Muda huu gari tatu,Polisi magari mawili na msd gari moja yamepita hapa kwa mwendo kasi ajabu wakiwa wamevalia full na siraha kamili.Aliyeko mtaani atujuze zaidi.
Updates:
Taswira ndani ya viunga vya Kariakoo.
Updates:
Taswira ndani ya viunga vya Kariakoo.
Inasemekana askari wa jiji walikuwa wanakamata biashara za wamachinga mtaa wa kongo, na wafanyabiashara hawakukubali ndipo fujo zikaanza na wafanyabiashara wakafunga barabra na kuchoma matairi, ndio Field Force wakaja kutawanya watu na mabomu ya machozi kupigwa kwa wingi na risasi za moto kupigwa hewani.
Ni hivi: ilikuwa ni operation ya kuondoa biashara holela hapa kariako hasa mitaa ya kongo na msimbazi, wamachinga wakadindisha, wakagoma kabisa! ndio vurugu za mabomu zilipoanza na watu kukimbizana kama mbwa pori.
MATOKEO: -watu wawili nasikia wamekufa kwa kugongwa na magari wakati wa mkimbizano.
- Majeruhi watatu ndio wameshushwa na taxi kwenye hospitali hapo mtaa wa lindi.., hali zao ni mbaya
BREAKING NEWS--NI VITA KARIAKOO, RISASI ZA ZARINDIMA NJENJE,MAGARI SOMA HAPA KUJUA
HABARI zilizotufikia Mda huu zinasema Vurugu kubwa imetokea mda huu maeneo ya kariakoo Jijini Dar Es Salaam na kupelekea Jeshi la polisi kurusha Risasi hovyo ili kuwatawanya Wamachinga walioanzisha Fujo hizo huku barabara za kuingia na kutoka kariakoo zikiwa zimefungwa kutokana na Matairi ya Gari yaliyochomwa moto barabarani.
Kwa Mujibu wa Shudhuda wetu aliyoko Maeneo hayo ya Kaliakoo anasema Chanzo cha vurugu hizo zinatokana na Wafanyabiashara Wadogodogo Maarufu Wamachinga kudai mfanya Biashara mwenzao kuuliwa na Mgambo wa jiji.
Shuhuda huyo alizidi kusema Mfanya Biashara huyo aliuliwa na Mgambo kwa kupigwa kipigo kikali na kumpelekea mauti, Wafanyabiashara hao wanadai hali hiyo ni ishara ya kuchoshwa na Manyanyaso hayo wanayofanyiwa na Mgambo hao na kuanzisha hali hiyo ya Fujo ambayo wanadai ni njia ya kupeleka ujumbe kwa Serikali.