VPL: Simba SC Vs Azam FC

VPL: Simba SC Vs Azam FC

".. tushukuru Mungu Okwi yupo hai hadi sasa, maana alipigwa kiwiko mshipa wa fahamu ulio nyuma chini ya kichwa chake na ndo maana alipoteza fahamu kwa zaidi ya dk 10"
Source: Dr. wa Simba Sc.

Nami pia nategemea kuona hatua kali saaana zikichukuliwa.
TFF ni lazima iwe makini zaidi, kwa sasa ligi imegeuka vita. Ladha ya soka safi inapotea na kinachoanza kuota mizizi ni kukamiana na rafu chafu zenye kuhatarisha uhai kwa wachezaji. Itafika wakati tutashindwa kuona tactical holding, piercing and physical confrontation kwa sababu wachezaji wataogopa kukaa na mpira au kulazimisha move kati kati ya msitu wa mabeki kwa kuogopa kilichompata Emanuel Okwi na Amis Tambwe. Kuna njia rafiki za kuchukua mpira kwa adui kama tackling and tactical obstruction ( refa akipeta poa) lakini huu uhuni mtauana. Marefa muwe makini . Faulo walizofanyiwa Tambwe na Okwi technically and tactically zina muathiri mchezaji kisaikolojia.
FAIR PLAY PLEASE
 
TFF ichukue hatua...OKWI alichezewa faulu mbaya sana ambayo ingeweza kupelekea kifo chake

Sasa tuone TFF na double standards zake
Ingekuwa ni mchezaji wa Yanga TFF ingechukua hatua kali za kisheria, lakini kwa Simba waliombea hata afe kabisa.
 
Mkuu kwa Yanga ile ni siasa tu imefanyika....wale jamaa Tambwe na Michae wote walikua wanapeana vikumbo kwa zamu.

Wote wamepigana ngumi za kisiri siri.

Sema tu kwa sababu Yanga ni timu ya Magazeti ndio maana imekuwa vile.

Sasa nataka ushuhudie jinsi TFF ilivyo na Double standard.Katika hili la OKWI kupigwa hadi kuzimia/kukaribia kufa....na hakuwa na mpira.

Nakuhakikishia TFF haitachukua hatua zozote
Ikichukua hatua nitashangaa sana....
 
TFF ni lazima iwe makini zaidi, kwa sasa ligi imegeuka vita. Ladha ya soka safi inapotea na kinachoanza kuota mizizi ni kukamiana na rafu chafu zenye kuhatarisha uhai kwa wachezaji. Itafika wakati tutashindwa kuona tactical holding, piercing and physical confrontation kwa sababu wachezaji wataogopa kukaa na mpira au kulazimisha move kati kati ya msitu wa mabeki kwa kuogopa kilichompata Emanuel Okwi na Amis Tambwe. Kuna njia rafiki za kuchukua mpira kwa adui kama tackling and tactical obstruction ( refa akipeta poa) lakini huu uhuni mtauana. Marefa muwe makini . Faulo walizofanyiwa Tambwe na Okwi technically and tactically zina muathiri mchezaji kisaikolojia.
FAIR PLAY PLEASE

Niliogopa sana pale wachezaji walivokua wanarushiana daruga live mbele ya refaree....zaidi ya mara 5...refa anaangalia tu.

Niliogopa sana Kavumbagu anamsukuma beki kwenye 18 na anampiga teke kipa wakati ameshashika mpira.

Niliogopa sana kuona refa anapotezea tu.

Nikajiuliza huyu refa haoni au kuna nini?

Anataka watu wajichukulie sheria mkononi?

Kwa rafu aliyochezewa Okwi...kupigwa kiwiko akiwa hana mpira...ikiachwa hivi hivi...simba tutajua cha kufanya
 
Ingekuwa ni mchezaji wa Yanga TFF ingechukua hatua kali za kisheria, lakini kwa Simba waliombea hata afe kabisa.

Juzi mlikuwa mnashangilia Tambwe alivyopigwa leo kapigwa mchezaji wenu ndio mnagundua kuna shida, wachezaji wa bongo hawajui fair play
 
Niliogopa sana pale wachezaji walivokua wanarushiana daruga live mbele ya refaree....zaidi ya mara 5...refa anaangalia tu.

Niliogopa sana Kavumbagu anamsukuma beki kwenye 18 na anampiga teke kipa wakati ameshashika mpira.

Niliogopa sana kuona refa anapotezea tu.

Nikajiuliza huyu refa haoni au kuna nini?

Anataka watu wajichukulie sheria mkononi?

Kwa rafu aliyochezewa Okwi...kupigwa kiwiko akiwa hana mpira...ikiachwa hivi hivi...simba tutajua cha kufanya
Kwa marefa hawa TFF na FRAT yake ijiandae kuchukua maiti ya refa siku moja. Mimi ninaamini hawa marefa sio kwamba wanahongwa ila hawana uwezo wa kuchezesha mpira wa miguu.

Mkuu unakumbuka pale mchezaji wa Simba alipochezewa rafu na kuanguka chini refa alipeta kwa kuwa Simba ilikuwa inashambuliwa, mpira ulipochukuliwa na Simba kuelekea lango la Azam ndipo alipiga filimbi ya kusimamisha mchezo jamaa atibiwe. Hata mtangazaji wa TBC Taifa alimshangaa refa kwa tukio lile.
 
Juzi mlikuwa mnashangilia Tambwe alivyopigwa leo kapigwa mchezaji wenu ndio mnagundua kuna shida, wachezaji wa bongo hawajui fair play

Tambwe hakupigwa ila walipigana.

Sema maamuzi yamefanyika kisiasa
 
Kwa marefa hawa TFF na FRAT yake ijiandae kuchukua maiti ya refa siku moja. Mimi ninaamini hawa marefa sio kwamba wanahongwa ila hawana uwezo wa kuchezesha mpira wa miguu.

Mkuu unakumbuka pale mchezaji wa Simba alipochezewa rafu na kuanguka chini refa alipeta kwa kuwa Simba ilikuwa inashambuliwa, mpira ulipochukuliwa na Simba kuelekea lango la Azam ndipo alipiga filimbi ya kusimamisha mchezo jamaa atibiwe. Hata mtangazaji wa TBC Taifa alimshangaa refa kwa tukio lile.

Nadhani kuna tatizo la msingi la ma refaereee

Nafikiri sio ishu ya kuhongwa

Ni ishu ya Competence na kukosa kujiamini

Kukosa kujiamini (Confidence) katika maamuzi ni tatizo la watanzania wengi

cc Makoye Matale
 
Last edited by a moderator:
Mkuu penye ukweli lazima usemwe. Refa aliyechezesha mechi ya Yanga na Polisi alishindwa kuthibiti nidhamu uwanjani matokeo yake mpira ukageuka vita badala ya burudani.

Jana mechi ya Simba vs Azam tuliokuwepo kiwanjani na hata walioshuhudia kupitia Luninga waliona refa kipindi cha pili mpira ulivyomshinda.
1. Lile tukio la Kavumbagu kumpiga teke la makusudi kipa wa Simba Manyika alitakiwa kutoa onyo. Matokeo yake rafu za kijinga zikaanza .
2. Tukio la mchezaji wa Simba kuchezewa rafu na kugaagaa chini lakini refa alipeta kwa kuwa Simba ilikuwa inashambuliwa. Baada ya Simba kunyan'ganya mpira na kuanza kuelekea langoni mwa Azam Refa akapiga filimbi ya kusimamisha mchezo ili mchezaji atibiwe. Inashangaza sana.
3. Tukio la wachezaji kurushiana madaluga upande wa mashariki ya uwanja kama mara nne hivi lilitokea tena mbele ya Refa, mpaka mchezaji wa Simba alipokita njumu kwenye ugoko wa mchezaji wa Azam ndipo refa alipopuliza filimbi.

Kwa matukio hayaTFF kupitia FRAT ina kazi kubwa sana ya kufanya.


Siku hizi TFF wana kitu cha ziada ukiacha report ya mwamuzi. Kuna CD/DVD ya kila mchezo. Sielewi kwa nini hawatumii hizo kutathmini kazi za marefa. Kwa mwendo huu, sioni mwamuzi wa Tanzania AFCON. Kombe la dunia ndio kabisa.
Kutoa goli tata au kukataa Lile la halali unaweza kusema mlungula umepita. Rafu zilizo dhahiri mbele ya mwamuzi sijui tuite kitu gani. Wachezaji wameanza kujenga imani kwamba marefa hawajui wajibu wao hivyo watafanya lolote uwanjani
 
Juzi mlikuwa mnashangilia Tambwe alivyopigwa leo kapigwa mchezaji wenu ndio mnagundua kuna shida, wachezaji wa bongo hawajui fair play
Mkuu hakuna mtu aliyeshangilia hapa, kilichofanyika ilikuwa ni kulinganisha alichofanya Tambwe na beki wa Ruvu Shooting na malalamiko yaliyotolewa na Yanga.

Okwi hakumfanyia mtu yoyote faulo na hakuwa na mpira lakini amefanyiwa faulo mbaya kuliko hata ile ya Tambwe.
 
Malipo yako duniani hapa hapa. Hivi majuzi mliinyoshea vidole Yanga kwa kulalamikia umafia aliotendewa Amisi Tambwe, mkadai Yanga ni timu ya kulalamikalamika tu. Hata wiki haijapita mmekutana na kigongo cha wiki na kuanza kulalama. Pole sana.

Anyway, tuache utani wala ushabiki, hatua lazima zichukuliwe vinginevyo makubwa zaidi yanaweza kutokea uwanjani.

Kuhusu suala la Tambwe, Bodi ya Ligi walikurupuka kutoa maamuzi ya haraka kabla hata kupata maelezo ya kamisaa wa michezo.. eti kisa Yanga katishia kujitoa katika ligi!!

Mf. Simba Sc ikasema itajitoa katka ligi [japo sitegemei kauli kama hii] kama mwamuzi asiposimamishwa itakuaje?? Je napo watamsimamisha mwamuzi??

Bodi ya Ligi inatakiwa iwaamini viongozi inaowateua kusimamia mechi kama makamisaa, marefa, n.k.. tofauti na hali ilivyo sasa ya kupuuza ripoti za makamisaa.
 
Malipo yako duniani hapa hapa. Hivi majuzi mliinyoshea vidole Yanga kwa kulalamikia umafia aliotendewa Amisi Tambwe, mkadai Yanga ni timu ya kulalamikalamika tu. Hata wiki haijapita mmekutana na kigongo cha wiki na kuanza kulalama. Pole sana.

Anyway, tuache utani wala ushabiki, hatua lazima zichukuliwe vinginevyo makubwa zaidi yanaweza kutokea uwanjani.
Mkuu fuatilia post yangu kuhusu rafu alizofanyiwa Tambwe, si kila mwanasimba alifurahishwa na zile rafu, wengine ni waumini wa fair play bila kujali nani hajafanya fair. Hata jana kama ulifuatilia vizuri baada ya rafu aliyofanyiwa Okwi post humu jukwaani zilipungua. Mchezaji anapigwa kiwiko hana mpira mpaka anapoteza fahamu na hakuna kadi iliyotoka na bado kuna wapuuzi wachache wanashangilia na kusema Simba wanatafuta sare kwa hiyo sijui walitaka wachezaji wetu wote wazimie ndo wafurahi, nadhani kuna haja ya wachezaji kufundishwa hata elementary ya mwili wa binadamu na sehemu gani zina madhara unapomgonga mchezaji na wakatazwe kabisa na ikitokea tu mchezaji kafanya hivyo afungiwe mechi kadhaa na faini juu mbona mabondia wamewekewe sheria kabisa hakuna kupiga below the belt kwa sababu wanajua mtu unaweza pigwa viungo vya uzazi, hakuna kupiga nyuma ya kichwa kwa sababu huko kuna mishipa ya fahamu na unaweza kusababisha mtikisiko wa ubongo pia. Haya madhara ya kujifanya kutojua madhara yake unakuta mchezaji mwingine anamgonga mwenzake kwenye uti wa mgongo. Kuna ulazima wa wachezaji kukumbushwa mara kwa mara kwamba mpira sio vita hata vita yenyewe kuna baadhi ya silaha haziruhusiwi.
 
Nadhani kuna tatizo la msingi la ma refaereee

Nafikiri sio ishu ya kuhongwa

Ni ishu ya Competence na kukosa kujiamini

Kukosa kujiamini (Confidence) katika maamuzi ni tatizo la watanzania wengi

cc Makoye Matale

Nashukuru sana kwa kukubaliana na low competency ya marefa wetu. Sisi Yanga tunapowalalamikia msiwe mnatuzodoa bali tuungane pamoja ili haki itendeke uwanjani kwa maslahi na mustakabali wa soka letu. Muda wa kuchekekelea mtu kuumizwa maadam ni wa timu pinzani umepita.
 
Huyu bwana anashindwa kujua kuwa Timu ya kwanza na simba zinatofautiana kwa point za gemu tatu tu

Na azam iko mbele kwa gemu moja

Hii simba itawaua kina Makoye Matale mwaka huu

Hakuna Simba ya kutuua sisi mwaka huu. Nawapongeza sana Simba kwa uamuzi wa kujenga timu ya vijana. Hata hivyo ujenzi wa timu una gharama zake ambazo ni pamoja na kupishana na vikombe kila mwaka na hata kukosa nafasi ya uwakilishi katika mechi za kimataifa. Nadhani unakumbuka Yanga tulivyofanya maamuzi magumu ya kuendeleza vijana waliojulikana kama "Yosso" Enzi za marehemu Tambwe Leya; baadhi yao ni akina Anwar Awadh, Salvatory Edward na wengineo. Tulipishana na vikombe kwa muda baadaye tukarudi mchezoni na kufanya kweli.

Hivyo, Simba endeleeni na ujenzi huo lakini kwa mwaka huu kikombe msahau kabisa. Hizo mechi tatu unazosema ni tofauti ni nyingi mno, kuli-cover ni vigumu. Sasa hivi ligi inaelekea ukingoni mwa round ya kwanza. Huenda kuanzia mwakani tukashuhudia matunda ya ujenzi wa timu yenu.
 
Back
Top Bottom