Dah.! Umenikumbusha mbali sana mkuu yaani tukisema kila mtu arudie kazi yake ya zamani...!
Mfano mimi nilikuwaga na washkaji flani tukawa tunaiba mafuta ya transformers ila sintosahau siku tulipoparamia transformer flani ghafla ulisikika mripuko wa ajabu kufumba na kufumbua mwenzetu mmoja alikufa pale pale mwingine alifia hospital kuanzia siku hiyo niliacha kabisa kazi hiyo.
Namshukuru Mungu sa ivi niko zangu Dom nna banda langu natengeneza na kuuza majeneza na maisha yangu yako fresh nimejenga,nimeoa na nnamiliki
"Kagari" japo ni kama kale ka Mr bean.

maisha yana historia ndefu sana.