Vuai: CCM Zanzibar itapinga kwa nguvu serikali 3

Vuai: CCM Zanzibar itapinga kwa nguvu serikali 3

Naibu katibu Mkuu wa Zanzibar amesema CCM haiko tayari na mfumo wa serekali 3. Amesema hayo Makunduchi jana.swali: kwanini baadhi ya CCM Zanzibar haitaki serekali 3? wao wanaathirika na nini?Jee 61% ya waliotoa maoni. CCM hawamo?

Alikuwa wapi wakati wa kura ya maoni? Wengi wape, hiyo ndio demokrasia!
 
Msimamo wa Wazanzibar na Watanganyika ni Serikali 3. Huyo Vuai akachambe akalale.
 
Wengi %ngapi? 64% tunataka serikali 3,misukule inadhani tunatengeneza katiba ya lumumba! mabadiliko ni kama mafuriko,huwezi yazuia kwa mikono yako mbulura wewe! yatapita na wewe.
91 katika kula ya maoni wengi walitaka tuendelee na mfumo wa chama kimoja lakini maamuzi yakafuatwa ya wachache waliotaka tuwe na mfumo wa vyama vingi huoni mawazo ya hawa wachache leo yameonekana kuwa na nantiki kuliko hayo ya hao wengi tafakari
 
Naibu katibu Mkuu wa Zanzibar amesema CCM haiko tayari na mfumo wa serekali 3. Amesema hayo Makunduchi jana.swali: kwanini baadhi ya CCM Zanzibar haitaki serekali 3? wao wanaathirika na nini?Jee 61% ya waliotoa maoni. CCM hawamo?


Vuai hakumsikia Mwenyekiti Kikwete aliposema CCM wajiandae kisaikolojia?
 
alipaswa kutoa maoni yake kwa tume ya Jaji Warioba, na kama alitoa basi anaangukia katika 41% ya walio na maoni tofauti (not in favor of serikali 3) ilhali 61% wakipendekeza serikali 3. hapaswi kutokwa na pofu jingi, anayo nafasi katika bunge la katiba, kisha kwenye kura ya maoni, zoezi litakalo washirikisha watanzania wote, bara na visiwani! ajipange, ila mwisho wa yote atalazimika kukubali na kuheshimu mawazo ya wengi, hiyo ndiyo demokrasia, 'majority rule, minority right'. lakini, sikuwahi kumsikia akiongelea hayo maswala alipokuwa mteule wa Rais, katika wadhifa nyeti wa uwaziri. why sasa? kunani? anyways, ni haki yake ya kikatiba!!
 
Hivi Nape Nnauye aliposema CCM imekubaliana na mapendekezo ya tume sii alikuwa anaisemea CCM hihii? Sasa huyo katoka wapi tena?
Basi naye wamfukuze kama yule mwingine waliyemfukuza kwa kwenda kinyume na chama chake.
 
Last edited by a moderator:
Mimi sijui tutaishia wapi na uking'ang'anizi huu wakati wengi wanataka serikali tatu.
 
Vuai litakuchwea. Sisi CUF na Wananchi wa Zanzibar tunataka serikali 3. Tumechoka mizozo Labda hao mamluki wenzako.
 
Wacha wao CCM wakatae serikali tatu ila wananchi wanataka serikali tatu. Swali Je CCM ni Zaidi ya Wananchi?
 
Hana lolote huyo ni Vvzl sawa na Nape ambaye alikuwa kati ya watu wa kwanza kuipongeza kamati kwa rasimu ya II!
 
Hii Serikali kodi mnakwepa tatu ndo mtatoa. Bila kodi hakuna Serikali. Mashine hizo hamzitaki. Mtaendesha Serikali kwa U cuf U cdm na U ccm. Tazama madeni ya ndani kisha upime kwa namna gani utaendesha hizo Serikali. KN ya majimbo imewazungua wanajuta. Eti 3. Uchumi wa kuaminika huna co mazao wala viwanda. Acheni utani tufufuwe uchumi kwanza Serikali baadaye. Kila unacho nunua Kodi 18%. Wewe unalipa au unataka tu Serikali I!!!!!!!!!!"!"!
 
Ingekuwa ni Tatizo iwapo kichwa cha habari kingesema:

Wazanzibari watapinga serikali tatu.

Vinginevyo kama ni suala la ccm kupinga, ni halali yao kwani ni sera rasmi ya ccm kuwa na serikali mbili. Lakini kwa vile suala la katiba ni suala la umma, na sio la vyama kama ilivyokuwa 1977, ndio maana watanzania zaidi ya 60% wamependelea serikali tatu kwa mujibu wa rasimu ya katiba. Muhimu zaidi ni kwamba, Vuai anaongelea wanachama wa ccm wasiozidi milioni sita ambao hawazidi 13% ya watanzania, na isitoshe, wana ccm zanzibar hawafiki hata asilimia moja ya watanzania. Kwa maana hii, kauli ya vuai maana yake ni kwamba:

<1% ya watanzania hawatakubali serikali tatu
.

Na kauli kama hizi zikitoka kwa wana lumumba (bara) maana yake ni kwamba:

13% ya watanzania hawatakubali serikali tatu
Vuta nikuvute itakuwa baina ya hao na wale zaidi ya 60% waliopendelea serikali tatu kwa mujibu wa rasimu ya katiba. Hadi hapo tunaona busara ipo wapi.

Cc Nguruvi3, Jasusi, JokaKuu, ZeMarcopolo, MwanaDiwani, MTAZAMO et al.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Naibu katibu Mkuu wa Zanzibar amesema CCM haiko tayari na mfumo wa serekali 3. Amesema hayo Makunduchi jana.swali: kwanini baadhi ya CCM Zanzibar haitaki serekali 3? wao wanaathirika na nini?Jee 61% ya waliotoa maoni. CCM hawamo?

wazanzibar walizoea vya bure vya tanganyika sasa watakula jeuri yao, kama hawataki serikali tatu basi moja! tumeshindwa kuwadekeza hawa midebwedo
 
Back
Top Bottom