Taarifa kwenye picha kuna Mwananchi amepanda NGUZO ya umeme wa msongo wa kilovoti 132 njia Mwanza-Musoma Nguzo namba 500 iliyopo Mwibagi Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara.
Mara baada ya kupata taarifa watu wetu wamewasiliana na Mkuu wa kituo cha polisi Kiabakari na kufanikiwa kufika eneo la tukio kwa wakati.
Timu yetu imefika na kumshawishi mhusika kushuka bila mafanikio. Jitihada za kumshusha bila kudhurika zinaendelea, na tunaweza kulazimika kuzima laini hiyo ambayo itapelekea Mkoa wote wa Mara kukosa umeme.