antimatter
JF-Expert Member
- Feb 26, 2017
- 49,688
- 130,567
Unakumbuka Sheria za mpira za utotoni?
1.Mwenye mpira Lazima acheze hata kama hajui mpira2.Dogo mnene Lazima awe golikipa
3.Mwenye mpira ataamua nani acheze na nani asicheze
4.kama haujashiriki kufuma mpira unaweza usipate namba
5.Ukichaguliwa mwishon ujue uwezo wako ni mdogo kuliko wote
6.Mwenye mpira akikasirika mpira umeisha, maana anauchukua na kusepa kimyakimya..
7.Inaruhusiwa kubadili golikipa kama ikitokea penat na baada ya hapo ataendelea kudaka yule yule
8.Mechi itaisha pale giza linapoingia
9.wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufuata mpira ukitoka nje
10.mtaalam wa soka huwa hakoc namba hata siku moja!
Ukiikumbuka unatabasam😁

