Tulipata ugeni ofisini kwetu miaka fulani,walikuwa watu wa Asia ambao hata wao kiingereza hakipandi vizuri
Ila mmoja wao alikuwa ni black kama sisi.ila hakuwa mzungumzaji sana
Kumbe yeye anajua lugha kuliko wenzie ila ananichora tu mi najua hajui
Basi bwana,katika siku zote tatu walizokaa tuliongea mengi kuhusu mipango yetu ya kiofisi na tulielewana vizuri tu
Basi siku ya mwisho tunaagana yule black mwenye asili ya kihabeshi aliniambia
Umejitahidi sana ila Kuna haya maneno sijakusikia ukitaja na hayaepukiki
Which,whose,whom,while, when,while n.k
Nilijisikia aibu sana hasa ukizingatia ndiyo tuliyo karirishwa mashuleni huko
