Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Bange noma!​

Kuna wana walikuwa wakivuta bange, kiberiti kikawaishia, wakamtuma mwenzao akatafute kingine, Ila bangi lilikuwa limemkolea sanaaa!
Akazungukazunguka huko na huko, hatimaye akarudi palepale kijiweni…
MWANA: oyaaa wanangu eeeh.. niazimeni kiberiti mwanangu mwenyewe...
WENZAKE: baharia eeeh, subiria kimtindo kuna mwana tumemtuma akatafute kiberiti mbele huko, atarejea muda muda tuu..
MWANA: akaketi kusubiria..
 

Mvua yazua jambo!​

Baba:- Halloo mke wangu..
Mama: abee mume wangu
Baba:- yaani ni shida huku, sitaweza kurudi nyumban, daraja limevunjika na kutoka Morogoro kurudi Dar haiwezekani
MAMA:- Mume wangu Morogoro ulienda bila kuniaga!?
BABA:- Ilikuwa ni ghafla sana mke wangu, sikuweza kukwambia..
MAMA:- khaa! Sasa watoto nani atawaangalia?!
BABA:- Unasemaje?! We uko wapi kwan?!!
MAMA:- Niko Bagamoyo na daraja limeondolewa na maji sitaweza kurudi.
BABA:- Unasemaje we mwanamke?! Nakwambia nikukute nyumban ndani ya dk 15..
Baada ya dk 15 Baba kafika nyumbani.
MAMA:- Haya, umefikaje kutoka Morogoro?
BABA:- Nimepewa lift na helkopta ya Mbowe😊
 

Kasuku​

Kasuku alisimama mlango wa kuingia supermarket wakapita wanawake watatu...
Kasuku: nyeupe, nyekundu, kijani.
Wale wanawake wakatatizika, baada ya muda wakajua ni chupi walizovaa. Wakasema basi kesho tubadilisheni..
Siku ya pili wakapita tena..
Kasuku: nyeusi, manjano, zambarau.
Loh! Wanawake hoi.. wakastaajabu sana...
Wakasema lazima wamshinde yule kasuku kwa hekima.
Wakaambiana basi kesho tusivae chupi tuone kama ni kweli anaona mpaka ikulu ndani.
Siku ilipowadia wakapita mbele ya kasuku tena..
Kasuku:- kipilipili, kipara, rasta 😎
Wanawake wakasemezana, wakaafikiana kutorejea tena kwa ile supermarket!!!
 
Acheni tu daah
sxc.jpg
 
Back
Top Bottom