DodomaTZ
Senior Member
- May 20, 2022
- 161
- 200
Saa chache kabla ya kufanyika kwa zoezi la Uchaguzi wa Madiwani, vurugu zimetokea katika Kata la Upanda Magharibu Jijini Dar es Salaam ambapo mmoja wa Watia Nia amedaiwa kwenda kufanya vurugu kwa mpinzani wake.
Video inayosambaa Mtandaoni inamuonesha Mgombea Udiwani Khallil Karim akiwa anadaia kupigwa na mmoja kati ya watu kwa lengo kuwa aumie na ashindwe kushiriki katika Uchaguzi wa Jumatatu.
Inadaiwa kuwa Karim katika maelezo yake anadai Diwani ambaye anamaliza muda wake, Adnan kitwana Kondo ambaye pia ni mgombea katika uchaguzi utakaofanyika Jumatatu Agosti 4, 2025 anahusika katika kutengeneza mazingira ya yeye kujeruhiwa.
Kondo pia anaonekana katika video inayoonesha vurugu hizo aliwa na Katibu Kata, Salma Kibene.
Polisi walifanikiwa kufika eneo la tukio na kuwachukua watu wote waliohusika katika vurugu hizo, wakapelekwa Kituo cha Polisi Salenda ambapo wamehojiwa na kuachiwa huku wakipewa maelekezo ambayo bado hayajawekwa wazi.
Shuhudia mwenyewe video kuona kilichotokea.