Vituo vya Chapati na Mihogo ya kukaanga ndiyo uchumi mpya wa Dar es Salaam?

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Maeneo mengi ya Dar es Salaam sasa yametawaliwa na machine za kukanda chapati na majiko ya kukaanga mihogo pembezoni mwa barabara hasa mida ya jioni

Na kuna wengine wanakaanga mihogo chini ya nguzo za umeme hasa maeneo ya kariakoo na Posta

Zamani ilikuwa ukiona watu wamekaa mzunguko unajua ni wale wala pweza ,Lakini sasa watu wanakula chapati na mihogo ya kukaanga hasa mida ya jioni

Vituo hivi vimefumuka kwa kasi sana ambayo inaleta shaka juu ya pato na maisha ya watu

Lengo la huu uzi ni kuangalia kwanini wanatumia sponji kukaanga zile chapati,Unakuta kile kigodoro kinapungua siku hadi siku ,Je si kinaishia kwenye chapati

Pia wakaanga mihogo wanafunika mihogo kwa kutumia nailoni na maboksi wakati wa kupika,Hii si ni hatari kwa afya?

Mamlaka za Afya hazioni hili ni janga kubwa kutumia sponji kukaanga chapati au kutumia nailoni na maboksi wakati wa kupika mihogo? Au chapati na mihogo ndio maendeleo yenyewe ya kiuchumi ndani ya Dar es Salaam?
 
Muhogo mmoja/kipande 300tsh
Chukulia ndoo moja kubwa shambani inauzwa 2000tsh inatoa vipande 100
100×300= 30000tsh
Ukiondoa gharama za kawaida
Faida si chini ya 20000tsh kwa Ndoo kubwa....katikati ya Mji hususani Dsm
 
Maeneo mengi ya Dar es Salaam sasa yametawaliwa na machine za kukanda chapati na majiko ya kukaanga mihogo pembezoni mwa barabara hasa mida ya jioni

Na kuna wengine wanakaanga mihogo chini ya nguzo za umeme hasa maeneo ya kariakoo na Posta

Zamani ilikuwa ukiona watu wamekaa mzunguko unajua ni wale wala pweza ,Lakini sasa watu wanakula chapati na mihogo ya kukaanga hasa mida ya jioni

Vituo hivi vimefumuka kwa kasi sana ambayo inaleta shaka juu ya pato na maisha ya watu

Lengo la huu uzi ni kuangalia kwanini wanatumia sponji kukaanga zile chapati,Unakuta kile kigodoro kinapungua siku hadi siku ,Je si kinaishia kwenye chapati

Pia wakaanga mihogo wanafunika mihogo kwa kutumia nailoni na maboksi wakati wa kupika,Hii si ni hatari kwa afya?

Mamlaka za Afya hazioni hili ni janga kubwa kutumia sponji kukaanga chapati au kutumia nailoni na maboksi wakati wa kupika mihogo? Au chapati na mihogo ndio maendeleo yenyewe ya kiuchumi ndani ya Dar es Salaam?
Wa Tanzania wengi wanaishi kwa buku jero kwa siku, au chini, harafu kuna kenge anaisifia ccm, na wengine kama wamekalia vile, wanasema "makinda akifanya dhihara, anatatua shida za watu"
Wa Tanzania wengi ni mafukara, kwa wanaoishi Dar, wale wanawake, wanaokaanga, karanga,tsmbi, anauza maji vichupa vitatu, na energy,wana maisha magumu Sana, umaskini kwenda mbele
 
Back
Top Bottom