Muadhama Profesa Emeritus Askofu Mkuu Dkt. Desmond Mpilo Tutu wa Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90! Askofu Mkuu Desmond Tutu alikuwa ni Askofu Mkuu wa Jimbo la Capetown na Mkuu wa Kanisa Anglikana Kusini mwa Afrika wakati wa utawala wa Ubaguzi wa Rangi nchini Afrika Kusini. Huyo ndiye aliyekuwa nguvu ya kimaadili katika mapambano ya ha haki na pia sauti ya Kanisa na dhamiri ya Mungu nchini Afrika Kusini wakati wa miaka ya giza!
Askofu Mkuu Tutu Atakumbukwa kwa jinsi alivyohatarisha maisha yake katika kutetea haki na kupambana na Mfumo wa Ubaguzi wa Rangi (Apartheid). Yeye hakuona aibu na wala hakuogopa hatari ya kuongozana na wapigania Uhuru wa Afrika Kusini wakati ule ambapo viongozi wengine wa Kanisa walikumbatia utawala wa kikandamizaji kwa maslahi binafsi. Atakumbukwa pia kwa ujasir wa kuongoza maandamano makubwa mjini Johannesburg!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula