VODACOM MNATUZOEA VIBAYA WATEJA WENU, MNATUNYONYA!
VodaCom.......VodaCom....VodaCom....!
Vodacom Tanzania
Tafadhari sana Kampuni kumbwa kama nyinyi kila siku mnajinasibu kuwa ni kampuni na mtandao unaongoza Tanzania. Sasa kwenu nyinyi wakubwa uendeshaji wa kibiashara wa mtandao wenu hukoje???? Kwasababu Yaani badala ya kuwa wenye kujali wateja wenu kwa kuwadumisha waendelee kutumia huduma zenu kwa huduma zenye bei nafuu lakini imekuwa wakubwa mwenye wateja wengi ambao sasa Mnatunyonya wateja wenu. Sasa kila siku mnaongeza tu gharama za kutumia mtandao wenu Yaani kifupi hamueleweki nini mnatafuta. Kwasababu kama biashara mnafanya vizuri na wateja wengi mnao sasa kwanini mnashindwa kuwa “Customer-care Oriented” nyie mnakuwa tu “Profit-care oriented”. Yaani kifupi mnatunyonya sana wananchi wa kawaida kama sisi. Kwa mabadiliko haya mlioyafanya ya mabando ni wazi kuwa mnatunyonya hakuna kingine cha kusema zaidi ya unyonyaji huu.
*Ya kawaida mambo ya ajabu ni haya:
i). Tsh.5,000= 2GB (kwa masaa 48)
ii).Tsh.2,000= 1GB (kwa masaa 24)
*Ya UNI-OFFER ndio maajabu huko yaani ni unyonyaji mtupu:
i). Tsh.3,000= 1.2GB( kwa siku 7)
ii).Tsh. 2,000= 512GB (kwa siku 7)
iii).Tsh. 1000= 500GB(kwa siku 7)
MY TAKE:
Yaani nawashauri sanaa VodaCom-Tz Yaani kama mnashindwa kuendesha huu mtandao kwa gharama ambazo ni rahisi kama wenzenu wanavyotumia nawashauri muache kujinadi kuwa ni kampuni na mtandao unaongoza Tanzania, kwasababu ninawasiwasi hata kwa upangaji wa bei zenu za data zenu sizani kama mnatumia njia hizi kuu za uuzaji..1. COST-PLUS METHOD 2.COMPETITIVE COMPARING METHOD 3. WHAT MARKET WILL BEAR METHOD.
Kwasababu kama mngekuwa mnatumia hizo njia msinge tunyonya hivyo kwakuwa mngeweza kuwa sawa na wenzenu kama TTCL au makampuni mengine kwa mfano gharama za TTCL ni za chini kweli:
i). Tsh. 1,500 = GB 1(kwa siku 7)
ii). Tsh.2,500=. GB 2.2( kwa siku 7)
Najua TTCL ni ya serikali lakini hata kama nyinyi ni tofauti na hawa haiondoi uhalalali wa nyinyi kwenda kinyume na tofauti sanaa na Mitandao mengine. Yaani hapa kuna Tatizo.
MWISHO:
Tegemeeni kupoteza wateja wengi sana hasa wale tunaotumia mabando ya internet na ambao ni wengi zaidi kama Hamtabadilika.