Chief Wingia
JF-Expert Member
- Jul 12, 2013
- 2,863
- 5,095
Habari zenu wakuu
Aisee ipo hivi kuna jirani hapa mtaani ana kijana wake anatarajia kuoa mwaka huu hivyo nikapewa mwaliko wa kikao cha kwanza cha harusi ambayo ilikuwa ni weekend.
Ila tokea nilipopata mwaliko nikawa nawaza why kikao kikafanyike mahala pagharama hivi wakati kuna sehemu za kawaida tu au hata nyumbani kwa huyu jirani tungefanya kikao.
Aaah! Ila nikapuuza na wala sikumuhoji muhusika zaidi ya kuitikia wito na siku ilipofika nikaenda kwenye kikao hivyo tuliowahi tukakaa kidogo kusubiri watu wengine then kikao kikaanza.
Nilianza kuona utofauti walipotaja budget ya ndoa ni 30.4M na kisha ahadi ya muoaji ni 1M na ahadi ya wazazi wa muoaji ni 2M, kimoyomoyo nikajisemea hivi hawa kenge jangwa ni timamu kweli wanategemea 27.4M watazipata kwa kuchangiwa.
Pledges zilipoanza kila mtu akatoa ahadi yake pale hadi tunafunga kikao ahadi ni 10M kwahiyo kuna loss ya 20.4M na ukumbuke kuna walioahidi ila hawatakupa mchango.
Nawasilisha.
Aisee ipo hivi kuna jirani hapa mtaani ana kijana wake anatarajia kuoa mwaka huu hivyo nikapewa mwaliko wa kikao cha kwanza cha harusi ambayo ilikuwa ni weekend.
Ila tokea nilipopata mwaliko nikawa nawaza why kikao kikafanyike mahala pagharama hivi wakati kuna sehemu za kawaida tu au hata nyumbani kwa huyu jirani tungefanya kikao.
Aaah! Ila nikapuuza na wala sikumuhoji muhusika zaidi ya kuitikia wito na siku ilipofika nikaenda kwenye kikao hivyo tuliowahi tukakaa kidogo kusubiri watu wengine then kikao kikaanza.
Nilianza kuona utofauti walipotaja budget ya ndoa ni 30.4M na kisha ahadi ya muoaji ni 1M na ahadi ya wazazi wa muoaji ni 2M, kimoyomoyo nikajisemea hivi hawa kenge jangwa ni timamu kweli wanategemea 27.4M watazipata kwa kuchangiwa.
Pledges zilipoanza kila mtu akatoa ahadi yake pale hadi tunafunga kikao ahadi ni 10M kwahiyo kuna loss ya 20.4M na ukumbuke kuna walioahidi ila hawatakupa mchango.
Nawasilisha.

