Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wlaya ya Kishapu, Elly Mlaki, ameangua kilio ndani ya kikao cha Baraza la madiwani wa halmashauri hiyo, baada ya kushindwa kujibu swali la mmoja wa madiwani.
Tukio hilo lilitokea jana mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ambamo kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Brigedia Jenerali Dokta Yohana Balele, kilifanyikia.
Hatua ya Mkurugenzi huyo kuangua kilio, Ilikuja baada ya Diwani wa Magalata, Albert Kapongo, kumuliza swali lililohusu jinsi ofisi yake ilivyotumia Sh 120 milioni, kununulia lori la Idara ya Elimu.
Hata hivyo mkurugenzi huyo, hakutoa maelezo ya kina kuhusu swali hilo, jambo lililomsukuma Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,kuingilia kati na kutaka ufafanuzi wa kina juu ya swali hilo.
"Ndugu mkurugenzi naomba kupata ufafanuzi wa matumizi ya Sh120 milioni zilizotumika kununulia lori la Idara ya Elimu,"alisema.
Akijibu swali hilo mkurugenzi huyo alidai kuwa lori hilo halijanunuliwa na kwamba fedha hizo zimetumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo mandalizi ya ziara mbalimbali za viongozi wa kitaifa.
"Nataka utoe ufafanuzi wa jinsi fedha hizo zilivyotumika," ling'aka Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, hatua iliyomlazimisha mkurugenzi huyo kuendelea kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu fedha hizo.
Alidai Sh 2 milioni katika kuwa fedha hizo zilitumika kununulia kapeti la rais na Sh 5 milioni, zilitumika kuwalipa walimu tarajali.
Hata hivyo mkuu wa mkoa alizidi kumbana zaidi mkurugenzi kuhusu fedha ambazo kimsingi, hakizikupaswa kutumika kwa shughuli nyingine.
"Hizo fedha zingine zilizobaki zikowapi,"aliuliza mkuu wa mkoa.
Kufuatia kubanwa kwa maswali hayo, mkurugenzi huyo aliaanza taratibu kutoa kwikwi na baadaye kuangua kilio hadharani kwa sauti kubwa na kuwafanya madiwani kushikwa na butwaa.
Hali hiyo ilipoendelea mkuu wa mkoa alimwomba mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuahirisha kikao hicho kwa vile haikuwa rahisi tena kuendelea nacho wakati kuna kilio cha mkurugenzi.
Kikao hicho kimepangwa kufanyika tena leo.
Tukio hilo lilitokea jana mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ambamo kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Brigedia Jenerali Dokta Yohana Balele, kilifanyikia.
Hatua ya Mkurugenzi huyo kuangua kilio, Ilikuja baada ya Diwani wa Magalata, Albert Kapongo, kumuliza swali lililohusu jinsi ofisi yake ilivyotumia Sh 120 milioni, kununulia lori la Idara ya Elimu.
Hata hivyo mkurugenzi huyo, hakutoa maelezo ya kina kuhusu swali hilo, jambo lililomsukuma Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,kuingilia kati na kutaka ufafanuzi wa kina juu ya swali hilo.
"Ndugu mkurugenzi naomba kupata ufafanuzi wa matumizi ya Sh120 milioni zilizotumika kununulia lori la Idara ya Elimu,"alisema.
Akijibu swali hilo mkurugenzi huyo alidai kuwa lori hilo halijanunuliwa na kwamba fedha hizo zimetumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo mandalizi ya ziara mbalimbali za viongozi wa kitaifa.
"Nataka utoe ufafanuzi wa jinsi fedha hizo zilivyotumika," ling'aka Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, hatua iliyomlazimisha mkurugenzi huyo kuendelea kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu fedha hizo.
Alidai Sh 2 milioni katika kuwa fedha hizo zilitumika kununulia kapeti la rais na Sh 5 milioni, zilitumika kuwalipa walimu tarajali.
Hata hivyo mkuu wa mkoa alizidi kumbana zaidi mkurugenzi kuhusu fedha ambazo kimsingi, hakizikupaswa kutumika kwa shughuli nyingine.
"Hizo fedha zingine zilizobaki zikowapi,"aliuliza mkuu wa mkoa.
Kufuatia kubanwa kwa maswali hayo, mkurugenzi huyo aliaanza taratibu kutoa kwikwi na baadaye kuangua kilio hadharani kwa sauti kubwa na kuwafanya madiwani kushikwa na butwaa.
Hali hiyo ilipoendelea mkuu wa mkoa alimwomba mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuahirisha kikao hicho kwa vile haikuwa rahisi tena kuendelea nacho wakati kuna kilio cha mkurugenzi.
Kikao hicho kimepangwa kufanyika tena leo.