Vuai: CCM Zanzibar itapinga kwa nguvu serikali 3

Vuai: CCM Zanzibar itapinga kwa nguvu serikali 3

ugasa

Senior Member
Joined
Oct 21, 2013
Posts
193
Reaction score
52
Naibu katibu Mkuu wa Zanzibar amesema CCM haiko tayari na mfumo wa serekali 3. Amesema hayo Makunduchi jana.swali: kwanini baadhi ya CCM Zanzibar haitaki serekali 3? wao wanaathirika na nini?Jee 61% ya waliotoa maoni. CCM hawamo?
 
Tanachanganyikiwa kama hii tume imeona watz wanautaka Muungano basi inamaana Serikali 1 mbili ama tatu za kufanya nn. Watufafanulie
 
serikali tatu safi na mbeleni tunataka serikali za majimbo
 
HAhahaaaaaaaa ndo shida ya kutokubali watu hawa. Huu mwaka watahama nchi tu!!!!!!
 
''hatuongei na mbwa tunaongea na mwenye mbwa''., Akina Vuai achaneni nao huyu hawashi wala hazimi., yupo yupo tu na ukada wake.,
 
Safi sana Vuai nchi hii ya wote, tulio wengi tunataka serikali mbili,achana na hawa mavuvuzela.
 
Vuai anajua kuwa serikali tatu ndio mwisho wa Muungano na dezo ambazo Zanzibar wanapata katika Muungano. Kwa vile serikali mbili haikubaliki basi kilichobaki ni serikali moja au Muungano uvunjwe. Hawakutegemea wakina Warioba wange"call their bluff".

Amandla.......
 
Serikali 3 tumechoka kila siku kusingiziwa tunawanyonya tu mara hatuwataki machogo kwetu wakati huku Tanganyika wamejaa mpka huku kwetu Tandahimba.Serikali 3 na kila serikali washirika achangie sawa kwnye serikali ya Muungano.
 
Safi sana Vuai nchi hii ya wote, tulio wengi tunataka serikali mbili,achana na hawa mavuvuzela.

Wengi %ngapi? 64% tunataka serikali 3,misukule inadhani tunatengeneza katiba ya lumumba! mabadiliko ni kama mafuriko,huwezi yazuia kwa mikono yako mbulura wewe! yatapita na wewe.
 
Serikali tatu haziepukiki! Mwisho wake ni kura ya maoni ambapo wengi ndio watakaoamua.

Kama CCM inahisi ina mass ya kutosha, iboreshe daftari la wapiga kura ili ipate kura nying zaidi!
 
Serikali tatu ndio mpango tumechoka kubeba majitu yasiobebeka,kila mtu ajitegemee na achangie sawa kwenye serikali ya muungano,
porojo hatutaki.
 
Naibu katibu Mkuu wa Zanzibar amesema CCM haiko tayari na mfumo wa serekali 3. Amesema hayo Makunduchi jana.swali: kwanini baadhi ya CCM Zanzibar haitaki serekali 3? wao wanaathirika na nini?Jee 61% ya waliotoa maoni. CCM hawamo?
wanaopinga serikali 3 wamepitwa na wakati, bila Tanganyika hakuna muungano,kwa maana nyingine Zanzibar imeungana na nchi gani?
 
Back
Top Bottom