Vodacom kufuta vifurushi vya Uni Offer

Vodacom kufuta vifurushi vya Uni Offer

Nilikuwa nafikiria nami niingie VODA, lakini kwa hili ni ngumu. Nilitaka kujiunga nao kutokana na maelekezo ya TCRA kuwa kila mtu awe na laini moja kwenye kampuni hizi, mimi nina laini mbili za AIRTEL, moja kwenye simu na moja kwenye MODEM yao ambayo nimekuwa nayo tangu 2010! Sasa VODA wanaleta zao za kuleta sijui mnanishauri nihamie wapi wana JF!
 
Kifurushi changu kinaisha leo cha 3000/= kwa 2GB, ila sasa wameshusha hadi 1.2GB kwa 3000/=


Nipo hapa nyumbani(TTCL) ni kitendo cha kufungua mlango na kuanza kuunga juhudi mdogo mdogo.

Vodacom Tanzania endeleani na kiburi chenu
Tangu wanipe gb 1.2 kwa 3000,nimerudi halotel
 
Nipo zangu zantel huku hakuna shida kabisa..... Wakizingua zentel naenda kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano
 
1500
1gb + 500mb wiki au sijui iko chako hebu nijuze unajiungaje

Maana wamepandisha na wao
Hao halotel gb 1 wiki nzima plus dakika 100 na sms 2000 kwa wiki unanunua kupitia halopesa.... Ukiweka vocha ya kawaida hupati hiko kifurushi


Piga menu ya halopesa nenda kwenye Mega bando
 
Vodacom kama mnausoma huu uzi inabidi mrudishe vifurushi vya uni offer,wateja wenu wanalalamika,muda si mrefu mtakosa watumiaji maana tunahamia mitandao mingine

RUDISHENI VIFURUSHI VYA UNI OFFER
Mimi kama mtandao hauvutii natupa line. Hata huwa sijiulizi mara mbilimbili.
 
Back
Top Bottom