia ina kama Kcal 450. Tena zile za kienyeji zinaweza kuwa hata mara mbili yake. Ukipiga yale mabia makubwa ya nusu lita manne ujue umeingiza Kcal kama 1,000 hivi. Wine zina kama 625 kwa chupa. Rum kama konyagi ukipiga nusu lita basi unakuwa umeingiza kama Kcal 800.

Soda zinacheza kwenye Kcal 400 hivi kwa litre.
Viazi vya kuchemsha ni kama 900kcal kwa kilo. Na mihogo ni kama 1600Kcal kwa kilo.

Vitu vyenye mafuta ndivyo vyakula vyenye nguvu kuliko vyote. Kilo moja ya karanga ina Kcal 5700. Zaidi ya mara mbili ya mahitaji ya mtu wa kawaida. Ukipiga packet mbili za karanga za 100g kila moja ujue umeingiza 1000Kcal. Unashangaa mbona sili sana!! Asubuhi napiga tu chai na karanga lakini nanenepa? Kumbe umeingiza Kcal za kutosha. Kuna zile karanga miti zinaitwa Macadamia nuts, zile kilo moja ina Kcal 7200!!! Pia kuna nazi. Lita ya tui la nazi ina Kcal 2300. Unakuta wamaza wa pwani vibonge vibonge kumbe matui ya nazi.

Litre moja ya maziwa ina Kcal 650.

Samaki hazina calories nyingi, ila siyo ndiyo tuzile kilafi.

Ubonge una madhara mengi sana kama Presha, kisukari ambacho huleta shida ya figo, macho na kifo cha mapema. Tunavyokula tuangalie sana kiasi cha mahitaji yetu ya calories kwa siku na calories zilizopo kwenye vyakula tunavyokula.

Wafilipi 3:19
19 Mwisho wa watu hao ni kuangamia, na Mungu wao ni tumbo; kwa sababu wao huyaonea fahari mambo ya aibu na mawazo yao yametawaliwa na mambo ya dunia.
 
Kuna tatizo la ubonge linainyemelea nchi. Hasa kwa watu wa kipato cha kati. Kiufupi ubonge unatokea pale ambapo unakula chakula chenye nguvu nyingi kuliko unazohitaji. Matokeo yake chakula hicho kinaenda kuhifadhiwa kama mafuta mwilini na kuleta ubonge.

Hivyo basi ili kuepuka ubonge tunahitaji kufahamu mahitaji ya nguvu mwilini na nguvu zilizomo katika vyakula tunavyokula. Kwa kawaida mahitaji ya nguvu katika mwili yanategemea mambo mengi. Kama jinsi yake, mwili wake, kazi yake, mazoezi etc. Lakini kwa wastani ni kati ya 2,000 kilocalories hadi 3,000 kilocalories. Mwanaume wa kawaida asiye active physically anahitaji kama Kcal 2,200 hivi kwa siku.

Sasa katika vyakula tunavyokula Tanzania mara nyingi hakuna chenye nguvu nyingi kama mboga maharage. Kilo moja ya maharage. Kilo moja ya maharage ina Kcal 3,470!! Kwa siku ukila gram 200 tu za maharage tayari unakuwa umeingiza kama Kcal 700 hivi.

Chakula kingine tunachokula sana ni ugali. Unga wa mahindi ni moja ya vyakula vyenye nguvu hasa. Kilo moja ya unga wa mahindi una Kcal 3800. Kama ukila ugali mchana na usiku kwa kusonga jumla nusu kilo basi unakuwa umetumbukiza mwilini Kcal 1400. Maharage yana nguvu kuliko nyama ya ng'ombe. Kilo ya nyama ya ng'ombe inahesabika kuwa na Kcal 2500.

Mchele, kilo moja ya mchele ina Kcal kama 1300. Unga wa ubga wa mahindi una kama mara tatu yake. Pengine ndiyo maana Waasia wala wali hawanaga ubonge.

Kilo moja ya ngano ina kama Kcal 3400.

Bia. Walevi huwaga si walaji wazuri, sababu moja wapo ni kuwa bia nazo zinashibisha sana, kwa maana zina nguvu nyingi. Lita moja ya bia ina kama Kcal 450. Tena zile za kienyeji zinaweza kuwa hata mara mbili yake. Ukipiga yale mabia makubwa ya nusu lita manne ujue umeingiza Kcal kama 1,000 hivi. Wine zina kama 625 kwa chupa. Rum kama konyagi ukipiga nusu lita basi unakuwa umeingiza kama Kcal 800.

Soda zinacheza kwenye Kcal 400 hivi kwa litre.
Viazi vya kuchemsha ni kama 900kcal kwa kilo. Na mihogo ni kama 1600Kcal kwa kilo.

Vitu vyenye mafuta ndivyo vyakula vyenye nguvu kuliko vyote. Kilo moja ya karanga ina Kcal 5700. Zaidi ya mara mbili ya mahitaji ya mtu wa kawaida. Ukipiga packet mbili za karanga za 100g kila moja ujue umeingiza 1000Kcal. Unashangaa mbona siana!! Napiga tu chai na karanga lakini nanenepa? Kumbe umeingiza Kcal za kutosha. Kuna zile karanga miti zinaitwa Macadamia nuts, zile kilo moja ina Kcal 7200!!! Pia kuna nazi. Lita ya tui la nazi ina Kcal 2300. Unakuta wamaza wa pwani vibonge vibonge kumbe matui ya nazi.

Litre moja ya maziwa ina Kcal 650.

Samaki hazina calories nyingi, ila siyo ndiyo tuzile kilafi.

Ubonge una madhara mengi sana kama Presha, kisukari ambacho huleta shida ya figo, macho na kifo cha mapema. Tunavyokula tuangalie sana kiasi cha mahitaji yetu ya calories kwa siku na calories zilizopo kwenye vyakula tunavyokula.

Wafilipi 3:19
19 Mwisho wa watu hao ni kuangamia, na Mungu wao ni tumbo; kwa sababu wao huyaonea fahari mambo ya aibu na mawazo yao yametawaliwa na mambo ya dunia.
Hivi vyakula vyote vinaliwa na watanzania lakini bado hawanenepi wamekondeana tofauti na miili ya watu kutoka west Afrika
 
Kwakweli ukiwa unafukia vyakula wewe unajiona sawa ila ni hatari sana ndugu zangu.
Tunaendekeza kula hovyo, dr janabi yuko sahihi.

Mleta mada asante kutukumbusha nisisitize tena tunywe maji ya kutosha, na tuache kula vyakula vigumu usiku.

Nimebadirika sana kiasi kwamba nikitembea kwa watu najikuta vyakula walivyo vipika siwezi kuvila.
Kwanza situmii , sukari, soda, juice za kununua, sili vyakula vyote vya kuunga nachemsha tu.

Mafuta kidogo nakutana nayo kwenye wali, nchicha na mayai pale ninapo yakaanga.( mchana tu)

Ratiba yangu inaanza saa 11:30 za asubuhi nakunywa ile chupa mkubwa ya maji yote. Yaani usiku wakati naenda kulala naenda nayo chumbani. (Sichemshi maji nanunua katon)
Hiyo chupa yote naipiga ingawa dr wangu wa ngozi aliniambia niwe nakunywa lita moja muda huo kabla ya mswaki..

Maji hayo hayatakiwi kuwa ya baridi yawe tu yakawaida usiyaweke kwenye friji. Nikimaliza kuyanywa huwa najisikia vibaya kwahiyo naendelea kulala kama lisaa nakaa sawa.

12:30 naamka nafanya shughuri
zangu kujianda kwenda kazini muda huo naanda breakfast ambayo sio chai nachemsha mhogo au gimbi nitakula na kipande kimoja cha labda kuku mchemsho au nakausha kweny Airflier nakula bila chai.

Saa 4: 00 nusu lita ya maji.

Chakula cha mchana tuseme saa 8 au 9 mchana hapa ndo changamojo aisee mazingira yetu ya kazi huwezi kukwepa wali, so nitakula wali kidogo na mlenda au na mboga za majani tu. Baada ya kula dk 40 zikipita nakunywa tena nusu lita ya maji.

Kuanzia saa 11 jion hadi saa 2 usiku huo muda nakuwa bado ofisin nakuwa nakunywa maji kidogo kidogo hadi saa 2 kamili usiku naenda home.

Nikifika home nafanya mazoezi kidogo kama nusu saa naoga nakula matunda tu, yaani tango mbili au papai moja au tikiti au nikisikia tumbo linalalamika kutoshiba nakula ka kipande ka kuku au ka samaki nalala. Mpaka kesho saa 11 na nusu.

Ratiba hii ni nzuri sana ukinywa maji asubuhi mapema lazima kila asubuhi uende choo.
Magonjwa kama UTI sikumbuki mwisho nimepata lini.
Ngozi yangu imekaa vizuri mno nina ule weusi chocolate flani niliyo kuwa naitamani (ni pamoja na kutumia lotion original za SH AMON'S.
Wakuu maji ni uhai.
Nb. Ukijisikia kuumwa usikimbilie kumeza dawa kwanza kunywa hata chupa moja ya maji kubwa baada ya nusu saa utaanza kukojoa. Baada ya kisaa ukiendelea kujisikia vibaya nenda kapime
Mwili ukikosa maji lazima ukupe taarifa utajisikia vibaya au utaumwa kichwa.

Nb mbinguni hakuna hotel hakikisha unakula vizuri. Usijinyime eti unawekeza kula kwa mpangilio.
 
Mabonge nyanya yataelewa yakianza kulazimishwa kulipia siti mbili kwenye usafiri wa umma.
fat1.jpg
 
Kwakweli ukiwa unafukia vyakula wewe unajiona sawa ila ni hatari sana ndugu zangu.
Tunaendekeza kula hovyo, dr janabi yuko sahihi.

Mleta mada asante kutukumbusha nisisitize tena tunywe maji ya kutosha, na tuache kula vyakula vigumu usiku.

Nimebadirika sana kiasi kwamba nikitembea kwa watu najikuta vyakula walivyo vipika siwezi kuvila.
Kwanza situmii , sukari, soda, juice za kununua, sili vyakula vyote vya kuunga nachemsha tu.

Mafuta kidogo nakutana nayo kwenye wali, nchicha na mayai pale ninapo yakaanga.( mchana tu)

Ratiba yangu inaanza saa 11:30 za asubuhi nakunywa ile chupa mkubwa ya maji yote. Yaani usiku wakati naenda kulala naenda nayo chumbani. (Sichemshi maji nanunua katon)
Hiyo chupa yote naipiga ingawa dr wangu wa ngozi aliniambia niwe nakunywa lita moja muda huo kabla ya mswaki..

Maji hayo hayatakiwi kuwa ya baridi yawe tu yakawaida usiyaweke kwenye friji. Nikimaliza kuyanywa huwa najisikia vibaya kwahiyo naendelea kulala kama lisaa nakaa sawa.

12:30 naamka nafanya shughuri
zangu kujianda kwenda kazini muda huo naanda breakfast ambayo sio chai nachemsha mhogo au gimbi nitakula na kipande kimoja cha labda kuku mchemsho au nakausha kweny Airflier nakula bila chai.

Saa 4: 00 nusu lita ya maji.

Chakula cha mchana tuseme saa 8 au 9 mchana hapa ndo changamojo aisee mazingira yetu ya kazi huwezi kukwepa wali, so nitakula wali kidogo na mlenda au na mboga za majani tu. Baada ya kula dk 40 zikipita nakunywa tena nusu lita ya maji.

Kuanzia saa 11 jion hadi saa 2 usiku huo muda nakuwa bado ofisin nakuwa nakunywa maji kidogo kidogo hadi saa 2 kamili usiku naenda home.

Nikifika home nafanya mazoezi kidogo kama nusu saa naoga nakula matunda tu, yaani tango mbili au papai moja au tikiti au nikisikia tumbo linalalamika kutoshiba nakula ka kipande ka kuku au ka samaki nalala. Mpaka kesho saa 11 na nusu.

Ratiba hii ni nzuri sana ukinywa maji asubuhi mapema lazima kila asubuhi uende choo.
Magonjwa kama UTI sikumbuki mwisho nimepata lini.
Ngozi yangu imekaa vizuri mno nina ule weusi chocolate flani niliyo kuwa naitamani (ni pamoja na kutumia lotion original za SH AMON'S.
Wakuu maji ni uhai.
Nb. Ukijisikia kuumwa usikimbilie kumeza dawa kwanza kunywa hata chupa moja ya maji kubwa baada ya nusu saa utaanza kukojoa. Baada ya kisaa ukiendelea kujisikia vibaya nenda kapime
Mwili ukikosa maji lazima ukupe taarifa utajisikia vibaya au utaumwa kichwa.

Nb mbinguni hakuna hotel hakikisha unakula vizuri. Usijinyime eti unawekeza kula kwa mpangilio.
Tupia kapicha ,tuone ngozi ilivyo laini,black beauty
 
Sawa uliyosema ni sahihi ila pamoja na yote maisha ni magumu wanangu lakini tusiache kula vizuri. Bora kufa ukiwa bonge kuliko kufa na utumbo uliojikunja kisa njaa 😂
Sasa maisha yalivyo magumu ndiyo uyaongezee na presha, kisukari na stress za kukosa nguvu za kiume🤣 Kuwa na afya hadi malaika mtoa roho aone uchungu anapoichukua roho yako.
 
Back
Top Bottom