only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...Kuna taarifa zimeanza kusambaa kuwa VODACOM-Tanzania inaweza ikajitoa kudhamini Miss Tanzania muda si mrefu watatoa taarifa rasmi.Akiongea Meneja Masoko wa Vodacom ndugu George Rwehumbiza alisema tayari barua ya kuonyesha wazo lao la kutaka kujitoa wamekwisha liwakilisha kwa Mkurugenzi wa Rino Agency ndugu Hashim Lundenga.Pengine hii inaweza kuwa ni pigo kubwa kwa waandaaji wa shindano hili na inaweza kuwa ndio mwanzo wa Hashim Lundenga kupoteza sehemu ya mapato yake kwa kiasi kikubwa.Alipotafutwa ili kutoa maelezo juu ya hili hakuweza kukubali wala kukataa juu la hili zaidi ya kutoa maelezo marefu yasiyo jibu swala husika.
source:Mwananchi
source:Mwananchi